Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g 6/15 uku. 8-9
  • Namna ya Kutia Nguvu Mapatano ya Ndoa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna ya Kutia Nguvu Mapatano ya Ndoa
  • Amuka!—2015
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • TATIZO
  • 1 Kuwa na Azimio
    Amuka!—2018
  • “Ndoa na Iheshimiwe”
    Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
  • Biblia Inasema Nini Juu ya Kuishi Pamoja Mbele ya Kufunga Ndoa?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Je, Biblia Inaweza Kusaidia Familia Yangu Iwe na Furaha?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
Amuka!—2015
g 6/15 uku. 8-9
Bibi na bwana wenye furaha wanatembea katika seluji

MUSAADA KWA FAMILIA | NDOA

Namna ya Kutia Nguvu Mapatano ya Ndoa

TATIZO

Siku ulifanya ndoa, ulifanya kiapo. Katika ahadi hiyo nzito, mulipatana kuishi pamoja maisha yenu yote, ni kusema, mulikusudia kushikamana ninyi wawili na kumaliza magumu yenye yatawapata.

Lakini kisha miaka mingi, matatizo ya ndoa yameharibisha ndoa yenu. Ungali unajisikia kuwa mapatano yenu ni yenye nguvu?

MAMBO UNAPASWA KUJUA

Bibi na bwana wanakaa katika mashua yenye kuwa na nanga

Uone mapatano kuwa nanga ya kusaidia ndoa isitikisike

Mapatano haiko tatizo, lakini yanasaidia kumaliza matatizo. Watu wengi leo hawatumainie mapatano. Watu fulani wanasema kuwa mapatano ni kama kamba yenye kufungia mutu kwenye uamuzi mubaya. Kama vile nanga inasaidia mashua isibebwe na maji, mapatano yanasaidia ndoa yako isitikisike. Mwanamuke mumoja mwenye kuitwa Megan anasema hivi: “Wakati hamusikilizane, jambo moja la muzuri sana juu ya mapatano ya ndoa ni kujua kuwa, kati yenu wawili, hakuna mwenye ataondoka.”a Kuwa na uhakika kuwa ndoa iko salama, hata ikiwa kuna magumu fulani, kunaweza kuwasaidia kumaliza magumu yenu.—Soma kisanduku “Mapatano na Ushikamanifu.”

Jambo la maana: Ikiwa uko na magumu katika ndoa yako, huu ndio wakati wa kutia nguvu mapatano yenu ya ndoa, kuliko kuwa na mashaka juu ya mapatano hayo. Namna gani unaweza kufanya hivyo?

MAMBO UNAWEZA KUFANYA

Chunguza mawazo yako. “Ndoa ni ya maisha yote.” Maneno hayo yanakufanya ujisikie kama mufungwa ao yanakufanya ujisikie salama? Wakati magumu yanatokea, kila mara unawaza kuwa kumuacha bibi ao bwana yako ndiyo njia ya muzuri ya kuyamaliza? Ili kutia nguvu mapatano yenu ya ndoa, ni jambo la lazima uone ndoa kuwa muungano wa maisha yote.—Kanuni ya Biblia: Mathayo 19:6.

Chunguza maisha yako ya zamani. Unaweza kuwa na mawazo mabaya juu ya mapatano ya ndoa kwa sababu ya mambo uliona kwa wazazi wako. Mwanamuke mumoja mwenye kuitwa Lea anasema hivi: “Wazazi wangu walivunja ndoa yao wakati nilikuwa ninakomaa. Pengine jambo lenye liliwafikia linanifanya nikuwe na mawazo mabaya juu ya mapatano.” Ukuwe hakika kuwa, katika ndoa yako, unaweza kufanya mambo tofauti na wazazi wako. Haulazimike kurudilia makosa ya wazazi wako!—Kanuni ya Biblia: Wagalatia 6:4, 5.

Chunguza maneno yako. Wakati hausikilizane na bibi ao bwana yako, usiseme maneno yenye utahuzunikia kisha hapo, maneno kama vile “Nitakuacha!” ao “Nitapata mutu mwengine mwenye ananiona kuwa wa lazima!” Maneno kama hayo hayatie nguvu mapatano yenu ya ndoa. Kuliko kumaliza tatizo, yanafanya tu ninyi wawili mujibiane kwa matusi. Usiseme maneno yenye kuumiza, lakini unaweza kusema maneno kama vile: “Kwa kweli, sisi wawili tunakasirika. Namna gani tunaweza kumaliza tatizo hili pamoja?” —Kanuni ya Biblia: Methali 12:18.

Onyesha ‘alama za mapatano.’ Kwenye kazi, tia picha ya bibi ao bwana yako juu ya meza. Sema mambo ya muzuri juu ya ndoa yenu wakati unaongea na wengine. Fanya mupango wa kuita bibi ao bwana yako wakati hamuko pamoja kwa muda murefu. Tumia mara nyingi maneno “sisi,” “mimi na bibi yangu,” ao “mimi na bwana yangu.” Wakati unafanya hivyo, unakazia kwa wengine na kwako mwenyewe kuwa umefanya mapatano ya ndoa.

Tafuta mashauri kwa watu wenye kuonyesha mufano muzuri. Uende kuona bibi na bwana wenye wameweza kupambana na matatizo ya ndoa. Uwaulize, “Munaona namna gani mapatano ya ndoa yenye mulifanya, na namna gani yamewasaidia katika ndoa yenu?” Biblia inasema hivi: ‘Chuma kinanolewa kwa chuma. Ndivyo mutu ananoa uso wa mwingine.’ (Methali 27:17) Ukifuata kanuni hiyo, unaweza kupata faida katika mashauri ya watu wenye wamefanya ndoa yao ikuwe na furaha, sivyo?

a Biblia inaruhusu mutu avunje ndoa ikiwa tu bibi ao bwana yake anafanya uzinifu. Soma habari “Mawazo ya Biblia—Uzinifu” katika Amuka! hii.

MAANDIKO YA LAZIMA

  • ‘Kile ambacho Mungu ameunganisha mutu yeyote asikitenganishe.’—Mathayo 19:6.

  • ‘Kila mumoja ataubeba muzigo wake mwenyewe.’ —Wagalatia 6:5.

  • ‘Kuna mutu anayesema bila kufikiri kama kwa upanga unaochoma, lakini ulimi wa mwenye hekima unaponya.’—Methali 12:18.

Mapatano Na Ushikamanifu

“Ikiwa wewe na bibi ao bwana yako munashikamana, munaweza kufurahia muungano wa maisha yote. Wakati munafikiria miezi na miaka mingi inayokuja, munajiona pamoja. Hamufikirie hata kidogo kuwa hamungepaswa kuoana, na hilo linafanya ndoa yenu ikuwe salama. Mwanamuke mumoja mwenye kuolewa anasema hivi: ‘Hata wakati ninamukasirikia sana [bwana yangu] na kuhuzunika sana juu ya hali yenye imetupata, sihangaike kuwa ndoa yetu itavunjika. Jambo lenye ninahangaikia ni namna tutarudilia hali yetu ya muzuri. Ninaendelea kuwa hakika kama tutamaliza tatizo hilo, hata kama wakati huo sijue namna tutalimaliza.’”—Habari hii inatoka katika gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 15 Mwezi wa 9, 2003.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine