Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g18 na. 3 uku. 14-15
  • Musaada wa Muzuri Zaidi kwa Wale Wenye Wamefiwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Musaada wa Muzuri Zaidi kwa Wale Wenye Wamefiwa
  • Amuka!—2018
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • UJIFUNZE MENGI ZAIDI KUHUSU TUMAINI KWA AJILI YA WATU WENYE WAMEKUFA
  • Habari zenye kuwa ndani
    Amuka!—2018
  • Musaada kwa Wale Wenye Wamefiwa na Mupendwa Wao
    Amuka!—2018
  • Watu wa Familia na Marafiki Wako Wenye Walishakufa Wanaweza Kuishi Tena!
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Mambo Yenye Unapaswa Kutazamia
    Amuka!—2018
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2018
g18 na. 3 uku. 14-15
Katika Paradiso, watu wako tayari kukaribisha wapendwa wao wenye wamefufuliwa

MUSAADA KWA WALE WENYE WAMEFIWA NA MUPENDWA WAO

Musaada wa Muzuri Zaidi kwa Wale Wenye Wamefiwa

HIVI KARIBUNI, WATU WENGI WAMETAFUTA HABARI ZAIDI JUU YA MAUMIVU YENYE MUTU ANAPATA WAKATI ANAFIWA NA MUTU MWENYE ANAPENDA. Lakini, kama vile tumekwisha kuzungumuzia, mashauri ya muzuri zaidi yenye yametolewa na watu wenye elimu, mara nyingi yanapatana na hekima ya zamani yenye kupatikana mu Biblia. Hilo linaonyesha wazi kuwa muongozo wa Biblia ni wenye faida sikuzote. Hata hivyo, Biblia iko na mambo mengi zaidi ya mashauri yenye kutumainika. Inatoa habari zenye haziwezi kupatikana fasi zingine, habari zenye zinaweza kuletea kitulizo wale wenye kuwa na huzuni ya kufiwa.

  • Inatuhakikishia kwamba wapendwa wetu wenye wamekufa hawateseke

    Katika Muhubiri 9:5, Biblia inasema hivi: “Wafu hawajue kitu chochote.” ‘Mawazo yao yanapotea.’ (Zaburi 146:4) Kufuatana na jambo hilo, Biblia inalinganisha kifo na usingizi muzito.​—Yohana 11:11.

  • Kuwa na imani yenye nguvu katika Mungu mwenye upendo kunaleta kitulizo

    Katika Zaburi 34:15, Biblia inasema hivi: “Macho ya Yehovaa yako juu ya wenye haki, na masikio yake yanasikiliza kilio chao cha kuomba musaada.” Wakati tunamuambia Mungu katika sala namna tunajisikia, tunapata kitulizo zaidi kuliko kitulizo chenye tunaweza kupata kwa kuambia mutu fulani ao kwa kutumia njia fulani ya kuzuia mawazo yetu. Kufanya vile kunatusaidia kuanzisha uhusiano wa pekee pamoja na Muumbaji wetu, mwenye anaweza kutumia nguvu zake ili kutupatia kitulizo.

  • Inatupatia tumaini kwa ajili ya wakati wenye kuja wa muzuri zaidi

    Wazia namna mambo itakuwa wakati watu wenye kuwa katika makaburi wataishi tena katika dunia! Biblia inazungumuzia wakati huo mara nyingi. Ili kuonyesha namna hali itakuwa katika dunia wakati huo, Biblia inasema kama Mungu “atapanguza kila chozi katika macho yao, na kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu havitakuwa tena.”​—Ufunuo 21:3, 4.

Watu wengi wenye kumuamini Yehova, Mungu mwenye kutajwa mu Biblia, wanapata kabisa nguvu ya kupambana na huzuni yao juu wako na imani kuwa wataona tena wapendwa wao wenye wamekufa. Kwa mufano, Ann, mwenye alifiwa na bwana yake wa miaka 65, anasema hivi: “Biblia inanihakikishia kuwa wapendwa wetu wenye wamekufa hawateseke na kuwa Mungu atafufua wale wote wenye kuwa mu kumbukumbu lake. Nakumbuka mambo hayo wakati wowote nafikiria kifo cha mupendwa wangu, na matokeo ni kwamba, sasa niko na uwezo wa kupambana na jambo la mubaya zaidi lenye limekwisha kunifikia!”

Tiina, mwenye tumekwisha kuzungumuzia katika gazeti hili, anasema hivi: “Tangu siku Timo akufe, Mungu amekuwa akinitegemeza. Nimeona kabisa mukono wa Yehova ukinisaidia wakati wa magumu. Na ahadi ya Mungu kuhusu ufufuo ni ya kweli kabisa kwangu. Inanitia nguvu kusonga mbele mupaka wakati wenye nitamuona tena Timo.”

Maneno hayo yanapatana na maneno ya mamilioni ya watu wenye kuwa hakika kama Biblia inasemaka kweli. Hata kama unawaza kuwa mambo yenye Biblia inasema haiko ya kweli ao ni ndoto tu, unapaswa kutafuta ushuhuda wenye kuonyesha kuwa mashauri na ahadi zake ni za kweli. Bila shaka utaona kuwa Biblia inatoa musaada wa muzuri zaidi kwa wale wenye kuwa na huzuni ya kufiwa.

UJIFUNZE MENGI ZAIDI KUHUSU TUMAINI KWA AJILI YA WATU WENYE WAMEKUFA

Angalia Video juu ya habari hii kwenye site yetu ya Enternete, jw.org

Katika Paradiso, watu wako tayari kukaribisha wapendwa wao wenye wamefufuliwa

Biblia inaahidi kuwa wakati wenye kuja tutakaribisha wapendwa wetu wenye wamekufa

WATU WENYE WAMEKUFA WAKO KATIKA HALI GANI?

Watu Wenye Wamekufa Wako Katika Hali Gani?

Ni nini inatokea wakati mutu anakufa? Jibu la Biblia lenye kuwa wazi linatuliza na kutia moyo

Fungua kichwa VICHAPO > VIDEO (Ona chini ya kichwa Video: Biblia)

UTAPENDA KUSIKIA HABARI NJEMA?

Utapenda Kusikia Habari Njema?

Kwa kuwa habari za mubaya ziko nyingi sana, ni wapi unaweza kupata habari njema? Video hii inatanguliza broshua Habari Njema Inayotoka kwa Mungu!

Fungua kichwa VICHAPO > VIDEO (Ona chini ya kichwa Video: Mikutano na kazi yetu ya Mahubiri)

a Yehova ni jina la pekee la Mungu kama vile inaonyeshwa mu Biblia.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine