Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g 3/14 uku. 4-7
  • Habari ya Uumbaji Yenye Watu Wengi Hawajue

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Habari ya Uumbaji Yenye Watu Wengi Hawajue
  • Amuka!—2014
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MUUMBAJI AMBAYE HAKUUMBWA
  • MUNGU ALITUMIA MUDA GANI ILI KUUMBA ULIMWENGU?
  • MUNGU ALITUMIA MAGEUZI?
  • UUMBAJI UNAONYESHA KWAMBA KUNA MUUMBAJI
  • Mambo Yenye Biblia Inatuambia
    Amuka!—2021
  • Uumbaji
    Amuka!—2014
  • Mashahidi wa Yehova Wanaamini Kama Mungu Aliumba Mbingu na Dunia kwa Siku Sita Zenye Urefu wa Saa 24?
    Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana Juu ya Mashahidi wa Yehova
  • Vitu Vyenye Uzima Vilianza Namna Gani?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2014
g 3/14 uku. 4-7
Ulimwengu

KICHWA

Habari ya Uumbaji Yenye Watu Wengi Hawajue

MAMILIARE ya watu wamesoma ao kusikia mambo yenye Biblia inasema juu ya mwanzo wa ulimwengu. Habari hiyo yenye imefanya miaka 3 500 inaanza na maneno haya yenye kujulikana sana: “Hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia.”

Hata hivyo, watu wengi hawajue ukweli wa kwamba viongozi wa dini zinazojiita kuwa za Kikristo, kutia ndani wanauumbaji (watu wanaoamini kwamba ulimwengu uliumbwa katika kipindi cha siku sita za saa 24 kila moja) na watu wenye imani kali ya kidini wamegeuza habari ya Biblia juu ya uumbaji na wameifanya kuwa hadisi nyingi za kuwazia zisizopatana na mambo Biblia inasema kabisa. Hadisi hizo hazipatane na mambo ya hakika yenye sayansi inasema. Hata ikiwa hadisi hizo hazipatikane katika Biblia, zimefanya watu fulani waone Biblia kuwa kitabu cha hadisi za kutunga tu.

Watu wengi hawajue habari ya kweli ya Biblia juu ya uumbaji. Hilo ni jambo la haya kabisa, kwa sababu Biblia inatoa maelezo yenye kupatana na akili na yenye kuaminika kuhusu mwanzo wa ulimwengu. Zaidi ya hilo, habari ya Biblia juu ya uumbaji inapatana na mambo yenye sayansi imevumbua. Kwa kweli, utafurahi na kushangazwa na habari ya Biblia juu ya uumbaji yenye watu wengi hawajue!

MUUMBAJI AMBAYE HAKUUMBWA

Bila mwanzo wala mwisho

Habari ya Biblia juu ya uumbaji inategemea ukweli wa kwamba kuna Mutu Mukubwa Zaidi, Mungu Mweza​-Yote, aliyeumba vitu vyote. Mutu huyo ni nani, na ana mwili wa namna gani? Biblia inaonyesha kwamba yeye ni tofauti kabisa na miungu inayoabudiwa na watu wengi na inayoabudiwa katika dini kubwa​-kubwa. Yeye ndiye Muumbaji wa vitu vyote, lakini watu wengi hawajue mambo mengi kumuhusu.

  • Mungu ni mutu anayeishi kwelikweli. Yeye si nguvu tu yenye haina mwili, inayoenda huku na huku katika ulimwengu wote bila kusudi. Ana mawazo, anaweza kufurahi ao kukasirika, na anaweza kukusudia kufanya jambo fulani.

  • Mungu ana nguvu na hekima isiyo na mipaka. Hiyo ndiyo sababu katika uumbaji wote kuna vitu vilivyoumbwa kwa njia isiyoeleweka, zaidi sana katika vitu vilivyo na uzima.

  • Mungu aliumba vitu vyote vinavyoonekana. Kwa hiyo, haingewezekana afanyizwe kutokana na vitu hivyo tunavyoona ambavyo yeye mwenyewe aliumba. Lakini, yeye ni mutu wa roho, hana mwili wa nyama na damu.

  • Mungu ni wa milele na milele. Amekuwa sikuzote na ataendelea kuwa. Kwa hiyo, hakuna mutu alimuumba.

  • Mungu ana jina lake la pekee, jina hilo linatumiwa mara maelfu katika Biblia. Jina hilo ni Yehova.

  • Yehova Mungu anapenda wanadamu na anawahangaikia.

MUNGU ALITUMIA MUDA GANI ILI KUUMBA ULIMWENGU?

Upande wa mbele wa saa

Biblia inasema kwamba Mungu aliumba “mbingu na dunia.” Lakini, maneno hayo yasiyo na maelezo mengi hayaonyeshe urefu wa wakati wala ufundi mbalimbali ambao Mungu alitumia ili kuumba ulimwengu. Tuseme nini juu ya wazo linaloenea sana la wanauumbaji wanaoamini kwamba Mungu aliumba ulimwengu wote kwa siku sita za saa 24 kila moja? Wazo hilo, ambalo wanasayansi wengi wanapinga, linategemea kutoelewa habari ya Biblia juu ya uumbaji. Fikiria mambo yenye Biblia inasema kabisa.

Biblia haiunge mukono mafundisho ya watu wenye imani kali ya dini na ya wanauumbaji, wanaosema kwamba siku za uumbaji zilikuwa siku za saa 24 kila moja

  • Biblia haiunge mukono mafundisho ya watu wenye imani kali ya dini na ya wanauumbaji, wanaosema kwamba siku za uumbaji zilikuwa siku za saa 24 kila moja.

  • Biblia inatumia mara nyingi neno “siku” ili kuonyesha vipindi mbalimbali vya wakati. Katika hali fulani, vipindi hivyo vina urefu usiojulikana. Mufano moja wa jambo hilo ni habari ya uumbaji inayozungumuziwa katika kitabu cha Biblia cha Mwanzo.

  • Katika habari hiyo ya Biblia, pengine kila siku moja ya uumbaji kati ya siku hizo sita ilikuwa na urefu wa maelfu ya miaka.

  • Wakati siku ya kwanza ya uumbaji ilianza Mungu alikuwa tayari ameumba ulimwengu, kutia ndani sayari dunia yenye haingewezesha kitu chochote kuishi.

  • Inaonekana kwamba siku hizo sita za uumbaji vilikuwa vipindi virefu ambamo Yehova Mungu alitayarisha dunia ili iwe makao ya wanadamu.

  • Habari ya Biblia juu ya uumbaji haipingane na mambo yenye wanasayansi wanasema juu ya miaka yenye ulimwengu umekwisha kufanya.

MUNGU ALITUMIA MAGEUZI?

Hatua ya mageuzi ya kuwazia​-wazia tu

Watu wengi wasioamini Biblia wanakubali wazo la kwamba vitu vilivyo na uzima vilitokana na kemikali zisizo na uzima zilizogeuka​-geuka kupitia hatua zisizojulikana na zisizo na kusudi lolote. Inaonekana kwamba kwa kadiri fulani, viumbe wanaofanana na bakteria walijifanya upya, na pole kwa pole wakajigawanya na kutokeza aina zote ambazo ziko leo. Hilo linaweza kumaanisha kwamba mwishowe mwili wa mwanadamu ulio mugumu kueleweka ulitokana na bakteria.

Fundisho hilo la mageuzi linakubaliwa pia na watu wengi wanaosema kwamba wanaamini Biblia kuwa ni neno la Mungu. Wanaamini kwamba Mungu alitokeza uzima wa kwanza duniani kisha hapo akaendelea tu kuchunguza na kufuatilia hatua za mageuzi ao labda kuziongoza. Lakini, Biblia haiseme hivyo.

Habari ya Biblia juu ya uumbaji haipingane na mambo yenye sayansi imevumbua, kwamba mabadiliko yanatokea katika aina fulani ya viumbe

  • Kulingana na Biblia, Yehova Mungu aliumba aina zote za kwanza​-kwanza za mimea na wanyama, na pia aliumba mwanaume na mwanamuke waliokuwa wakamilifu na waliokuwa na uwezo wa kujijua, wakiwa na upendo, hekima, na haki.

  • Ni wazi kwamba aina za wanyama na mimea ambazo Mungu aliumba zimebadilika na zimetokeza aina zingine ndani ya aina hizo zenyewe. Katika hali nyingi, aina za uzima zinazotokezwa zinatofautiana kati yazo.

  • Habari ya Biblia juu ya uumbaji haipingane na mambo yenye sayansi imevumbua, kwamba mabadiliko yanatokea katika aina fulani ya viumbe.

UUMBAJI UNAONYESHA KWAMBA KUNA MUUMBAJI

Katika mwaka wa 1850 hivi, mwanabiolojia Mwingereza Alfred Russel Wallace alikubaliana na Charles Darwin juu ya fundisho la mageuzi la kwamba viumbe vilivyo na uzima vinaishi ikiwa ni vyenye nguvu ao vinakufa ikiwa ni zaifu kulingana na namna vinajipatanisha na mazingira. Lakini, mwanamageuzi huyo mwenye kujulikana sana alisema hivi: “Wale ambao wana macho ya kuona na akili iliyozoezwa kufikiri wanapaswa kutambua kwamba ndani ya chembe ndogo, ndani ya damu, katika dunia yote, na kuzunguka ulimwengu wetu . . . , kuna muongozo wenye akili na ufahamu; kwa kifupi, kuna Mutu mwenye akili.”

Karibu miaka elfu mbili mbele ya Wallace, Biblia ilikuwa tayari imesema hivi: ‘Kwa maana sifa [za Mungu] ambazo hazionekane, zinaonekana waziwazi tangu kuumbwa kwa ulimwengu na kuendelea, kwa sababu zinaeleweka kwa vitu vilivyofanywa, yaani, nguvu zake za milele na Uungu.’ (Waroma 1:20) Mara kwa mara, unaweza kuchukua wakati ili kufikiria vitu vizuri ajabu vinavyopatikana katika mazingira, kuanzia unyasi mudogo mupaka kufikia nyota na sayari nyingi zinazojaa katika ulimwengu. Kwa kuchunguza uumbaji, unaweza kuona kwamba kuna Muumbaji.

Unaweza kuuliza hivi: ‘Lakini ikiwa kuna Mungu mwenye upendo aliyeumba vitu vyote, sababu gani anaacha watu wateseke? Je, ameacha viumbe vyake vya duniani? Wakati unaokuja utakuwa namna gani?’ Biblia ina habari zingine nyingi za kweli ambazo watu wengi hawaelewe. Habari hizo zimefichwa kwa sababu ya mawazo ya wanadamu na mafundisho ya dini nyingi, na kwa hiyo, watu wengi hawazijue. Wachapishaji wa gazeti hili, ni kusema, Mashahidi wa Yehova, watafurahi kukusaidia uchunguze kweli ya Biblia isiyochanganywa na mawazo ya watu na watakusaidia ujifunze mengi zaidi juu ya Muumbaji na namna maisha ya wanadamu ambao aliumba yatakuwa wakati unaokuja.

NAMNA MATUKIO YA UUMBAJI YALIVYOFUATANA

  • MWANZO

    Mbingu na dunia vinaumbwa.​—Mwanzo 1:1.

  • Dunia isiyo na umbo na yenye giza

    GIZA

    Dunia isiyokuwa na umbo, ukiwa, na yenye giza.​—Mwanzo 1:2.

  • Siku ya 1: nuru; muchana na usiku

    SIKU YA KWANZA

    Nuru inayotawanyika inapenya ao kupita ndani ya anga​-hewa la dunia. Ikiwa kungekuwa mutu duniani mbele ya hapo, hangeona jua, mwezi na nyota. Lakini sasa, kukakuwa tofauti kati ya usiku na muchana.​—Mwanzo 1:3-5.

  • Siku ya 2: nafasi iliyo wazi

    SIKU YA PILI

    Dunia inafunikwa na maji na muvuke mukubwa. Vitu hivyo viwili vinatenganishwa, na hivyo kukakuwa nafasi iliyo wazi kati ya maji na muvuke. Biblia inaeleza nafasi hiyo iliyo wazi kuwa ‘anga kati ya maji’ na inaiita “Mbingu.”​—Mwanzo 1:6-8.

  • Siku ya 3: inchi kavu na mimea

    SIKU YA TATU

    Maji yanapunguka na inchi kavu inatokea. Anga-hewa inakuwa wazi ili kuruhusu mwangaza zaidi wa jua ufike kwenye udongo. Mimea fulani inatokea, na aina zingine mupya za mimea zinaendelea kutokea katika siku ya tatu na katika siku zingine za uumbaji zilizofuata.​—Mwanzo 1:9-13.

  • Siku ya 4: Jua, mwezi, na nyota

    SIKU YA INE

    Jua na mwezi vinaanza kuonekana duniani.​—Mwanzo 1:14-19.

  • Siku ya 5: samaki na ndege

    SIKU YA TANO

    Mungu anaumba viumbe wengi wanaoishi katika bahari na viumbe wengi wanaoruka wakiwa na uwezo wa kuzaana kati ya aina zao.​—Mwanzo 1:20-23.

  • Siku ya 6: wanyama wa inchi kavu na wanadamu

    SIKU YA SITA

    Wanyama wa inchi kavu wanaumbwa, wakubwa na wadogo. Siku hiyo ilimalizika kwa kazi ya ufundi mukubwa zaidi ya uumbaji wa Mungu duniani, maana yake, mwanaume na mwanamuke wa kwanza.​—Mwanzo 1:24-31.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine