Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g18 na. 2 uku. 11
  • 8 Onyesha Mufano

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 8 Onyesha Mufano
  • Amuka!—2018
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MAANA YAKE NINI?
  • SABABU GANI NI JAMBO LA MAANA
  • MAMBO YENYE UNAWEZA KUFANYA
  • Wazazi, Musaidie Watoto Wenu Wamupende Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Jinsi ya Kuwafundisha Watoto Kumhusu Mungu—Ni Njia Gani Zinazofaa Zaidi?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Wazazi, Mufundishe Watoto Wenu Wamupende Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • Wazazi, Musaidie Watoto Wenu Wakuwe na Imani Yenye Nguvu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2018
g18 na. 2 uku. 11
Mutoto mwanamuke anatembea akifuata hatua za baba yake katika teluji

Ni hatua za namna gani zenye unaachia watoto wako wafuate??

KWA AJILI YA WAZAZI

8 Onyesha Mufano

MAANA YAKE NINI?

Wazazi wenye kuonyesha mufano wanaishi kulingana na mambo yenye wanafundisha. Kwa mufano, hauwezi kutazamia mutoto wako akuwe anasema kweli ikiwa siku moja wakati haukupenda kuongea na mutu mwenye alikuja kukuona, mutoto alikusikia unasema, “Umuambie kama nimetoka.”

“Watu wengi wanasema ‘Ufanye kile ninasema, hapana kile ninafanya.’ Lakini hilo haliwezi kusaidia watoto. Watoto wako kama sifongo (chiffon) yenye kunyonya kila kitu chenye tunasema ao kufanya, na wanaweza kutuambia wakati mambo yenye tunafanya hayapatane na mambo yenye tunajaribu kuwafundisha.”​—David.

KANUNI YA BIBLIA: “Wewe, unayehubiri ‘Usiibe,’ je, wewe unaiba?”​—Waroma 2:21.

SABABU GANI NI JAMBO LA MAANA

Watoto na hata vijana wenye kuwa na miaka kati ya 13 na 19 wanachochewa zaidi sana na wazazi wao kuliko mutu mwingine yeyote​—kutia ndani watoto ao vijana wenzao. Hilo linamaanisha kuwa wewe ndiye uko na nafasi ya muzuri zaidi ya kuongoza watoto wako katika njia ya muzuri; ikiwa tu unatenda kulingana na mambo yenye unafundisha.

“Tunaweza kusema jambo fulani mara nyingi na kujiuliza ikiwa mutoto wetu iko anasikiliza, lakini wakati tu tunashindwa kufanya vile tulisema, mutoto atatukumbusha jambo hilo. Watoto wanaangalia kila kitu tunafanya, hata kama tunawaza kuwa hawaangalie.”​—Nicole.

KANUNI YA BIBLIA: “Hekima inayotoka juu . . . si ya kinafiki.”​—Yakobo 3:17.

MAMBO YENYE UNAWEZA KUFANYA

Chunguza kanuni zako mwenyewe. Ni mambo gani ya kujifurahisha yenye unaangaliaka? Unatendea namna gani bibi ao bwana yako na watoto wako? Marafiki wako ni watu wa namna gani? Unafikiriaka watu wengine? Kwa kifupi, uko na sifa zenye unapenda watoto wako wakuwe nazo?

“Mimi na bwana yangu hatuambie watoto wetu wafuate kanuni zenye sisi wenyewe hatufuate.”​—Christine.

Omba musamaha wakati unafanya makosa. Watoto wako wamekwisha kujua kama haukamilike. Kwa kusema “munisamahe” wakati unakosea ​—ikuwe bibi ao bwana yako ao watoto​—unawafundisha somo la maana la kusema kweli na kuwa munyenyekevu.

“Watoto wetu wanapaswa kusikia vile tunakubali makosa yetu na kuomba musamaha juu ya makosa yetu. Ikiwa hatufanye vile, hawatakuwa wanakubali wakati wanafanya makosa.”​—Robin.

“Tukiwa wazazi, mambo yenye tunafanya yako na matokeo makubwa zaidi juu ya watoto wetu, na mufano wetu ni njia ya muzuri zaidi yenye tunaweza kutumia kwa sababu kila wakati wanaona mufano wetu. Ni kama vile wanafundishwa kila wakati kupitia namna wazazi wao wanaishi.”​—Wendell.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine