KICHWA | SABABU GANI UENDELEE KUISHI?
Sababu ya 3 Kuna Tumaini
“Wapole wataimiliki dunia, nao watapata furaha yao tele katika wingi wa amani.”—ZABURI 37:11.
Biblia inaonyesha kwamba maisha ni ‘yenye kujaa musukosuko.’ (Ayubu 14:1) Leo, kila mutu anaweza kupatwa na tatizo la aina fulani ao nyingine. Lakini watu fulani wanapoteza kabisa tumaini juu ya maisha yao, wanaona sawa vile tatizo lao haliwezi kutatuliwa na hawana tumaini kwa ajili ya wakati unaokuja. Wewe pia unajisikia hivyo? Ikiwa jibu lako ni ndiyo, ukuwe na uhakika kwamba Biblia inatoa tumaini la kweli, si kwako tu lakini pia kwa wanadamu wote. Kwa mufano:
Biblia inafundisha kwamba Yehova Mungu alikusudia tuwe na maisha mazuri sana.—Mwanzo 1:28.
Yehova Mungu anaahidi kuifanya dunia yetu iwe paradiso.—Isaya 65:21-25.
Ahadi hiyo itatimia hakika. Andiko la Ufunuo 21:3, 4 linasema hivi:
“Hema la Mungu liko pamoja na wanadamu, naye atakaa pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Na Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao. Naye atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.”
Tumaini hilo si ndoto tu. Yehova Mungu anakusudia kabisa kulitimiza, ana nguvu na anapenda kabisa kufanya hivyo. Tumaini ambalo Biblia inatutolea ni lenye kutegemeka, na linatupatia jibu nzuri la ulizo “Sababu gani uendelee kuishi?”
UKUMBUKE JAMBO HILI: Hata ikiwa namna unajisikia moyoni inaweza kuyumba-yumba kama mashua iliyo katika bahari yenye upepo, habari ya Biblia ya tumaini inaweza kuwa kama vile nanga ya kukufanya uendelee kutulia.
JAMBO UNALOWEZA KUFANYA SASA: Uanze kuchunguza mambo Biblia inafundisha juu ya tumaini la kweli la wakati unaokuja. Mashahidi wa Yehova watafurahi kukusaidia. Unaweza kuwapata katika eneo lenu ao kupata habari ya kukusaidia kwenye adresi yao ya Internete, jw.org.a
a Pendekezo: Fungua adresi yetu jw.org na ufungue kichwa VICHAPO > MAKTABA KWENYE INTERNETE. Kisha, tafuta maneno makubwa kama vile “kushuka moyo” ao “kujiua,” ili kupata musaada zaidi.