Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g16 na. 3 uku. 4-7
  • Kazi Yenye Wanafanya ili Luga Isikuwe Tena Kizuizi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kazi Yenye Wanafanya ili Luga Isikuwe Tena Kizuizi
  • Amuka!—2016
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Faida Zenye Kudumu
  • Vyombo kwa Ajili ya Kazi ya Kuhubiri—Vichapo kwa Ajili ya Kazi ya Kuhubiri Duniani Pote
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • A1 Kanuni za Kutafsiri Biblia
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • Kutolewa kwa Kitabu cha Maana Sana Kuliko Vitabu Vyote
    Namna Michango Yako Inatumiwa
  • Yehova Mungu, Anazungumuza na Watu Wake
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2016
g16 na. 3 uku. 4-7

HABARI KUBWA

Kazi Yenye Wanafanya ili Luga Isikuwe Tena Kizuizi

“Wakati fulani, watu wanasema kwamba kazi ya kutafsiri ni ngumu kuliko kazi zingine.”—“The Cambridge Encyclopedia of Language.”

MBELE ya kuanza kutafsiri, kuko kazi yenye inafanywa kwa uangalifu sana juu ya vichapo vya Mashahidi wa Yehova: kutayarisha habari, kutafuta maelezo zaidi juu ya habari hiyo, na kuiandika. Wakati huo, Biro ya Uandikaji yenye kuwa kwenye makao yao makubwa katika muji wa New York inachunguza habari zote ili kuhakikisha kwamba ni za kweli na kwamba zimeandikwa kulingana na kanuni zenye kutumiwa sasa za luga.a

Kisha, Biro ya Uandikaji inatumia vikundi vingi vya watafsiri habari hizo. Wengi kati yao wanaishi na kutumikia mahali kwenye watu wanasema luga yenye wanatafsiri, na wanatafsiri katika luga yao ya kizalikio. Wanapaswa kuelewa muzuri habari yenye watatafsiri na pia luga yao.

Kikundi cha watafsiri kinafanya kazi

NAMNA KAZI YA KUTAFSIRI INAFANYWA

Kwenye ukurasa huu, tunaona namna kazi ya kutafsiri Amuka! katika luga ya Kihispania inafanywa

  • Kikundi cha watafsiri kinapokea habari za Kiingereza zenye zitatafsiriwa katika luga ya Kihispania kutoka kwenye makao makubwa ya Mashahidi wa Yehova katika inchi ya États-Unis

  • Kila mutu anachunguza kwa uangalifu habari za kutafsiri

  • Mbele ya kuanza kutafsiri, kikundi cha watafsiri kinakutana ili kuzungumuzia habari ya kutafsiri

  • Watafsiri wanahakikisha kwamba habari yenye wametafsiri inatumia maneno yenye watu wanatumia, iko wazi, inapatana na Kiingereza, na kama imeandikwa kulingana na kanuni za luga

  • Kisha kupata mabadiliko ya mwisho, habari zenye zimetafsiriwa zinatumwa kwenye zitachapishwa na kugawanywa

  • Wasomaji katika dunia yote wanapata faida kupitia mashauri yenye hekima ya Biblia katika luga yao

Namna gani watafsiri wanafanya kazi yao?

Geraint, mutafsiri mwenye kuwa katika inchi ya Grande-Bretagne, anasema hivi: “Ninatumika pamoja na kikundi cha watafsiri. Kwa hiyo, siri ni kutumika kwa umoja. Sisi wote tunajikaza kutafuta namna ya kumaliza magumu yenye tunakutana nayo wakati tunatafsiri. Wakati huo, hatuchunguze tu maneno, lakini pia mafungu ya maneno. Tunawaza sana ili kujua maneno hayo yanamaanisha nini kabisa, na kila mara tunakumbuka habari hiyo iliandikwa kwa ajili ya nani.”

Ni jambo gani munatafuta wakati munatafsiri?

“Wakati tunatafsiri tunatafuta musomaji ajisikie kama habari yenye anasoma ilitayarishwa katika luga yake ya kizalikio. Habari hiyo haipaswe kuonekana kama ilitafsiriwa kutoka katika luga ingine. Ili kutimiza jambo hilo, tunajikaza kuandika namna watu wanatumia luga yao wakati wanazungumuza. Katika njia hiyo, tunafanya musomaji akuwe na hamu ya kusoma, na aendelee kusoma kama vile anakula chakula kitamu.”

Kuko faida gani ya kuishi mahali kwenye luga inazungumuziwa?

“Kuishi pamoja na watu wenye tunatafsiria kunatusaidia sana. Tunasikia namna wanaongea katika luga yao kila siku. Pia, tunaweza kuuliza wasomaji ili kujua kama maneno fulani ni yenye kueleweka, ni ya kawaida, na yenye kuvutia. Hilo linatusaidia kutafsiri maana ya kweli ya habari yenye ilitayarishwa katika luga ya Kiingereza.”

Namna gani munafanya kazi yenu?

“Kila kazi inapewa kikundi cha watafsiri. Kwanza, kila mumoja anasoma habari yenye tutatafsiri ili kuielewa na kujua imeandikwa kwa ajili ya nani, na ili kujua namna imeandikwa. Tunajiuliza hivi: ‘Habari hii iliandikwa kwa ajili ya nani? Inazungumuzia nini na iko na kusudi gani? Nitajifunza nini katika habari hii?’ Tunaendelea kufikiria maulizo hayo wakati tunatafsiri.

“Kisha, wote wanakutana pamoja ili kusikiliza mawazo ya kila mumoja. Tunajiuliza hivi: ‘Tuko hakika kwamba tumeelewa habari yenye tutatafsiri? Namna gani tunaweza kuitafsiri ili ikuwe kama habari yenye ilitayarishwa katika Kiingereza?’ Kusudi letu ni kusaidia musomaji ajisikie namna ule mwenye alitayarisha habari alipenda musomaji ajisikie.”

Namna gani kikundi cha watafsiri kinafanya kazi?

“Kusudi letu ni kusaidia wasomaji waelewe habari hiyo wakati tu wanaisoma. Ili kufikia kusudi hilo, tunasoma mara mingi kwa sauti kila fungu lenye tunatafsiri.

“Mutafsiri anaandika fungu katika luga yetu, na tunaweza kuona fungu hilo kwenye ordinatere zetu. Tunalinganisha maneno ya Kiingereza na ya luga yetu ili kuona kama hakuna wazo lenye tulisahau ao kuongeza. Tena tunaangalia kama fungu linaeleweka muzuri, limeandikwa bila makosa, na kama linaheshemia kanuni za luga yetu. Kisha, mumoja anasoma fungu hilo kwa sauti. Kama anakwama wakati anasoma, tunatafuta ili kujua sababu gani anakwama. Wakati tunamaliza kutafsiri habari yote, mumoja anaisoma kwa sauti na wengine wanaangalia na kuandika mambo ya kutengeneza.”

Hiyo ni kazi kubwa kabisa!

“Ndiyo kabisa! Na kila mangaribi tunachoka. Kwa hiyo, tunaangalia tena habari hiyo asubui wakati akili yetu inatulia. Kisha majuma fulani, Biro ya Uandikaji inatuma mabadiliko ya mwisho. Kisha tunasoma tena habari yenye tumetafsiri ili kuhakikisha kwamba inaeleweka kabisa na haina tena makosa.”

Munatumia programu gani za ordinatere?

“Kwa kweli, ordinatere haziwezi kukamata nafasi ya watafsiri. Lakini, Mashahidi wa Yehova wamefanya programu fulani za ordinatere ili kusaidia kazi ikuwe mwepesi. Kati ya programu hizo, kuna kamusi (dictionnaire) mwenye tunatia maneno yenye tunatumia kwa ukawaida. Programu ingine inatusaidia kutafuta maneno yote yenye tumekwisha kutafsiri katika luga yetu na kuona namna tuliamua juu ya magumu yenye tulikutana nayo zamani wakati tulitafsiri.”

Namna gani munaona kazi yenu?

“Tunaona kazi yetu kuwa zawadi kwa wasomaji. Na tunajikaza sana ili watu waifurahie. Tunapenda kabisa habari ya gazeti ao habari yenye kuwa kwenye Internete iguse moyo wa mutu mwenye ataisoma na kufanya maisha yake yakuwe muzuri zaidi.”

Faida Zenye Kudumu

Katika dunia yote, mamilioni ya watu wanapata faida kwa kusoma vichapo vya Mashahidi wa Yehova katika luga yao. Mashauri yenye hekima yenye kupatikana katika vichapo vyao na video, na habari zingine zenye kuwa kwenye adresi yao ya Internete ya jw.org vinategemea Biblia. Zaidi ya hilo, Mungu, mwenye jina lake ni Yehova, anatuambia kwamba anataka watu wa ‘kila taifa na kabila na luga’ wasikie ujumbe wenye kuwa katika kitabu hicho kitakatifu.—Ufunuo 14:6.b

a Habari zenye zitatafsiriwa zinatayarishwa katika luga ya Kiingereza.

b Fungua adresi yetu ya Internete www.jw.org ili kupata habari fulani za kusoma, za kusikiliza tu, na video katika luga yako na katika luga zingine nyingi.

JW.ORG

Adresi ya Internete ya Mashahidi wa Yehova

Luga zaidi ya 700

Umusikilize Mungu ili Uishi Milele

Broshua yenye kuchapishwa na Mashahidi wa Yehova

Luga zaidi ya 640

Munara wa Mulinzi

Gazeti lenye kuchapishwa na Mashahidi wa Yehova

Luga zaidi ya 250

Amuka!

Gazeti lenye kuchapishwa na Mashahidi wa Yehova

Luga zaidi ya 100

Gazeti Amuka! katika luga mbalimbali

“Niko na matatizo ya afya. Hata kama munganga wangu aliendelea kunitunza, habari fulani katika Amuka! yenye kupatikana katika luga yangu ya Kimalagasi (Malgache) ilinisaidia sana. Gazeti Amuka! lilinisaidia kujua namna ya kuzuia hasira yangu. Lilizungumuzia pia chakula chenye kufaa na mazoezi ya mwili yenye kufaa.c Nilitumikisha mambo yenye nilisoma, na afya yangu inaendelea kuwa muzuri zaidi.”—Ranaivoarisoa, inchi ya Madagaska.

“Munganga wangu ni mutaalamu wa kuchunguza namna homoni (hormones) zinafanya kazi. Anatumia Amuka! katika luga ya Gujarati ili kufundisha watu juu ya mambo ya afya. Kwenye masomo munganga huyo alizungumuzia dawa za kulewesha na kunywa pombe kupita kipimo. Kisha majuma kidogo, wanafunzi walisema kwamba habari zenye kupatikana katika gazeti Amuka! zilichochea baba zao watumie feza kidogo kwa ajili ya pombe, na feza nyingi kwa ajili ya watoto wao.”—Janet, inchi ya India.

c Gazeti Amuka! halipendekeze chakula fulani ao jambo fulani la kufanya ili afya ikuwe muzuri. Kila mutu anapaswa kuchunguza hali yake mbele ya kuamua ni chakula gani atakula na mazoezi gani ya mwili atafanya.

Mutoto mwanaume anaangalia video Ni Vibaya Kuiba kwenye jw.org

Gazeti Amuka! lilipokea ripoti ya mama mumoja wa inchi ya Angola. Mama huyo anasema hivi: “Mutoto wangu wa miaka 8 alipoteza kalamu (crayons) zake; kwa hiyo, aliiba kalamu za wanafunzi wenzake. Kisha kuangalia video Ni Vibaya Kuiba katika luga ya Kireno (Portugais) kwenye jw.org, aliomba huruma bila kuogopa. Aliniomba tuende naye kwenye masomo ili kuomba wanafunzi wenzake huruma na kuwaambia sababu gani aliamua kurudisha kalamu zao zenye aliiba. Mwalimu wake aliruhusu tuonyeshe wanafunzi wote video hiyo. Kisha kuangalia video hiyo, wanafunzi wengi walisema kwamba hawatakuwa wanaiba tena.”

Mwanaume mwenye kutumia programu ya JW Lugha

Programu ya Kusaidia Watu Kujifunza Luga!

Alama ya JW Lugha

Katika mwaka wa 2014, Mashahidi wa Yehova walitangaza kutolewa kwa programu ya kielektroniki yenye kuitwa JW Language. Programu hiyo yenye unaweza kupata kwa bure inasaidia kufundisha Biblia katika luga ingine. Programu hiyo inapatikana katika luga ya Kibengali, Kichina, Kiingereza, Kifaransa, Kijerumani, Kihindi, Kiindonesia, Kiitaliano, Kijapani, Kikorea, Kimyanmar, Kireno (Portugais), Kirusi, Kihispania, Kiswahili, Kitagalogi, Kithai, na Kituruki. Ili kujua mengi zaidi, ufungue jw.org na utafute JW Language.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine