Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g20 na. 1 uku. 5-7
  • Mukazo Ni Nini?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mukazo Ni Nini?
  • Amuka!—2020
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MUKAZO WA MUZURI NA WA MUBAYA
  • Habari Zenye Kuwa Ndani
    Amuka!—2020
  • Uko na Mukazo?
    Amuka!—2020
  • Namna ya Kupambana na Mukazo
    Amuka!—2020
  • Namna ya Kushinda—Mahangaiko ya Akili
    Amuka!—2014
Amuka!—2020
g20 na. 1 uku. 5-7
Katika muji, mwanaume mumoja mufanyabiashara iko anakimbilia mbio ku biro.

KITULIZO KWA WALE WENYE KUWA NA MUKAZO

Mukazo Ni Nini?

Mukazo ni namna mwili wetu unatenda wakati tuko mbele ya hali ngumu. Ubongo wako unatuma hormone mingi katika sehemu zote za mwili. Hormone hizo zinafanya moyo uanze kupiga mbiombio, zinabadilisha mwendo wa damu, zinapanua ao kufinya mapafu (mafafa), na zinakaza misuli yako. Mbele utambue kabisa jambo lenye kutendeka, mwili wako uko tayari kwa ajili ya kutenda. Wakati hali fulani yenye kuleta mahangaiko inamalizika, “mushtuko” unamalizika na mwili unarudia tena mu hali ya kawaida.

MUKAZO WA MUZURI NA WA MUBAYA

Mukazo ni uwezo wa kawaida wenye unatusaidia kupambana na tatizo ao hatari fulani. Hali hiyo inaanzia katika ubongo wetu. Mukazo wa muzuri unatusaidia tutende haraka. Kiasi fulani cha mukazo kinaweza kutusaidia kufikia miradi yetu ao kupata matokeo ya muzuri, pengine wakati wa mashindano ku masomo, wakati tunaulizwa maulizo kuhusu kazi, ao wakati wa muchezo fulani.

Lakini, mukazo wenye kuendelea, wenye kuvuka mipaka, ao wenye kukawia unaweza kukuletea matokeo ya mubaya. Wakati unajikuta kila mara katika mukazo ao uko na mukazo wenye kuendelea unaweza kuanza kuteseka kimwili, kihisia, na kiakili. Tabia yako, kutia ndani namna unatendea wengine vinaweza kubadilika. Mukazo wenye kuendelea unaweza pia kufanya mutu aanze kunywa pombe kupita kiasi, kutumia dawa za kulewesha na kufanya mambo ingine yenye haifae ili kujaribu kumaliza mukazo. Mukazo unaweza hata kukufanya ushuke moyo, uchoke kimwili na kiakili, ao kukufanya ukuwe na mawazo ya kujiua.

Hata kama mukazo hauwezi kuwa na matokeo ileile kwa kila mutu, unaweza kuleta magonjwa mingi. Na mukazo unaweza kugusa karibu kila sehemu ya mwili.

MATOKEO YA MUKAZO JUU YA MWILI WAKO

Mishipa ya ufahamu.

Mwanaume mumoja mwenye kutia mukono wake ku uso, iko na mukazo.

Mishipa yako ya ufahamu inafanya hormone mbalimbali kama vile adrenalini na cortisol zitokee. Hormone hizo zinafanya moyo upige mbiombio na zinaongeza mwendo wa damu na kiasi cha sukari katika damu yako. Ile yote ni juu uweze kutenda haraka wakati hatari inatokea. Mukazo wenye kuvuka mipaka unaweza kufanya mutu

  • akuwe mwenye kukasirika-kasirika, akuwe na wasiwasi, ashuke moyo, akuwe na maumivu ya kichwa, akose usingizi

Misuli na mifupa.

Misuli yako inasimama ili kukulinda usiumie. Mukazo wenye kuvuka mipaka unaweza kutokeza

  • maumivu ya mwili, kichwa kuuma sana, mushtuko wa misuli (crampe)

Uwezo wa kupumua.

Unapumua haraka sana ili kuvuta oksijeni mingi zaidi. Mukazo wenye kuvuka mipaka unaweza

  • kufanya mutu apumue haraka-haraka na akose pumuzi, na pia kufanya mutu akuwe na woga sana

Moyo.

Moyo wako unapiga haraka sana na kwa nguvu ili kupeleka damu katika mwili wote. Mishipa ya damu inapanuka ao kufinywa ili kupeleka damu fasi kwenye mwili uko nayo lazima sana, kama vile katika misuli yako. Mukazo wenye kuvuka mipaka unaweza

  • kuongeza mwendo wa damu, kuleta ugonjwa wa moyo, kuleta ugonjwa wa kupooza

Uwezo wa kutokeza hormone.

Tezi (glandes) zako zinatokeza hormone zenye kuitwa adrenalini na cortisol, zenye zinasaidia mwili utende wakati wa mukazo. Maini yako inafanya sukari yenye kuwa ndani ya damu iongezeke ili upate nguvu mingi. Mukazo wenye kuvuka mipaka unaweza

  • kutokeza ugonjwa wa sukari, kupunguza uwezo wa mwili wa kujikinga na kufanya mutu ashambuliwe na magonjwa, kufanya hisia za mutu zikuwe zinabadilika-badilika, kufanya kilo ya mutu iongezeke

Uwezo wa mwili wa kusaga na kutumia chakula.

Mukazo unafanya tumbo isifanye kazi kama kawaida kisha mutu kula chakula. Mukazo wenye kuvuka mipaka unaweza kufanya mutu

  • ajisikie kama anataka kutapika, atapike, apate ugonjwa wa kuhara, na akose choo

Uwezo wa kuzaa.

Mukazo unaweza kuwa na matokeo juu ya tamaa ya kufanya ngono na juu ya namna ya kutumika ya viungo vya uzazi. Mukazo wenye kuvuka mipaka unaweza

  • kufanya mwanaume akose nguvu ya kufanya ngono, kuvuruga siku za mwanamuke za kuona mwezi

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine