Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g 11/13 uku. 16
  • Wewe, Una “Karamu Sikuzote”?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Wewe, Una “Karamu Sikuzote”?
  • Amuka!—2013
  • Habari za Kufanana na Zile
  • 4 | Ulinde Tumaini Yako
    Amuka!—2022
  • Muache Kuhangaika
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Shangwe—Sifa Yenye Tunapata Kutoka kwa Mungu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
  • Mawazo Yako Ni ya Maana Sana!
    Amuka!—2016
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2013
g 11/13 uku. 16

Wewe, Una “Karamu Sikuzote”?

‘Siku zote za mwenye kuteseka ni mbaya, lakini mutu aliye muchangamufu moyoni ana karamu sikuzote.’​—Methali 15:15.

MANENO hayo yanamaanisha nini? Yanamaanisha hali ya mutu ya moyoni na ya akilini. Mutu “mwenye kuteseka” anakazia akili mambo mabaya, mutazamo huo unafanya siku zake ziwe “mbaya,” ao zenye kuhuzunisha. Lakini, ‘mutu aliye muchangamufu moyoni’ anajaribu kukazia akili mambo mazuri, mutazamo huo unachochea furaha ya moyoni, na hilo linamufanya awe na “karamu sikuzote.”

Sisi wote tuna magumu ambayo yanaweza kutufanya tupoteze furaha kwa kadiri fulani. Hata hivyo, tunaweza kufanya mambo fulani ambayo yanatusaidia kubaki na furaha yetu wakati wa magumu. Ona mambo ambayo Biblia inasema.

  • Usiache mahangaiko ya kesho yakulemee. Yesu Kristo alisema hivi: “Msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake.”​—Mathayo 6:34, Union Version.

  • Jaribu kukazia akili mambo mazuri ambayo yamefanyika katika maisha yako. Kwa kweli, wakati unashuka moyo, unaweza kuandika mambo hayo mazuri na kuyafikiria. Pia, usifikirie sana makosa ao mambo mabaya uliyofanya wakati uliopita. Ujifunze kutokana na mambo hayo, na uendelee mbele. Uwe kama mutu anayetembeza motokari ambaye anatupa jicho katika kioo cha motokari cha kuangalia nyuma lakini hakazie uangalifu katika kioo hicho. Kumbuka pia kwamba Mungu ‘anasamehe kwa njia kubwa.’​—Isaya 55:7.

  • Wakati mahangaiko yanakulemea, uzungumuze na mutu fulani ambaye anaweza kukutia moyo. Andiko la Methali 12:25 linasema hivi: “Hangaiko” linafanya moyo wetu ‘uiname, lakini neno njema linaufanya ushangilie.’ Hilo ‘neno njema’ linaweza kutoka kwa mutu wa familia yetu ao rafiki mwenye kutumainika, ni kusema, mutu fulani mwenye kujali wengine ao aliye na maoni mazuri, ambaye “anapenda nyakati zote.”​—Methali 17:17.

Maneno ya hekima yaliyo katika Biblia yamesaidia watu wengi kupata furaha zaidi katika maisha, hata wanapokuwa na magumu. Maneno hayo mazuri na yakusaidie wewe pia.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine