Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g 6/14 uku. 3
  • Habari Fulani za Ulimwengu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Habari Fulani za Ulimwengu
  • Amuka!—2014
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • China
  • Ulimwengu
  • Kanada
  • Irelandi
  • Maulizo ya Wasomaji Wetu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Ndoa ya Mashahidi wa Yehova Inakuwaka Namna Gani?
    Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana Juu ya Mashahidi wa Yehova
Amuka!—2014
g 6/14 uku. 3

HABARI FULANI ZA ULIMWENGU

China

Bibi na bwana ambao wameachana

Hesabu ya watu wanaovunja ndoa katika muji wa Beijing iliongezeka kufikia 41 juu ya 100 katika kipindi cha miezi kenda ya kwanza ya mwaka wa 2013 ikilinganishwa na kipindi hichohicho katika mwaka wa 2012. Wachunguzi wanaamini kwamba inawezekana kuongezeka huko kumekuwa kwa sababu watu wenye kuoana wanajaribu kuepuka kulipa kodi ya 20 juu ya 100 ambayo wale wanaouzisha nyumba zao wanaombwa. Katika hali fulani kodi inapunguzwa kwa watu wanaovunja ndoa wakati wanauzisha nyumba ya pili.

Ulimwengu

Sahani ya vidudu vivyoliwa

Umoja wa Mataifa umeshauri kwamba ikiwa watu wengi zaidi wanakula vidudu, hilo litasaidia kumaliza shida ya kukosa kula chakula kinachojenga mwili. Ripoti ya hivi karibuni inasema kwamba kwa sababu vidudu vina protini nyingi na vinapata protini hiyo wakati vinakula vitu visivyokuliwa na watu, vidudu vinavyokuliwa vinaweza “kusaidia wale ambao hawana uwezo wa kupata nyama.” Lakini, ripoti hiyo inaonyesha pia kama “watu wa jamii fulani wanachukia sana kula vidudu.”

Kanada

Viini vyenye kugandishwa vilivyo hai

Hospitali ambazo zinawapatia dawa watu walio na magumu ya kuzaa zinakosa mahali pa kutia viini vilivyogandishwa (mbegu za uzazi za mwanaume na mwanamuke ambazo zimeunganishwa na kugandishwa) ambavyo wenye viini hivyo hawajulikane tena. Inasemekana kwamba hospitali moja inaweka viini 1000 vilivyogandishwa na ambavyo vinaendelea kuishi na wenye viini hivyo “wamekosekana kabisa.”

Irelandi

Biro ya mambo ya ndoa ya  watu wasiojaoli mambo ya dini

Wakatoliki ambao wanaoana katika inchi ya Irelandi walipaswa kuchagua ikiwa wataoana katika kanisa ao katika biro ya mukubwa wa serikali mupaka mwaka wa 2013, wakati watu walianza kupendelea ndoa ambayo inasimamiwa na kikundi cha watu wasiojali mambo ya dini. Kulingana na ripoti ya shirika la habari la Reuters, “maombi ambayo haijajibiwa ya watu wanaotaka kuandikisha ndoa zao kwa serikali tu lakini ambao wanakataa kufanya arusi za kidini wametokeza uhitaji mukubwa” kwa wafanyakazi wa biro mupya ya watu wasiojali mambo ya dini.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine