Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g16 na. 5 uku. 14-15
  • Aristote

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Aristote
  • Amuka!—2016
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Aliandika Juu ya Mambo Mengi
  • Wakatoliki Wanakubali Mafundisho ya Aristote
  • Ni Nani Aliyetunga Sheria Zinazoongoza Ulimwengu Wetu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Habari Zilizo Ndani
    Amuka!—2016
  • Wazo Hilo Laingia Dini ya Kiyahudi, Jumuiya ya Wakristo, na Uislamu
    Jambo Gani Hutufikia Tunapokufa?
  • Biblia Ni ya Zamani Sana ao Ilisema Mambo Mbele ya Wakati?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2018
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2016
g16 na. 5 uku. 14-15

MAMBO YENYE HISTORIA INATUFUNDISHA

Aristote

Aristote

ZAIDI ya miaka 2300 hivi yenye imepita, Aristote alileta muchango mukubwa sana katika sayansi na filozofia. Mambo yenye aliandika yamependeza watu wengi na yametafsiriwa sana, na watu wengi wamejifunza sana mambo hayo. James MacLachlan, Profesa wa Historia, aliandika kama, “mawazo ya Aristote juu ya ulimwengu, yalienea sana katika Ulaya kwa miaka karibu 2000 hivi.” Mawazo fulani ya Aristote yalichochea mafundisho ya Wakatoliki na Waprotestanti, na hata pia Waislamu.

Aliandika Juu ya Mambo Mengi

Aristote aliandika juu ya ufundi mbalimbali, nyota, biolojia, mwenendo, luga, sheria, mantiki (logique), nguvu za sumaku, metafizikia, mwendo (mouvement), raha, mashairi, siasa, saikolojia, ufundi wa kusema, na hata pia juu ya nafsi, yenye aliona kuwa inaweza kufa. Lakini, anajulikana sana kwa sababu ya mambo yenye aliandika juu ya biolojia na mantiki.

Wagiriki wa zamani wenye elimu walitemegea uwezo wao wa kuangalia, wa kukata kauli, na mantiki yao ili kufasiria ulimwengu wa asili. Kuanzia mambo yenye waliona kuwa hayawezi kupingwa, waliamini kwamba ikiwa wanayachunguza kwa uangalifu, wangefikia kupata ukweli.

Kupitia filozofia hiyo, walifikia kuelewa muzuri mambo fulani. Kwa mufano, walifikia kujua kwamba kuna utaratibu fulani katika ulimwengu. Lakini, tatizo kubwa ni kwamba, uwezo wao wa kuangalia ulikuwa na mipaka; hilo lilipotosha watu wengi wenye elimu, kutia ndani Aristote. Kwa mufano, waliamini kama sayari (planètes) na nyota zinazunguka dunia. Wakati huo, hilo lilionekana kuwa ukweli wenye kuwa wazi. Kitabu kimoja kinasema hivi: “Ujuzi na uelewaji mudogo wenye watu walikuwa nao ulionekana kama ulihakikisha mawazo ya Wagiriki juu ya dunia, ni kusema, dunia iko katikati ya ulimwengu.”—The Closing of the Western Mind.

Mawazo hayo yenye makosa yangekuwa na matokeo kidogo kama yangebakia tu katika sayansi. Lakini haikuwa hivyo.

Wakatoliki Wanakubali Mafundisho ya Aristote

Katika kipindi kati ya mwaka wa 500 hivi mupaka 1500, mafundisho fulani ya Aristote yalifikia kuonwa kuwa ya kweli na “Wakristo” wa Ulaya, ni kusema, wengi waliyakubali. Wanateolojia wa dini ya Katoliki ya Roma, zaidi sana Thomas d’Aquin (aliishi karibu na mwaka wa 1224 mupaka mwaka wa 1274), waliingiza katika teolojia yao maandishi ya Aristote. Kwa hiyo, mawazo ya Aristote yenye kuonyesha kwamba dunia iko katikati ya ulimwengu na kwamba haizunguke yalifikia kuwa fundisho la dini ya Katoliki. Fundisho hilo lilikubaliwa pia na viongozi wa dini ya Kiprotestanti, kama vile Calvin na Luther, wenye walisema kwamba hilo lilikuwa fundisho la Biblia.—Ona kisanduku “Walisoma Mambo Mengi Katika Biblia.”

Mafundisho fulani ya Aristote yalifikia kuonwa kuwa ya kweli

Muandikaji mwenye kuitwa Charles Freeman alisema hivi: “Hakukuwa tofauti hata kidogo kati ya njia fulani za kufikiri [mafundisho ya Aristote] na mafundisho ya dini ya Katoliki.” Kwa hiyo, watu wengi walisema kwamba Thomas d’Aquin “alibatiza” Aristote katika imani ya Kikatoliki. Lakini, kwa kweli, “Thomas d’Aquin ndiye alifikia kuamini mafundisho ya Aristote,” kama vile Freeman aliandika. Na kwa kadiri fulani, tunaweza kusema kwamba kanisa lilifikia pia kufanya hivyo. Matokeo ni kwamba, Galileo, Muitaliano mwenye elimu ya nyota na hesabu, mwenye alipima kutoa ushuhuda kulingana na mambo yenye aliona kwamba dunia inazunguka jua, aliombwa kufika kwenye Tribinali ya Kuhukumu Waasi wa Dini. Kwenye tribinali hiyo walimukaza akubali kwamba mambo yenye alisema yalikuwa ya uwongo.a Jambo la kushangaza ni hili: Aristote alitambua kwamba ujuzi wa mambo ya sayansi unaongezeka hatua kwa hatua, na kwamba unaombwa kurekebishwa. Ingekuwa muzuri kama kanisa zingekubali pia mawazo hayo!

a Ili kupata habari zaidi juu ya “Mgogoro Kati ya Galileo na Kanisa,” ona gazeti Amuka! la tarehe 22, Mwezi wa 4, 2003.

MAELEZO MAFUPI

  • Aristote alipenda sana kujua mambo na “alikuwa na heshima nyingi kwa ajili ya faida yenye ulimwengu ulikuwa nao juu yake.”—Aristotle—A Very Short Introduction.

  • Alifikiri kwamba ulimwengu uko na “Muanzishaji wa Mwendo,” mwenye kuishi milele, ambaye anatokeza mwendo wa milele, ambaye ni wa muzuri na anapatikana inje ya ulimwengu.

  • Aristote anajulikana kuwa yeye ndiye alianzisha sayansi mbili: biolojia na mantiki.

  • Aristote alifundisha kijana wa Makedonia mwenye alianzisha utawala mukubwa, ambaye alifikia kuitwa Alexandre Mukubwa.

A drawing of an earth-centered universe

Many ancients believed in an earth-centered universe

Walisoma Mambo Mengi Katika Biblia

Wanateolojia fulani wa zamani walishikamana kabisa na mawazo ya Aristote yenye kuonyesha kwamba dunia iko katikati ya ulimwengu kwa sababu walisoma maandiko mengi katika Biblia, kama vile Zaburi 104:5. Andiko hilo linasema hivi: ‘[Mungu] ameiwekea dunia musingi juu ya mahali pake palipofanywa imara; haitatikiswa mupaka wakati usio na kipimo, ao milele.’ Muandikaji huyo wa Biblia hakuwa anazungumuzia mahali penye kuwa dunia katika ulimwengu. Lakini, alikuwa anaonyesha kupitia maneno ya mufano kwamba dunia itadumu milele kulingana na kusudi la Mungu.—Mhubiri 1:4.

Hata hivyo, wakati Biblia inazungumuzia mambo ya sayansi, inasema kweli. Kwa mufano, andiko la Ayubu 26:7, lenye liliandikwa kumepita karibu miaka 3500, linasema kwamba Mungu “[alitundika] dunia pasipo na kitu.” Andiko la Ayubu 38:33 linaonyesha kwamba vitu vyenye kuwa katika anga vinaongozwa na sheria za asili.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine