Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g18 na. 1 uku. 3
  • Namna ya Kupata Njia

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna ya Kupata Njia
  • Amuka!—2018
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Wenye Furaha Ni Wale Wenye Kumutumikia “Mungu Mwenye Furaha”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
  • Habari Zenye Kuwa Ndani
    Amuka!—2018
Amuka!—2018
g18 na. 1 uku. 3
Mwanaume mwenye kutembea katika njia

NJIA YA MAISHA YENYE FURAHA

Namna ya Kupata Njia

UNAJIONAKA KUWA MUTU MWENYE FURAHA? Ikiwa ni hivyo, ni nini inakufanyaka ukuwe mwenye furaha? Familia yako, kazi, ao dini yako? Pengine unatumainia jambo fulani likuletee furaha, kama vile kumaliza masomo, kupata kazi ya muzuri ao kuuza motokari ya mupya.

Watu wengi wanapata furaha kwa kiasi fulani wakati wanatimiza mupango fulani ao kupata kitu chenye walipenda sana. Lakini, furaha kama hiyo inakawia? Mara nyingi furaha hiyo haikawie, na hilo linaweza kuvunja moyo.

“Furaha” imefasiriwa kuwa “hali ya muzuri yenye kuendelea kwa kiasi fulani, yenye inaleta hisia kuanzia hali ya kutosheka mupaka shangwe nyingi katika maisha, pamoja na tamaa ya kupenda hali hiyo iendelee.”

Zaidi ya hilo, kama vile hali ya muzuri yenye kuendelea kwa kiasi fulani, furaha imefasiriwa kuwa kama vile safari, hapana kama vile muradi ao fasi kwenye mutu anaenda. Kusema kama, “Nitakuwa na furaha wakati tu . . .” kwa kweli, ni kuchelewesha furaha.

Kwa mufano, tunaweza kulinganisha furaha na kuwa na afya ya muzuri. Namna gani tunaweza kuwa na afya ya muzuri? Tunapaswa kuwa na tabia za muzuri kuhusu chakula, mazoezi na katika maisha yetu yote. Vilevile, furaha inatokea wakati tuko na tabia za muzuri katika maisha, kwa kuishi kulingana na kanuni za muzuri.

Ni kanuni ao sifa gani katika maisha zinasaidia mutu kupata njia ya maisha yenye furaha? Hata kama kanuni ao sifa fulani ni za maana kuliko zingine, kanuni ao sifa zenye kuonyeshwa hapa chini ni za maana zaidi:

  • KUTOSHEKA NA UKARIMU

  • AFYA YA KIMWILI NA UWEZO WA KUVUMILIA

  • UPENDO

  • KUSAMEHE

  • KUSUDI KATIKA MAISHA

  • TUMAINI

Kitabu kimoja chenye hekima na chenye kuhemishiwa sana kinasema hivi: “Wenye furaha ni wale wasio na kosa katika njia yao.” (Zaburi 119:1) Tuzungumuzie basi njia hiyo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine