Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g16 na. 2 uku. 8-9
  • Kumusaidia Mutoto Wako Katika Kipindi cha Mwili Kuanza Kukomaa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kumusaidia Mutoto Wako Katika Kipindi cha Mwili Kuanza Kukomaa
  • Amuka!—2016
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MAGUMU
  • MAMBO UNAPASWA KUJUA
  • MAMBO UNAWEZA KUFANYA
  • Habari Zenye Kuwa Ndani
    Amuka!—2016
  • Utafanya Nini Kijana Wako Akitilia Shaka Imani Yako?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Amuka!—2016
g16 na. 2 uku. 8-9
A father talks to his son

MUSAADA KWA FAMILIA| KULEA WATOTO

Kumusaidia Mutoto Wako Katika Kipindi cha Mwili Kuanza Kukomaa

Baba na mutoto wake mwanaume wanaangalia alama yenye kuonyesha kipindi cha mwili kuanza kukomaa kuanzia utoto mupaka kuwa mutu muzima

MAGUMU

Inaonekana kama vile ni jana tu ulikuwa unakamata mutoto wako katika mikono yako. Sasa uko na kijana mbele yako, ni kweli angali mutoto. Lakini anaingia katika kipindi chenye mwili wake unaanza kukomaa. Miaka hiyo ni kipindi cha wakati chenye kitamuongoza kuwa mutu muzima.

Namna gani unaweza kumusaidia mutoto wako mwanaume ao mwanamuke apiganishe mabadiliko hayo ya kuvuruga akili na wakati fulani ya kuogopesha, yenye yatamufanya akuwe na uwezo wa kuzaa?

MAMBO UNAPASWA KUJUA

Kipindi cha mwili kuanza kukomaa kinaanza na miaka mbalimbali. Kipindi hicho kinaweza kuanza na miaka 8 ao 15 hivi. Kitabu kimoja kinasema hivi: “Kipindi cha kawaida cha mwili kukomaa kinaanza na miaka mbalimbali.” (Letting Go With Love and Confidence)

Kipindi cha mwili kuanza kukomaa kinaweza kuhangaisha akili. Vijana wanaweza kuhangaikia sana namna wengine wanawaona. Kijana mumoja mwanaume mwenye kuitwa Jareda anakumbuka hivi: “Nilianza kuhangaikia namna watu wengine walikuwa wananiona na namna yangu ya kutenda. Wakati nilikuwa pamoja na watu wengine nilikuwa ninajiuliza ikiwa walikuwa wananiona kuwa mutu wa kawaida.” Kijana anaweza kuacha kujitumainia wakati chunusi (boutons) zinaanza kumutoka. Kellie, kijana mwanamuke wa miaka 17, anakumbuka hivi: “Nilisikia sawa vile sura yangu ilishambuliwa! Ninakumbuka namna nilikuwa ninalia na kujiona kuwa na sura ya mubaya.”

Kijana wenye kuanza kukomaa mbele ya wakati kuliko wengine wako na matatizo ya pekee. Jambo hilo ni kweli zaidi kwa vijana wanawake, wenye wanaweza kuchekwa na wengine kwa sababu wanaanza kuwa na maziwa ao umbo la mwili wao linaanza kubadilika. Kitabu kimoja kinasema hivi: “Wako pia katika hatari ya kuvutia wanaume wakubwa wenye kujua zaidi mambo ya ngono.” (A Parent’s Guide to the Teen Years)

Kuanza kukomaa kwa mwili haiko kuwa mutu muzima. Andiko la Methali 22:15 linasema hivi: ‘Ujinga umefungwa pamoja na moyo wa muvulana.’ Kuanza kukomaa kwa mwili hakubadilishe jambo hilo. Kijana anaweza kuonekana kuwa amekomaa, lakini kulingana na kitabu kimoja, hilo “halimaanishe kama amekuwa na uwezo wa kukamata maamuzi ya muzuri, kutenda kama mutu muzima, kujizuia, na kufanya mambo mengine yenye kuonyesha kama amekuwa mutu muzima.” (You and Your Adolescent)

MAMBO UNAWEZA KUFANYA

Zungumuza na mutoto wako juu ya kipindi cha mwili kukomaa mbele kianze. Umuelezee mutoto wako mambo yenye yatamufikia, zaidi sana juu ya kipindi cha mwezi (kwa vijana wanawake) na kutokwa na shahawa ao maji ya wanaume (kwa vijana wanaume). Tofauti na mabadiliko ya pole kwa pole ya kipindi cha mwili kuanza kukomaa, mambo hayo yanaanza kwa kushitukia na yanaweza kuvuruga akili ao hata kuogopesha. Wakati unazungumuzia mambo kama hayo, ukuwe na mawazo ya muzuri, uonyeshe kama kipindi cha mwili kuanza kukomaa kinaleta mabadiliko yenye kufanya kijana akuwe mutu muzima.—Kanuni ya Biblia: Zaburi 139:14.

Ueleze mambo waziwazi. Kijana mwanaume mwenye kuitwa John anakumbuka hivi: “Wakati wazazi wangu walizungumuza na mimi juu ya kipindi cha kuanza kukomaa kwa mwili, walieleza mambo kijuu-juu tu. Ningependa wanifasirie mambo waziwazi.” Alana, kijana wa miaka 17 anajisikia vile pia. Anasema hivi: “Mama yangu alinisaidia kuelewa mabadiliko yenye nilikuwa ninaona katika mwili wangu, lakini ningependa ikiwa angenisaidia kupambana muzuri na mambo yenye yalikuwa katika moyo wangu.” Wazazi wanaweza kujifunza nini? Hata kama inaonekana kuwa mambo ya haya, zungumuza na mutoto wako juu ya mambo yote yenye kuhusu kipindi cha mwili kuanza kukomaa.—Kanuni ya Biblia: Matendo 20:20.

Uliza maulizo yenye kuchochea mazungumuzo. Ili kusaidia watoto wajisikie huru, zungumuzia namna watu wengine walipambana na kipindi cha mwili kuanza kukomaa. Kwa mufano, unaweza kuuliza kijana wako mwanamuke, “Kuko wanafunzi fulani kwenye masomo wenye wameanza kuzungumuza juu ya kipindi cha mwezi?” “Watoto wanacheka vijana wanawake wenye kukomaa haraka?” Unaweza kuuliza kijana wako mwanaume, “Watoto wanachokoza vijana wenye kipindi chao cha mwili kuanza kukomaa kinachelewa?” Wakati vijana wanaanza kuzungumuza juu ya namna vijana wengine wanapitisha kipindi chao cha mwili kuanza kukomaa, inaweza kuwa rahisi kwao kuzungumuza waziwazi juu ya namna wanajisikia na mambo yenye wamejionea. Wakati wanafanya hivyo, fuata shauri hili la Biblia lenye kusema: ‘Ukuwe mwepesi kuhusu kusikia, si mwepesi wa kusema.’—Yakobo 1:19.

Umusaidie kijana wako akomalishe “hekima inayotumika na uwezo wa kufikiri.” (Methali 3:21) Kipindi cha mwili kuanza kukomaa haiko tu mabadiliko ya mwili na namna ya kujisikia katika moyo. Lakini, katika kipindi hicho, kijana wako anakomalisha pia uwezo mbalimbali wa kufikiri wenye utamusaidia kukamata maamuzi ya muzuri wakati atakuwa mutu muzima. Tumia nafasi hiyo ili kufundisha kijana wako kanuni za muzuri.—Kanuni ya Biblia: Waebrania 5:14.

Usichoke. Inaonekana kama vijana wengi hawapendi kuzungumuza na wazazi wao juu ya kipindi cha mwili kuanza kukomaa, lakini hilo lisikuzuie. Kitabu kimoja kinasema hivi: “Kijana mwenye kujifanya kama hapendi, hana hamu, hafurahie kuzungumuza ao mwenye kujifanya kuwa hasikilize, anaweza kuwa anachunga katika akili mambo yote yenye unamuambia.” (You and Your Adolescent)

a Majina fulani yamebadilishwa katika habari hii.

MAANDIKO YA MAANA

  • “Nimeumbwa kwa njia ya ajabu yenye kuogopesha.”—Zaburi 139:14.

  • “Sikuepuka kuwaambia ninyi lolote kati ya mambo yenye faida.”—Matendo 20:20.

  • “Watu wakomavu [wenye kukomaa] . . . nguvu zao za ufahamu zimezoezwa kutofautisha yaliyo sawa na yaliyo makosa pia.”—Waebrania 5:14.

“Wazazi wangu walinisaidia sana wakati nilikuwa katika kipindi cha mwili wangu kuanza kukomaa, zaidi sana mama yangu. Mama alichukua wakati wa kunifasiria kila kitu. Nilijua kabisa mambo yenye yangenifikia, kwa hiyo wakati mambo hayo yalifika, sikushangaa. Zaidi ya hiyo, mama yangu alinisaidia nijisikie huru kuzungumuza naye wakati wowote. Wazazi wangu walifanya ikuwe rahisi kwangu kupambana na mambo yenye kuonekana kuwa ya haya.”—Marie, mwenye miaka 16.

“Wazazi wangu walinisaidia. Kwa mufano, hawakuelezea mutu mwengine mambo yenye yalikuwa yananifikia, kwa sababu walijua kama yalikuwa mambo ya haya kwangu. Hilo lilinisaidia sana. Na walinifasiria mambo yenye ningepatwa nayo mbele yanifikie.”—Joan, mwenye miaka 18.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine