Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g18 na. 2 uku. 14
  • 11 Kutumika kwa Bidii

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 11 Kutumika kwa Bidii
  • Amuka!—2018
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MAANA YAKE NINI?
  • SABABU GANI NI JAMBO LA MAANA
  • MAMBO YENYE UNAWEZA KUFANYA
  • Namna ya Kufurahia Kazi Ngumu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Kazi
    Amuka!—2015
  • ‘Ona Mema kwa Ajili ya Kazi Yako Ngumu’
    Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
  • Ufurahie Kazi Yako
    Namna ya Kubakia Katika Upendo wa Mungu
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2018
g18 na. 2 uku. 14
Kijana mwanamuke iko anakimbia

Kujifunza kutumika kwa bidii ni kama vile kufanya mazoezi; kutakuletea faida hapa sasa na wakati wenye kuja

KWA AJILI YA VIJANA

11 Kutumika Kwa Bidii

MAANA YAKE NINI?

Watu wenye kutumika kwa bidii hawakimbiake kazi. Lakini wanafurahia kutumika kwa bidii ili kupata mambo yenye wako nayo lazima na kusaidia watu wengine​—wanafanya hivyo hata kama kazi yao ni ya hali ya chini.

SABABU GANI NI JAMBO LA MAANA

Tupende ao tusipende, maisha yanatuomba kutimiza madaraka mengi. Katika dunia ambamo watu wengi hawapendi kutumika sana, kufanya kazi kwa bidii kutakuletea faida.​—Mhubiri 3:13.

“Nimejifunza kwamba wakati unatumika kwa bidii, unajivunia kazi yako na unatosheka moyoni. Hali hiyo ya kujisikia mwenye kutosheka imefanya nijifunze kupenda kazi. Kukomalisha tabia za muzuri za kufanya kazi kutakusaidia pia ujulikane kuwa mufanyakazi muzuri.”​—Reyon.

KANUNI YA BIBLIA: ‘Kwa kila kazi ngumu kunatokea faida.’​—Methali 14:23.

MAMBO YENYE UNAWEZA KUFANYA

Ukuwe na maoni yenye kufaa juu ya kazi kwa kufuata hatua zenye kuonyeshwa hapa chini.

Ujifunze kufanya mambo muzuri. Ikuwe unafanya kazi za nyumbani, unamaliza kufanya kazi za masomo, ao kazi ya kimwili, ufanye kazi hizo kwa bidii. Kisha kufanya muzuri kazi fulani, tafuta njia za kuifanya haraka zaidi ao muzuri zaidi. Kadiri unaendelea kuwa na uzoefu, ni vile utafurahia zaidi kazi yako.

KANUNI YA BIBLIA: ‘Je, umemuona mutu stadi [ao, fundi] katika kazi yake? Yeye atasimama mbele ya wafalme; hatasimama mbele ya watu wa kawaida.’​—Methali 22:29.

Usijifikirie wewe mwenyewe tu. Karibu katika kila hali, wakati unatimiza madaraka yako muzuri, unaletea wengine faida. Kwa mufano, wakati unafanya kazi za nyumbani kwa bidii, unapunguzia wengine kazi katika familia.

KANUNI YA BIBLIA: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.”​—Matendo 20:35.

Ufanye mengi zaidi. Kuliko kufanya kidogo tu, jaribu kufanya mengi zaidi kuliko yale unaombwa kufanya. Kwa kufanya hivyo, unaongoza muzuri maisha yako​—utafanya mengi zaidi, haiko juu unalazimishwa, lakini kwa sababu unaamua kufanya hivyo.​—Mathayo 5:41.

KANUNI YA BIBLIA: ‘Tendo lako njema likuwe, si kwa kulazimishwa, bali kwa kupenda kwako mwenyewe.’​—Filemoni 14.

Ukuwe na usawaziko. Watu wenye kufanya kazi kwa bidii hawako wavivu, wala hawapendi kazi kupita kiasi. Wanajikaza kuwa na usawaziko, wanafurahia kutumika kwa bidii na pia vipindi vya mapumuziko.

KANUNI YA BIBLIA: ‘Konzi [ao, mukono] moja ya pumuziko ni afazali kuliko konzi mbili za kazi ngumu na kufuatilia upepo.’​—Mhubiri 4:6.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine