HABARI FULANI ZA ULIMWENGU
Hispania
Kikundi kimoja cha wanasayansi kinaamini kwamba pengine jambo ambalo wanadamu walifanya ndilo lilichochea kutokea kwa tetemeko la inchi la mwaka wa 2011 lililoua watu kenda na kuumiza watu wengi katika muji wa Lorca, kusini mwa inchi ya Hispania. Watu wanaojifunza mambo ya udongo waliona kuwa kuna uhusiano kati ya tetemeko hilo lenye kuua na nafasi ambapo watu walichimba ili kupata maji mengi ya kumwangia katika mashamba.
China
Watembeaji kutoka China walitumia dolare miliare 102 za Amerika juu ya kusafiri katika inchi mbalimbali mwaka wa 2012. Kulingana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Utalii (ao matembezi), kwa mara ya kwanza hesabu hiyo ilifanya inchi ya China ichukue nafasi ya kwanza kati ya inchi zinazotumia feza nyingi ili kufanya matembezi katika inchi mbalimbali. Inchi ya China ilichukua nafasi ya kwanza mbele ya inchi ya Ujerumani iliyotumia dolare miliare 84 na inchi ya Amerika iliyotumia dolare miliare 83.
Japani
Gazeti la matunzo la Uingereza (BMJ) lilitoa ripoti ya uchunguzi uliofanywa juu ya watu karibu 68 000 katika inchi ya Japani waliokuwa na miaka 23 kwa kukadiria. Wachunguzi walivumbua kwamba wanawake waliozaliwa kati ya mwaka wa 1920 na 1945 ambao walianza kuvuta tumbaku mbele ya kueneza miaka 20 walikufa miaka kumi hivi mbele ya wale ambao hawajavuta tumbaku hata siku moja; wanaume walikufa miaka munane mbele.
Moritania
Ili kulinda wanyama wanaoishi katika bahari na wanyama wa inchi kavu, inakatazwa kuingiza katika inchi, kutengeneza, na kutumia mifuko ya plastiki, kwa sababu wanyama wanaweza kufa wakikula mifuko hiyo. Serikali inapendekeza kutumia mifuko inayoweza kuoza kuliko kutumia mifuko ya plastiki.
Ulimwengu
Mashirika ya bima (assurance) yanatumia dolare miliare 50 za Amerika kila mwaka ili kulipia hasara ao uharibifu wa vitu unaotokezwa na hali mbaya ya hewa. Kuanzia mwaka kati ya 1981 na 1990, malipo hayo yameongezeka mara mbili kila miaka kumi kwa sababu ya kupanda kwa bei ya vitu.