Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g 11/15 uku. 3-6
  • Dini Zimeanza Kukosa Watu?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Dini Zimeanza Kukosa Watu?
  • Amuka!—2015
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Sababu Gani Watu Wanaachana na Dini?
  • Kuachana na Dini Kulitabiriwa Zamani!
  • ‘Mutoke Kwake’!
  • Mwisho wa Dini ya Uwongo Unakaribia!
    Misho wa Dini ya Uwongo Unakaribia!
Amuka!—2015
g 11/15 uku. 3-6

HABARI KUBWA

Dini Zimeanza Kukosa Watu?

Watu wa familia wanasimama inje ya kanisa lenye kufungwa

Gaffar, mwenye alizaliwa katika inchi ya Uturuki, alihangaishwa na wazo la kwamba Mungu analipiza kisasi, lenye alifundishwa katika dini yake. Hediye, bibi yake, alianza kuwa na mashaka juu ya dini yake wakati alikuwa tu na miaka 9. Alisema hivi: “Nilifundishwa kuamini kama kila kitu chenye kutufikia katika maisha kimepangwa mbele ya wakati. Kwa sababu nilikuwa yatima, nilijiuliza, ‘Nilifanya nini ili jambo hili linifikie?’ Mara nyingi, nililia usiku muzima. Kufikia miaka 15, nilikuwa nimeachana na dini yangu katika moyo wangu.”

UMEACHANA na dini fulani? Kama jibu lako ni ndiyo, hauko wewe mwenyewe. Katika inchi nyingi, hesabu ya watu wenye kusema kama ‘hawana dini’ inaendelea kuongezeka, jambo hilo linaonyesha kama haijulikane ikiwa dini itakuwa namna gani wakati unaokuja. Inchi fulani kati ya hizo zinaonyeshwa hapa chini.

AUSTRALIA

Uchunguzi mbalimbali unaonyesha kama karibu wakaaji 50 juu ya 100 wa inchi hiyo wanasema kama hawana dini. Wakaaji wengine 10 juu ya 100 wanasema kama “hawaamini kabisa kama kuko Mungu.” Katika mwaka wa 2010, kiongozi mumoja wa dini alilalamika kuwa katika “miaka 40 hivi iliyopita, watu wengi sana wameacha kuwa Wakristo.”

UFARANSA

Kati ya watu wenye waliulizwa, ni watu 37 tu juu ya 100 ndio walisema kama wako na dini. Wengine walikuwa watu wenye hawaamini kama kuko Mungu na wengine hawakukuwa na dini. Kulingana na gazeti moja (The Economist), katika sehemu fulani za inchi hiyo ambamo dini ya Katoliki ilitia mizizi, dini hiyo iko ­“karibu kuanguka.”

IRELANDI

Wairelandi wengi wanaonekana kuwa wameanza kupoteza imani yao. Kati ya watu wenye waliulizwa, karibu watu 45 juu ya 100 walisema hawana dini, na wengine 10 juu ya 100 walisema hawaamini kama kuko Mungu. Kulingana na hesabu, inchi ya Irelandi ilikuwa kati ya inchi kumi zenye kuwa na wakaaji wengi wenye hawaamini kama kuko Mungu. Ripoti za vyombo vya habari ziko zinasema juu ya “mwisho wa Katoliki ya Irelandi.”

JAPANI

Kati ya Wajapani wenye waliulizwa, Wajapani 16 tu juu ya 100 ndio walisema kama wako na dini; 62 juu ya 100 walisema hawana dini ao hawaamini kama kuko Mungu.

AFRIKA KUSINI

Kati ya mwaka wa 2005 na 2012, watu 19 juu ya 100 walipunguka kwenye hesabu ya Wakaaji wa Afrika Kusini wenye walisema kama walikuwa na dini.

TUNISIA

Katika mwaka wa 2013, kati ya wakaaji wa Tunisia wenye waliulizwa, karibu wakaaji 60 juu ya 100 walisema kama hawaende tena kwenye misikiti (mosquées) yao lakini wanasali nyumbani. Walisema kama ni kwa sababu ya mawazo ya jeuri yenye kufundishwa humo.

INCHI YA AMERIKA

Tangu mwaka wa 2005, watu 13 juu ya 100 walipunguka kwenye hesabu ya watu wenye kusema kama wako na dini. Kati ya watu 5 wenye waliulizwa, karibu mutu 1 hakukuwa na dini yoyote. Kwa watu wazima wenye kuwa na miaka chini ya 30, ni mutu 1 juu ya 3 ndiye hakukuwa na dini. Makanisa mengi yanafunga milango kila mwaka.

VIETNAMU

Kati ya mwaka wa 2005 na 2012, hesabu ya watu wenye kusema kama wako na dini ilipunguka kutoka watu 53 juu ya 100 mupaka kufikia watu 30 tu juu ya 100.

Hesabu za inchi zote isipokuwa tu Tunisia zinatoka katika kitabu kimoja (2012 Global Index of Religion and Atheism) chenye kilichapishwa na shirika la Gallup International. Uchunguzi huo mbalimbali ulifanywa juu ya inchi 57, hilo linamaanisha wakaaji wa dunia zaidi ya 73 juu ya 100.

Karte yenye kuonyesha Australia, Ufaransa, Irelandi, Japani, Afrika Kusini, Tunisia, Inchi ya Amerika, na Vietnamu

Sababu Gani Watu Wanaachana na Dini?

Kuko sababu nyingi zenye kufanya watu wavunjike moyo kwa sababu ya dini. Kati ya sababu hizo kuko jeuri ao matendo ya kuogopesha yenye dini inachochea ao kuitika, matendo machafu ya uasherati yenye kufanywa na viongozi wa dini, na mambo mengine ambayo hayaonekane waziwazi yenye kufanya watu wengi zaidi waachane na dini. Mambo hayo ni kama vile:

  • Utajiri: Kichapo kimoja kinasema hivi: “Kama mutu anakuwa tajiri sana, hatahangaikia pia dini sana.” (Global Index of Religion and Atheism) Jambo lenye kichapo hicho kilisema ni la maana kwa sababu katika inchi nyingi, utajiri umeongezeka sana. Kulingana na John Nye, profesa wa mambo ya feza, katika maeneo fulani watu wanaishi “maisha yenye ingefanya mufalme mukubwa mwenye aliishi miaka mia mbili iliyopita atamani sana utajiri wao.”

    MAMBO BIBLIA INASEMA: Biblia ilitabiri kama katika “siku za mwisho,” watu watapenda feza kuliko kupenda Mungu na jirani. (2 Timotheo 3:1-5) Muandikaji mumoja wa Biblia alijua hatari yenye kuletwa na utajiri, kwa hiyo, alimuambia Yehova Mungu hivi: ‘Usinipe umasikini wala utajiri.’ Sababu gani aliomba hivyo? Aliongeza hivi: “Nisije nikashiba nikakukana.”—Methali 30:8, 9.

  • Desturi za dini na mwenendo: Watu wengi, zaidi sana vijana, wanaona kuwa dini haina faida leo.Wengine hawatumainie tena dini. Tim Maguire, musimamizi wa vyombo vya habari wa shirika moja katika inchi ya Écosse (Humanist Society Scotland), alisema hivi: “Kama unaangalia namna dini zimejiendesha kwa mamia ya miaka, watu wameachana nazo kwa sababu hawaamini tena kuwa ziko na mamlaka ya kutoa mashauri juu ya mwenendo.”

    MAMBO BIBLIA INASEMA: Juu ya walimu wa uongo, Yesu Kristo alitoa angalisho hili: ‘Kwa matunda yao mutawatambua. . . . Kila muti muzuri unazaa matunda mazuri, lakini kila muti uliooza unazaa matunda yasiyofaa.’ (Mathayo 7:15-18) Kati ya “matunda [hayo] yasiyofaa,” tunaweza kutaja kujiingiza katika siasa na kuitika matendo yenye kumuchukiza Mungu, kama vile mwanaume kulala na mwanaume ao mwanamuke kulala na mwanamuke. (Yohana 15:19; Waroma 1:25-27) Tena, kufundisha watu mafundisho na desturi zenye hazina maana kuliko kuwafundisha mafundisho ya muzuri yenye kuwa katika Maandiko ni kati ya matunda hayo yasiyofaa. (Mathayo 15:3, 9) Yesu alisema hivi: “Lisha kondoo wangu wadogo.” (Yohana 21:17) Lakini, leo watu wengi wako na njaa sana ya kiroho.

  • Dini na feza: Kulingana na Kituo cha Utafiti cha Pew, watu wengi wanaona kuwa dini inakazia sana feza. Shida kubwa zaidi ni kwamba, tofauti na waamini wao, viongozi fulani wa dini wanaishi maisha ya hali ya juu sana. Kwa mufano, katika muji mumoja wa Ujerumani kwenye watu wengi wanaoenda kwenye kanisa wako na shida ya kupata mambo ya lazima katika maisha, askofu ameshitakiwa kuwa anaishi maisha ya hali ya juu sana. Maisha hayo yamekwaza Wakatoliki wengi katika muji huo. Pia, ripoti moja ya gazeti GEO inasema kama katika inchi ya Nigeria, “kwenye watu milioni 100 wanaishi na feza dola moja hivi kwa siku, maisha ya hali ya juu sana ya mapasta fulani yanaanza kukwaza watu.”

    MAMBO BIBLIA INASEMA: Paulo,muandikaji mumoja wa Biblia aliandika hivi: “Sisi si wachuuzi wa [hatuuzishe] neno la Mungu.” (2 Wakorintho 2:17) Hata kama Paulo alikuwa mutumishi mwenye alijulikana katika kutaniko la Kikristo la wakati wa mitume, mara nyingi alifanya kazi ya mikono ili asiwekee wengine muzigo. (Matendo 20:​34) Kufanya hivyo kulionyesha kama alitii amri hii ya Yesu: ‘Mulipokea bure, mutoe bure.’—Mathayo 10:7, 8.

Mashahidi wa Yehova wanafuata kanuni hizo, hawauzishe vichapo vyao ao kulipisha mafundisho ya Biblia. Tena hawaombe sehemu ya kumi, wala hawakusanye ­sadaka kwenye mikutano yao. Lakini, feza zenye wako nazo lazima ili kuendesha kazi yao zinapatikana kupitia michango yenye watu wanatoa kwa kupenda.—Mathayo 6:2, 3.

Kuachana na Dini Kulitabiriwa Zamani!

Miaka fulani iliyopita, ingekuwa vigumu kuwazia hali mbaya yenye kupata dini leo. Lakini, Mungu aliona jambo hilo mbele ya wakati na alilionyesha katika Biblia. Kwa kutumia maneno ya mufano, Mungu alifananisha dini zote zenye kukosa uaminifu kwake na kahaba mwenye kujipodoa sana mwenye kuitwa ‘Babiloni Mukubwa.’—Ufunuo 17:1, 5.

Ufananisho huo ni wenye kufaa kwa sababu hata kama dini za uongo zinasema kuwa zinamutumikia Mungu kwa uaminifu, zimejiunga na watawala wa ulimwengu ili zipate nguvu na utajiri. Andiko la Ufunuo 18:9 linasema hivi: ‘Wafalme wa dunia walifanya uasherati pamoja naye.’ Tena, neno “Babiloni” linafaa, kwa sababu mafundisho na desturi za uongo za dini, kama vile kutokufa kwa nafsi, fundisho la utatu, na uchawi, yalianzia katika Babiloni ya zamani, muji wenye ulikuwa unajaa dini ya uongo na kuamini mambo ya uchawi.a—Isaya 47:1, 8-11.

Muji wenye nguvu wa Babiloni ulianguka wakati maji yake ya ulinzi ‘yalikaushwa.’ Maji hayo ni mufereji wenye ulikuwa unapata maji kutoka kwenye Muto Efrati, na kukaushwa kwa maji hayo kulisaidia majeshi ya Wamedi na Waajemi kupata ushindi juu ya muji huo. (Yeremia 50:1, 2, 38) Kwa kweli, muji wa Babiloni ulikamatwa katika usiku mumoja!—Danieli 5:7, 28, 30.

Babiloni Mukubwa naye ‘anakaa juu ya maji mengi.’ Biblia inatuambia kama maji hayo yanamaanisha “vikundi vya watu na umati,” ni kusema, mamilioni ya watu ­wenye kuunga mukono dini za uongo. (Ufunuo 17:1, 15) Biblia ilitabiri kama maji hayo ya mufano yatakauka, jambo hilo linaonyesha uharibifu wa haraka na wenye kuwa karibu wa Babiloni wa leo. (Ufunuo 16:12; 18:8) Lakini ni nani atamuharibisha? Viongozi wa kisiasa wenye anajiunga nao, ambao upendo wao kwake utageuka kuwa chuki. Pia, watakamata mali yake yote, ao kula nyama yake ya mufano.—Ufunuo 17:16, 17.b

Mwanaume anasoma Biblia na anaona akilini maji yenye kupunguka yaliyozunguka muji wa Babiloni na watu wenye kutoka katika Babiloni Mukubwa

Maji yenye kupunguka yaliyozunguka Babiloni yanafananisha kutoka kwa watu katika Babiloni Mukubwa

‘Mutoke Kwake’!

Kwa sababu ya mambo yenye yatapata Babiloni Mukubwa, kwa upendo, Mungu anatoa angalisho hili: ‘Mutoke kwake, watu wangu, ikiwa hamutaki kushiriki pamoja naye zambi zake, na ikiwa hamutaki kupokea sehemu ya mapigo yake.’ (Ufunuo 18:4) Ona neno “ikiwa,” lenye kutajwa mara mbili katika andiko hilo. Kwa kweli, Mungu anatoa angalisho hilo kwa watu wenye wanahangaishwa na mafundisho yenye kutenganisha watu na Mungu na wenye wanataka kukubaliwa na yeye, watu kama vile Gaffar na Hediye, wenye tumekwisha kutaja.

Mbele Gaffar ajifunze Biblia, alimuona Mungu kuwa mutu mwenye tunapaswa kutii kwa sababu tu ya woga. Alisema hivi: “Nilitulizwa sana kujua kama Yehova ni Mungu wa upendo, na kama anataka tumutii kwanza kwa sababu ya upendo.” (1 Yohana 4:8; 5:3) Hediye alipata amani ya moyoni wakati alijua kama haiko Mungu ndiye alimufanya yatima, na kama hali yake haikupangwa mbele ya wakati. Alitiwa moyo na maandiko ya Biblia kama vile andiko la Yakobo 1:13, lenye kusema kama Mungu hajaribu watu kupitia mambo mabaya. Yeye na Gaffar waliitika mafundisho ya Biblia na wakatoka katika “Babiloni.”—Yohana 17:17.

Wakati Babiloni Mukubwa ataharibiwa, watu wenye wameonyesha utii kwa kutoka kwake ili ‘kuabudu Baba kwa roho na kweli’ hawatapatwa na jambo lolote mbaya. (Yohana 4:23) Watu hao wako na tumaini la kuona dunia ‘inajaa na kumujua Yehova kama vile maji yanavyoifunika bahari.’—Isaya 11:9.

Ndiyo, dini ya uongo na matunda yake mabaya vitaisha, kwa sababu Mungu ‘hawezi kusema uongo.’ (Tito 1:2) Lakini ibada ya kweli itaendelea milele!

a Ili kupata habari zingine juu ya Babiloni Mukubwa, mambo Biblia inasema juu ya hali ya wafu, namna Mungu iko, na uchawi, soma kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? Unaweza kupata kitabu hicho kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org/swc.

b Soma habari “Mawazo ya Biblia—Mwisho wa Dunia,” katika gazeti hili la Amuka!

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine