Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g17 na. 4 uku. 10-11
  • Wakati Watoto Hawako Tena Nyumbani

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Wakati Watoto Hawako Tena Nyumbani
  • Amuka!—2017
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MAGUMU
  • SABABU GANI HALI HIYO INATOKEA
  • MAMBO UNAWEZA KUFANYA
  • Wazazi, Mufundishe Watoto Wenu Wamupende Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • Namna Mukristo Anaweza Kufanya Ndoa Yake Ikuwe ya Muzuri
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • “Ndoa na Iheshimiwe”
    Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
  • Wakati Mawazo Inapingana
    Musaada kwa Familia
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2017
g17 na. 4 uku. 10-11
Bwana mumoja anaangalia televizyo katika sehemu moja ya chumba wakati bibi yake anashona kwa shindano katika sehemu ingine

MUSAADA KWA FAMILIA | NDOA

Wakati Watoto Hawako Tena Nyumbani

MAGUMU

Mara nyingi, bibi na bwana wanapambana na magumu wakati watoto wao wanakomaa na kuondoka nyumbani. Kuishi katika nyumba yenye haina tena watoto kunaweza kuwafanya wajisikie kama watu wenye hawajuane kabisa. Gary Neuman, mushauri wa mambo ya familia, anasema hivi: “Nashauria watu wengi wenye hawajue namna ya kurudisha urafiki wao pamoja na bibi ao bwana zao. Sasa kwa sababu watoto hawako tena nyumbani, [wazazi] hawana tena mambo mengi ya kuzungumuzia ao ya kufanya pamoja.”a

Ndoa yenu iko kwa njia fulani katika hali kama hiyo? Kama ni hivyo, munaweza kufanya uhusiano wenu ukuwe muzuri. Kwanza, tufikirie mambo yenye yanaweza kufanya bibi na bwana wasikuwe na uhusiano muzuri.

SABABU GANI HALI HIYO INATOKEA

Kwa miaka mingi, mulitanguliza kwanza watoto. Wakiwa na nia nzuri, wazazi wengi wanatia mahitaji ya watoto wao mbele ya mahitaji ya ndoa yao. Matokeo ni kwamba wanafikia kuzoea kutimiza daraka la baba na mama hivi kwamba wanapoteza uhusiano wao wa bibi na bwana. Jambo hilo linaonekana haraka wakati watoto hawako tena nyumbani. Bibi mumoja wa miaka 59 anasema hivi: “Wakati watoto walikuwa nyumbani, tulifanya mambo mengi pamoja.” Lakini wakati watoto waliondoka nyumbani, anasema hivi: “Kila mutu alikuwa na mambo yake ya kutanguliza.” Wakati fulani aliambia bwana yake hivi: “Kila mutu iko katika njia yake.”

Bibi na bwana fulani hawajitayarishe ili kujipatanisha na hali hii ya sasa katika maisha. Kitabu Empty Nesting kinasema hivi: “Kwa bibi na bwana wengi, ni kama tu kuwa katika ndoa mupya.” Kwa sababu wanaona kwamba hawana mambo mengi ya kufanya pamoja, bibi na bwana wengi wanafuatilia kila mumoja mambo yake, na kufikia kuwa kama vile watu wenye kuishi katika chumba kimoja kuliko kuwa kama wenye kuoana.

Jambo la kufurahisha ni kwamba munaweza kuepuka mitego hiyo na hata kupata faida katika hali hii mupya yenye inatokea katika maisha. Biblia inaweza kuwasaidia kufanya hivyo. Tuone namna gani.

MAMBO UNAWEZA KUFANYA

Ujikaze kukubali mabadiliko. Kuhusu watoto wenye kukomaa, Biblia inasema hivi: ‘Mwanaume atamuacha baba yake na mama yake.’ (Mwanzo 2:24) Mukiwa wazazi, kusudi lenu ni kuzoeza watoto wenu kwa muda huo, kuwasaidia wakuwe na uwezo wenye wako nao lazima ili kuishi kama watu wazima. Mukifikiria mambo katika njia hiyo, mutaona kuondoka kwa watoto wenu nyumbani kuwa jambo la muzuri.​—Kanuni ya Biblia: Marko 10:7.

Ni kweli kwamba mutaendelea kuwa wazazi kwa watoto wenu. Lakini, sasa, munakuwa zaidi watu wa kutoa mashauri kuliko kuwa watu wa kuwaongoza. Hali hii mupya inakuwezesha kuendelea kuwa na uhusiano wa karibu pamoja na watoto wako wakati unahangaikia kwanza bibi ao bwana yako.b​—Kanuni ya Biblia: Mathayo 19:6.

Muzungumuzie pamoja mahangaiko yenu. Ambia bibi ao bwana yako namna unajisikia kuhusu mabadiliko hayo mapya katika maisha, na ukuwe tayari kusikia mahangaiko yake. Ukuwe muvumilivu na mwenye kuelewa mwenzako. Inaweza kuchukua wakati murefu ili kutia nguvu uhusiano wenu mukiwa bibi na bwana, lakini kujikaza kufanya hivyo kunaleta matokeo mazuri.​—Kanuni ya Biblia: 1 Wakorintho 13:4.

Mutafute mambo mapya ya kufanya pamoja. Muzungumuzie mambo yenye munapenda kutimiza pamoja. Kwa kuwa mumekomalisha watoto, mumepata hekima katika maisha. Sababu gani musitumie hekima hiyo ili kusaidia wengine?​—Kanuni ya Biblia: Ayubu 12:12.

Muonyeshe kwamba mungali munapendana. Mukumbuke sifa zenye zilifanya mupendane. Mukiwa bibi na bwana, mufikirie mambo mazuri yenye mulifanya pamoja na magumu yenye mulipambana nayo. Kwa kumalizia, mujue kwamba munaweza kufurahia hali hii mupya yenye inatokea katika maisha yenu. Kwa kweli, kama munaungana mukono, muko na nafasi ya kufanya ndoa yenu ikuwe muzuri zaidi na kurudisha tena pa nafasi ya kwanza upendo wenye uliwaunganisha.

a Habari hii inatoka katika kitabu Emotional Infidelity.

b Kama ungali unakomalisha watoto, ukumbuke kwamba uko ‘mwili mumoja’ pamoja na bibi ao bwana yako. (Marko 10:8) Watoto wanajisikia salama zaidi sana wakati wanaona kwamba wazazi wao wako na uhusiano muzuri.

MAANDIKO YA MAANA

  • ‘Mwanaume atamuacha baba yake na mama yake.’​—Marko 10:7.

  • ‘Kile ambacho Mungu ameunganisha mutu yeyote asikitenganishe.’​—Mathayo 19:6.

  • ‘Upendo ni wenye ustahimilivu na wenye fazili.’​—1 Wakorintho 13:4.

  • “Je, hekima haimo katikati ya wazee?”​—Ayubu 12:12.

Salvatore na Aurora

SALVATORE NA AURORA

“Tulifikia kutambua kwamba sasa tulikuwa na wakati mwingi na kwamba tulipaswa kufaidika na wakati huo. Kwa hiyo, tuliamua kusaidia watu wengi zaidi​—familia zenye kuwa na watoto na pia bibi na bwana wenye hawajakawia katika ndoa yao. Tunapenda kusaidia wengine na kuwaonyesha mambo yenye tulikutana nayo katika maisha.”

Carlo na Caterina

CARLO NA CATERINA

“Iliomba wakati murefu ili kukubali kwamba maisha yetu yalikuwa yamebadilika. Kwa miaka mingi tulizungumuzia zaidi sana watoto. Sasa, wakati tunafanya mambo pamoja, tumeanza polepole kuzoea kuzungumuza kuhusu sisi wenyewe na mapendezi yetu.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine