Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g19 na. 2 uku. 8-9
  • Namna ya Kupambana na Magumu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna ya Kupambana na Magumu
  • Amuka!—2019
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • KUJUA KUPAMBANA NA MAGUMU MAANA YAKE NINI?
  • JUU YA NINI NI JAMBO LA MAANA MUTOTO AJUE KUPAMBANA NA MAGUMU?
  • NAMNA YA KUMUSAIDIA AJUE KUPAMBANA NA MAGUMU
  • Niko na Roho Nguvu?
    Vijana Wanauliza
  • Namna ya Kusaidia Watoto Wakati Wanashindwa Kufanya Jambo Fulani
    Musaada kwa Familia
  • Kufundisha Watoto Unyenyekevu
    Amuka!—2017
  • Namna ya Kusifu Watoto
    Amuka!—2015
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2019
g19 na. 2 uku. 8-9
Mama anasaidia mutoto wake mwanamuke mwenye anajisikia mubaya juu keki yenye alitengeneza haikutoka muzuri

SOMO LA 3

Namna ya Kupambana na Magumu

KUJUA KUPAMBANA NA MAGUMU MAANA YAKE NINI?

Mutu mwenye kujua kupambana na magumu, anajisikia muzuri haraka na kuendelea na maisha kisha kupatwa na jambo fulani la mubaya. Mutu anakomalishaka ule uwezo kisha kupatwa na jambo fulani mu maisha. Kama vile tu mutoto hawezi kujifunza namna ya kutembea bila kuanguka wakati fulani, hawezi kujifunza namna ya kuweza mu maisha bila kupata magumu wakati fulani.

JUU YA NINI NI JAMBO LA MAANA MUTOTO AJUE KUPAMBANA NA MAGUMU?

Watoto fulani wanavunjika moyo wakati wanashindwa kufanya jambo fulani, wanapatwa na hali ngumu, ao wakati wanaonyeshwa makosa yenye wamefanya. Wengine wanavunjika moyo kabisa. Lakini, wanapaswa kuelewa mambo yenye kufuata yenye ni ya kweli:

  • Sikuzote hatuwezi kupata matokeo ya muzuri mu kila jambo lenye tunafanya.​—Yakobo 3:2.

  • Kila mutu anafikia kupatwa na magumu mu maisha.​—Muhubiri 9:11.

  • Mutu iko na lazima ya kuonyeshwa makosa yake ili afanye maendeleo.​—Mezali 9:9.

Kufundisha mutoto namna ya kupambana na hali fulani ya mubaya kutamusaidia akuwe hakika kama anaweza kupambana na magumu ya maisha na kupata ushindi.

NAMNA YA KUMUSAIDIA AJUE KUPAMBANA NA MAGUMU

Wakati mutoto wako anashindwa kufanya jambo fulani.

KANUNI YA BIBLIA: “Mwenye haki anaweza kuanguka mara saba (7), na atasimama tena.”​—Mezali 24:16.

Saidia mutoto wako akuwe na uwezo wa kujua ikiwa tatizo ni kubwa ao hapana. Kwa mufano, anaweza kufanya nini kama anashindwa mashindano fulani ku masomo? Anaweza kuvunjika moyo na kusema, “Hakuna kitu chenye nitawezaka kufanya muzuri!”

Ili kumufundisha namna ya kupambana na ile hali, umusaidie afikirie namna anaweza kufanya muzuri zaidi wakati wenye kuja. Mu ile njia atajikaza kumaliza tatizo kuliko kuendelea kuumia.

Wakati uleule, usimalize tatizo la mutoto wako pa nafasi yake. Lakini umusaidie ajue namna ya kumaliza tatizo lake. Unaweza kumuuliza, “Unaweza kufanya nini ili uweze kuelewa muzuri zaidi habari yenye mwalimu anafundisha?”

Wakati mambo ya mubaya inatokea.

KANUNI YA BIBLIA: “Hamujue maisha yenu yatakuwa namna gani kesho.”​—Yakobo 4:14.

Hakuna mutu mwenye anajua namna maisha yake ya kesho itakuwa. Mutu mwenye kuwa tajiri leo anaweza kuwa maskini kesho na mutu mwenye kuwa na afya ya muzuri leo anaweza kuwa mugonjwa kesho. Biblia inasema hivi: “Haiko wenye mbio ndio wanashinda kila mara katika mbio, wala haiko wenye nguvu ndio wanashinda katika vita, . . . kwa sababu wakati na matukio yenye hayatazamiwe yanafikia wote.”​—Muhubiri 9:11.

Ukiwa muzazi, unafanya nguvu yako yote ili kulinda watoto wako wasipatwe na hatari. Lakini kusema kweli, haiwezekane kulinda mutoto wako na kila jambo la mubaya mu maisha.

Ni kweli kwamba, pengine mutoto wako hawezi kujua namna mutu anajisikia wakati anapoteza kazi ao wakati iko na matatizo ya feza juu angali mutoto mudogo. Lakini, unaweza kumusaidia kupambana na magumu ingine; kama vile, wakati urafiki wake pamoja na mutu fulani unaisha ao wakati mutu wa familia anakufa.a

Wakati mutoto wako anaambiwa kama anapaswa kubadilika.

KANUNI YA BIBLIA: “Sikiliza shauri . . . ili ukuwe na hekima katika wakati wako wenye kuja.”​—Mezali 19:20.

Wakati mutu fulani anaonyesha mutoto wako kama anapaswa kubadilika, hafanye vile ili kumuogopesha ao kumuumiza lakini anapenda kumusaidia abadilishe tabia ao mwenendo fulani wenye unapaswa kubadilishwa.

Wakati unafundisha mutoto wako akubali kurekebishwa, nyinyi wote wawili munapata faida. Baba mumoja mwenye kuitwa John anasema kama “ikiwa sikuzote hatuache watoto warekebishe makosa yao, hawatajifunza hata kidogo. Wataendelea kuwa na matatizo mingi mu maisha yao, na ukiwa muzazi utakuwa tu na kazi ya kumaliza matatizo yao. Ile inafanya maisha ikuwe ya mubaya sana kwa wazazi na kwa mutoto.”

Namna gani unaweza kusaidia mutoto wako apate faida wakati anarekebishwa? Wakati mutoto wako anarekebishwa​—ikuwe ku masomo ao fasi ingine​—usiseme kama wamemuonea. Lakini unaweza kumuuliza:

  • “Unawaza ni juu ya nini walikurekebisha?”

  • “Namna gani unaweza kufanya mabadiliko?”

  • “Utafanya nini wakati utakuwa tena katika hali hii?”

Kumbuka kama, kurekebishwa kutasaidia mutoto wako, hapana leo tu lakini pia wakati atakuwa mukubwa.

a Ona habari “Msaidie Mtoto Wako Akabiliane na Huzuni,” mu gazeti Munara wa Mulinzi wa tarehe 1, Mwezi wa 7, 2008.

Mama anasaidia mutoto wake mwanamuke mwenye anajisikia mubaya juu keki yenye alitengeneza haikutoka muzuri

UMUZOEZE KUANZIA LEO

Mutoto mwenye anafikia kujifunza kupitia makosa yake na mwenye havunjike moyo, ataweza pia kujifunza ufundi mupya na kuujua muzuri hata kama ufundi huo unaweza kuwa nguvu kujifunza

Ufundishe Kupitia Mufano

  • Je, ninakubali makosa yangu, ao ninatupia wengine makosa yangu?

  • Ninazungumuza kuhusu mambo yenye nilishindwa kufanya na kile nilijifunza kupitia ile mambo?

  • Ninacheka wengine kwa sababu ya makosa yao?

Mambo Yenye Tulifanya . . .

“Hatukulinda watoto wetu kutokana na kila magumu, kushindwa, ao kila kosa. Wakati nilikuwa kijana, kuvumilia ile mambo yote kulinifanya nikuwe mutu muzuri zaidi. Ninawaza kama watoto wetu wote wawili walikomaa wakiwa wenye usawaziko na wenye kufikiri muzuri juu hatukuwabembeleza.”​—Jeff.

“Wakati mimi na bibi yangu tulikosea watoto wetu, kila mara tuliomba musamaha. Nawaza kama wazazi wanapaswa kuzungumuza pamoja na watoto wao juu ya makosa yao wenyewe na vizuizi vyenye walikutana navyo ili kuwasaidia waelewe kama ile ni mambo ya kawaida mu maisha.”​—James.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine