Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g 7/15 uku. 14-15
  • Mambo Unapaswa Kujua Juu ya Malaria

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mambo Unapaswa Kujua Juu ya Malaria
  • Amuka!—2015
  • Vichwa Vidogo
  • 1 MALARIA NI NINI?
  • 2 NAMNA GANI MUTU ANAPATA MALARIA?
  • 3 NAMNA UNAWEZA KUJILINDA
Amuka!—2015
g 7/15 uku. 14-15

Mambo Unapaswa Kujua Juu ya Malaria

Shirika la Afya Ulimwenguni (OMS) linakadiria kuwa, katika mwaka wa 2013, watu zaidi ya milioni 198 walipata ugonjwa wa malaria, na watu karibu 584000 walikufa kwa sababu ya ugonjwa huo. Kati ya kila watu 5 wenye walikufa kwa sababu ya Malaria, watu karibu 4 walikuwa watoto wa chini ya miaka tano. Ugonjwa huo unatesa watu katika inchi na maeneo karibu 100 duniani pote, na kwa hiyo unahatarisha maisha ya watu miliare 3 na milioni 200 hivi.

1 MALARIA NI NINI?

Malaria ni ugonjwa wenye kuletwa na mikrobe yenye inaingizwa katika mwili. Kati ya alama zenye kuonyesha kuwa mutu iko na malaria kuna homa (fièvre), baridi, kutokwa jasho, maumivu ya kichwa, maumivu ya mwili, kichefuchefu (nausée), na kutapika. Wakati fulani, alama za malaria zinaweza kurudia kisha kila saa 48 mupaka 72, kulingana na aina ya mikrobe ya malaria yenye mutu iko nayo ao kulingana na wakati wenye mutu amefanya na ugonjwa huo.

2 NAMNA GANI MUTU ANAPATA MALARIA?

  1. Muchoro wenye kuonyesha namna malaria inaingia katika mwili wa mutu

    Mikrobe ya malaria yenye kuitwa Plasmodia inaingizwa katika damu ya mutu wakati anaumwa na imbu wa kike wa aina ya Anophèles.

  2. Mikrobe hiyo inaingia katika chembe za maini ya mutu, na humo inaanza kuongezeka.

  3. Wakati chembe ya maini inapasuka, mikrobe hiyo inatoka, kisha inashambulia chembe nyekundu za damu. Kisha mikrobe hiyo inaendelea kuongezeka katika chembe nyekundu.

  4. Mikrobe ya malaria inashambulia chembe nyekundu za damu na inafanya zipasuke

    Wakati chembe nyekundu ya damu inapasuka, inatoa mikrobe hiyo, na inashambulia chembe zingine nyekundu.

  5. Chembe nyekundu za damu zinaendelea kushambuliwa na kupasuka. Kwa kawaida mutu anaonyesha alama za malaria kila wakati chembe nyekundu za damu zinapasuka.

3 NAMNA UNAWEZA KUJILINDA

Ikiwa unaishi katika inchi yenye kuwa sana na malaria . . .

  • Utumie mustikere. Mustikere hiyo inapaswa kuwa:

    • yenye kutiwa dawa ya kuua vidudu.

    • bila tundu ao nafasi yenye kupasuka.

    • yenye kuingizwa muzuri chini ya matelas.

  • Tumikisha dawa ya kupulizia katika nyumba ili kuua vidudu.

  • Ikiwezekana, uweke mustikere kwenye milango na madirisha, na utumie mashine za kutia hewa katika nyumba, kwa sababu zinafukuza imbu.

  • Uvae nguo zenye rangi yenye kungaa zenye kufunika muzuri mwili wako.

  • Ikiwa inawezekana, uepuke kuwa nafasi yenye miti ao majani mengi, kwa sababu imbu wengi wanaishi hapo, ao nafasi yenye kuwa na maji yasiyoteremuka kwa sababu wanataga mayai hapo.

  • Ikiwa unapata malaria, utafute matunzo bila kukawia.

Muchoro wenye kuonyesha namna watu na imbu wanaachiana malaria

Mutu anaweza kupata malaria wakati anaumwa na imbu yenye kuwa na mikrobe ya malaria. Vilevile, imbu yenye haina mikrobe ya malaria inaweza kupata mikrobe hiyo ikiwa inauma mutu mwenye kuwa na mikrobe hiyo. Kisha imbu yenye imepata mikrobe ya malaria inaweza kuiachia mutu mwengine

Ikiwa unapanga kusafiri katika inchi yenye kuwa sana na malaria . . .

  • Utafute habari za hivi karibuni mbele ya kusafiri. Aina ya mikrobe ya malaria katika inchi moja inaweza kuwa tofauti na mikrobe yenye kuwa katika inchi ingine, na hilo linasaidia kujua ni dawa gani inaweza kuwa ya muzuri zaidi. Tena, umuulize muganga ni mambo gani unapaswa kujua, kwa kufikiria magonjwa yenye yamekwisha kukupata.

  • Wakati uko katika inchi hiyo, utumikishe mambo yenye kutajwa katika habari hii kwa ajili ya watu wenye kuishi katika inchi zenye kuwa sana na malaria.

  • Ikiwa unapata malaria, utafute matunzo bila kukawia. Ujue kama alama za malaria zinaweza kuonekana juma moja ao juma mbili kisha kupata ugonjwa huo.

MAMBO MENGINE UNAWEZA KUFANYA

  1. Ufuate mipango ya serikali ao mipango mingine ya eneo lenu kwa ajili ya afya.

  2. Ununue dawa kwa watu wenye kuwa na ruhusa ya kuuzisha dawa. (Dawa za mubaya ao za uongo zinaweza kufanya ugonjwa uendelee kwa muda murefu, ao zinaweza kuongeza hatari ya kufa.)

  3. Usafishe kila nafasi penye imbu wanaweza kutagia mayai karibu-karibu na nyumba yako.

Ikiwa unaishi katika eneo lenye kuwa na malaria, ao ikiwa ulikuwa katika eneo kama hilo, usizarau alama hizi za malaria . . .

  • Kupanda kwa joto ya mwili (fièvre)

  • Kutokwa jasho

  • Kutetemeka kwa sababu ya baridi

  • Maumivu ya kichwa

  • Maumivu ya mishipa

  • Kuchoka

  • Kichefuchefu (nausée)

  • Kutapika

  • Kuhara

Ikiwa malaria haitunzwe, inaweza kupunguza sana damu katika mwili, na bila kukawia inaweza kuhatarisha maisha. Utafute matunzo mara moja, mbele alama hizo zikuwe hatari sana, zaidi sana kwa watoto na wanawake wenye mimba.a

a Ili kupata habari zingine, soma Amuka! ya Mwezi wa 11, 2011, ukurasa wa 24 mupaka 25, na ya Mwezi wa 11, 2009, ukurasa wa 26 mupaka 29.

ULIJUA?

Saa yenye kuhesabu dakika imewekwa kwenye karte ya Afrika

Katika Afrika tu, mutoto mumoja anakufa kila dakika moja kwa sababu ya malaria

  • Watoto na wanawake wenye mimba wako katika hatari kubwa zaidi ya kugonjwa sana ikiwa wanapata malaria.

  • Katika Afrika tu, mutoto mumoja anakufa kila dakika moja kwa sababu ya malaria.

  • Watu fulani wamepata malaria kwa kutiwa damu katika mishipa, lakini hilo halitokee mara nyingi.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine