Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g 7/14 uku. 5
  • Unapoteza Vitu Vyako Vyote

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Unapoteza Vitu Vyako Vyote
  • Amuka!—2014
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • NAMNA YA KUPAMBANA NA MUSIBA
  • Wakati Musiba Unatokea
    Amuka!—2014
  • Kazi ya Kutolea Ndugu Misaada Wakati wa Magumu
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Mashahidi wa Yehova Wanasaidiaka Wale Wenye Wanafikiwa na Misiba?
    Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana Juu ya Mashahidi wa Yehova
  • Mutu Ambaye Unapenda Anakufa
    Amuka!—2014
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2014
g 7/14 uku. 5
Mabomoko kisha tetemeko la inchi na tsunami

KICHWA WAKATI MUSIBA UNATOKEA—UNAWEZA KUFANYA NINI?

Unapoteza Vitu Vyako

Siku ya Tano, tarehe 11 Mwezi wa 3, 2011, kulikuwa tetemeko lenye kipimo cha 9.0 kwenye Richter huko Japani. Watu zaidi ya 15000 walikufa na vitu vinavyoweza kuuzwa kwa dola miliare 200 za Amerika viliharibika. Kisha kuonywa mbele ya wakati kuhusu tsunami, mutu mumoja anayeitwa Kei mwenye miaka 32 alikimbilia mahali palipoinuka. Anasema hivi: “Siku iliyofuata asubuhi nilirudi nyumbani ili kukamata vitu ambavyo ningeweza kubeba, lakini maji yalikuwa yameteremusha vitu vyote ndani ya bahari, na hata nyumba yangu. Musingi wa nyumba tu ndiyo ulibaki.”

Kei

“Sikuelewa mara moja kwamba sikupoteza tu vitu fulani, lakini vitu vyangu vyote. Motokari yangu; ordinatere yangu ya kazi, meza, viti, na kiti aina ya sofa ambacho nilitumia ili kuwakaribishia watu, kibodi, gitari kubwa, gitari ndogo, filimbi; vifaa ninavyotumia ninapofanya kazi na rangi, mafuta, na chokaa; michoro na picha ambazo nilifanya, vyote hivyo vilipotea.”

NAMNA YA KUPAMBANA NA MUSIBA

Jaribu kukaza akili juu ya vitu ulivyo navyo kuliko vile ambavyo ulipoteza. Biblia inasema: ‘Hata wakati mutu ana vitu vingi uzima wake hautokane na vitu alivyo navyo.’ (Luka 12:15) Kei anakumbuka hali yake: “Mwanzoni, niliandika oroza ya vitu ambavyo nilihitaji, lakini kuandika vitu hivyo kulifanya nikumbuke vitu ambavyo nilipoteza. Niliamua kuandika tu kwenye oroza hiyo vitu ambavyo nilihitaji kabisa, na kadiri mahitaji yangu yalishugulikiwa, nilibadilisha mambo fulani kwenye oroza hiyo. Kufanya hivyo kulinisaidia kupanga tena maisha yangu.”

Kuliko kujitenga na wengine, wafariji wengine kupitia mambo ambayo umekwisha kujionea. Kei anasema hivi: “Nilipata misaada kutoka kwa marafiki na mashirika ya kutoa misaada, lakini wakati nilizoea kupata misaada, nilianza kujiona wa bure. Kwa hiyo, nilifikiria maneno ya andiko la Matendo 20:35 ambalo linasema ‘kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.’ Kwa sababu sikuwa na uwezo wa kuwatolea wale ambao walipatwa na musiba musaada wa kimwili, niliamua kuwafariji. Kuonyesha ukarimu kwa njia hii kulinisaidia sana.”

Usali kwa Mungu ili akupe hekima ya kupambana na musiba. Kei aliamini maneno ya Biblia yanayoonyesha kwamba Mungu “ataielekea sala ya wale waliovuliwa kila kitu.” (Zaburi 102:17) Wewe pia unaweza kumuiga.

Je, ulijua? Biblia ilitabiri kwamba kuna wakati ambao hakutakuwa mutu ambaye atahuzunika kwa sababu ya kupoteza vitu katika musiba wa asili.a—Isaya 65:21-23.

a Ili kujifunza kuhusu kusudi la Mungu juu ya dunia, soma sura ya 3 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? Kitabu hicho kilichapishwa na Mashahidi wa Yehova na kinapatikana kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine