Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g18 na. 2 uku. 6
  • 3 Kuheshimiana

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 3 Kuheshimiana
  • Amuka!—2018
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MAANA YAKE NINI?
  • SABABU GANI NI JAMBO LA MAANA
  • MAMBO YENYE UNAWEZA KUFANYA
  • Namna ya Kuonyesha Heshima
    Amuka!—2016
  • Namna ya Kuelewana
    Amuka!—2014
  • Wakati Urafiki Unakuwa wa Nguvu Sana
    Amuka!—2013
  • Namna ya Kuonyesha Shukrani
    Amuka!—2017
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2018
g18 na. 2 uku. 6
Bibi na bwana wanatumia ciment ili kujenga

Maneno yenye heshima yako kama ciment yenye inaweza kuunganisha ndoa yenu

KWA AJILI YA BIBI NA BWANA

3 Kuheshimiana

MAANA YAKE NINI?

Bibi na bwana wenye kuheshimiana wanahangaikiana hata wakati hawakubaliane juu ya jambo fulani. Kitabu Ten Lessons to Transform Your Marriage kinasema, “Bibi na bwana kama hao wanaepuka kujiingiza katika hali yenye itafanya wakatae kukubaliana. Lakini wanaendelea kuzungumuzia matatizo yoyote yenye kufanya wasielewane. Kila mumoja wao anasikiliza kwa heshima mawazo ya mwenzake na wanafikia makubaliano yenye yatawasaidia wote wawili.”

KANUNI YA BIBLIA: ‘Upendo . . . hautafute faida zake wenyewe.’​—1 Wakorintho 13:4, 5.

“Ninaonyesha kuwa ninaheshimia bibi yangu kwa kupendezwa na mambo yenye anaona kuwa ya maana na kwa kuepuka kufanya jambo lolote lenye litamuumiza ao kuharibu ndoa yetu.”​—Micah.

SABABU GANI NI JAMBO LA MAANA

Bila heshima, mazungumuzo kati ya bibi na bwana yanaweza kuwa yenye kuchambua, yenye mazarau, na hata yenye kukosa adabu​—wachunguzi wanasema kuwa mambo kama hayo ni alama yenye kuonyesha kuwa ndoa itafikiaka kuvunjika.

“Kutumia maneno yenye mazarau, ya kushushiana heshima, ao mizaha ya kuchekesha juu ya bibi yako kutamufanya tu ajione kuwa mutu mwenye hafae kitu, kutamufanya asikutumainie tena, na kutaharibu ndoa yenu.”​—Brian.

MAMBO YENYE UNAWEZA KUFANYA

UJICHUNGUZE

Ukazie uangalifu mazungumuzo na matendo yako kwa muda wa juma moja. Kisha ujiulize:

  • ‘Ni mara ngapi nilitumia maneno yenye kuchambua bibi ao bwana yangu, na ni mara ngapi nilimupongeza?’

  • ‘Ni katika njia gani zenye kuwa wazi nilionyesha kuwa ninamuheshimia bibi ao bwana yangu?’

ZUNGUMUZA NA BIBI AO BWANA YAKO

  • Ni matendo na maneno gani yatasaidia kila mumoja wenu ajisikie kuwa anaheshimiwa?

  • Ni matendo na maneno gani yenye yanafanyaka kila mumoja wenu ajisikie kuwa anakosewa heshima?

MASHAURI

  • Andika njia tatu ambamo ungependa kuonyeshwa heshima. Ambia bibi ao bwana yako afanye pia hivyo. Kila mumoja apatie mwenzake liste yenye alifanya, na mujikaze kuonyesha heshima katika mambo yenye muliandika.

  • Fanya liste ya sifa za bibi ao bwana yako zenye zinakupendeza. Kisha ambia bibi ao bwana yako kuwa unapendezwa sana na sifa hizo.

“Kuheshimia bwana yangu kunamaanisha: kuonyesha kupitia matendo yangu kama ninamuona kuwa mutu wa maana na kama ninapenda akuwe na furaha. Heshima haionekane tu kwa kufanya mambo makubwa; wakati fulani mambo madogo-madogo yenye mutu anafanya mara kwa mara yanaweza kuonyesha heshima ya kweli.”​—Megan.

Utafikia kujua kama, haitegemee kujiona wewe mwenyewe kuwa mutu mwenye kuonyesha heshima ao hapana; ni kujua ikiwa mwenzako anajisikia kuwa anaheshimiwa.

KANUNI YA BIBLIA: ‘Mujivike upendo mwororo wenye huruma, fazili, unyenyekevu wa akili, upole, na ustahimilivu [ao, uvumilivu].’​—Wakolosai 3:12.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine