Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • nwt uku. 2022-2023
  • B1 Ujumbe wa Biblia

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • B1 Ujumbe wa Biblia
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kisha 4026 M.K.Y.
  • 1943 M.K.Y.
  • Kisha 1070 M.K.Y.
  • 29 K.K.Y.
  • 33 K.K.Y.
  • Karibu 1914 K.K.Y.
  • Wakati Wenye Kuja
  • Unabii wa Zamani Wenye Unakuhusu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Yehova Anafunua Kusudi Lake
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Kwa Nini Ni Muhimu Kujua Yaliyotukia Edeni?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Mungu Ana Kusudi Gani juu ya Dunia?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
B1 Ujumbe wa Biblia

B1

Ujumbe wa Biblia

Maandishi

Yehova Mungu iko na haki ya kutawala. Namna yake ya kutawala ndiyo ya muzuri zaidi. Kusudi lake kwa ajili ya dunia na kwa ajili ya wanadamu litatimia.

Adamu na Eva Katika Bustani ya Edeni na nyoka akiwa karibu nao

Kisha 4026 M.K.Y.

“Nyoka” anatilia mashaka haki ya Mungu ya kutawala na namna yake ya kutawala. Yehova anaahidi kutokeza “uzao,” ao “mbegu,” wenye mwishowe utamuponda nyoka, ni kusema, Shetani. (Mwanzo 3:1-5, 15, maelezo ya chini) Lakini, Yehova anaachia wanadamu wakati ili wajitawale wakiongozwa na nyoka.

Abrahamu anasikiliza ahadi ya Mungu

1943 M.K.Y.

Yehova anamuambia Abrahamu kwamba “uzao” wenye uliahidiwa utakuwa mumoja wa wazao wake.—Mwanzo 22:18.

Mufalme Daudi

Kisha 1070 M.K.Y.

Yehova anamuhakikishia Mufalme Daudi na kisha mwana wake Sulemani kwamba “uzao” wenye uliahidiwa ungetokea katika kizazi chao.—2 Samweli 7:12, 16; 1 Wafalme 9:3-5; Isaya 9:6, 7.

Yesu wakati wa ubatizo wake

29 K.K.Y.

Yehova anamutambulisha Yesu kuwa “uzao” wenye uliahidiwa ambao ni Muriti wa kiti cha ufalme cha Daudi.—Wagalatia 3:16; Luka 1:31-33; 3:21, 22.

Yesu wakati wa kifo chake

33 K.K.Y.

Nyoka, ni kusema Shetani, anaumiza kwa wakati mufupi “uzao” wenye uliahidiwa kwa kumufanya Yesu auawe. Yehova anamufufua Yesu kwenye uzima mbinguni na anakubali samani ya uzima mukamilifu wa Yesu, hilo linatoa musingi wa kusamehe zambi na kupatia wazao wa Adamu uzima wa milele.—Mwanzo 3:15; Matendo 2:32-36; 1 Wakorinto 15:21, 22.

Nyoka, ni kusema, Shetani, anatupwa kwenye dunia kama vile iliahidiwa katika Ufunuo

Karibu 1914 K.K.Y.

Yesu anamutupa nyoka, ni kusema, Shetani, katika dunia, ­anamuzuia katika dunia kwa wakati mufupi.—Ufunuo 12:7-9, 12.

Yesu akitawala dunia kutokea kiti chake cha ufalme mbinguni kama vile iliahidiwa katika Ufunuo

Wakati Wenye Kuja

Yesu anamutia Shetani katika kifungo kwa miaka elfu (1000) na ­kisha anamuharibu, kwa njia hiyo anamuponda kichwa kwa njia ya mufano. Kusudi la kwanza kabisa la Yehova kwa ajili ya dunia na kwa ajili ya wanadamu linatimizwa, jina lake linaondolewa lawama, na namna yake ya kutawala inatetewa.—Ufunuo 20:1-3, 10; 21:3, 4.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine