4. Mungu Alituumba Juu Tuteseke?
Juu ya Nini Ni Muzuri Kujiuliza Vile?
Juu jibu la ulizo hilo linaweza kubadilisha namna yetu ya kuona maisha.
Jambo la Kufikiria
Juu ya nini Mungu mwenye aliumba vitu vyenye kupendeza anaruhusu mateso?
Watu wenye hawapendezwe na mambo ya dini wanaona mateso kuwa sababu ya kushakia mipango ya Mungu, na hata kuwa na mashaka kama yeye iko. Wanaamini kuwa mateso inaonyesha kama, ao (1) Mungu hana nguvu ya kumaliza mateso, ao (2) Mungu hahangaike kumaliza mateso, ao (3) Mungu hakuwake.
Kwa kweli, zile njo sababu zenye zinafanya watu wateseke?
IKIWA UNAPENDA KUJUA MINGI ZAIDI
Angalia video Namna Gani Tunaweza Kuwa Hakika Kama Biblia Inasema Kweli? yenye kuwa ku jw.org.
Mambo Yenye Biblia Inasema
Mungu hakutuumba juu tuteseke.
Anapenda tufurahie maisha.
“Hakuna jambo la muzuri zaidi [kwa watu] kuliko kufurahi na kufanya mema wakati wa maisha yao, na kwamba kila mutu anapaswa kula na kunywa na kufurahia kazi yake yote ya nguvu. Ni zawadi ya Mungu.”—MUHUBIRI 3:12, 13.
Mungu alipatia wanadamu wawili wa kwanza kila kitu chenye walikuwa nacho lazima ili waishi bila mateso.
Hakuwaumba juu wao ao watoto wao wateseke.
“Mungu akawaambia: ‘Muzae na mukuwe wengi, mujaze dunia na kuitawala.’”—MWANZO 1:28.
Wanadamu wa kwanza wawili walichagua kukosa kumutii Mungu
Matokeo ni kuwa walijeletea mateso wao wenyewe na watoto wao wote.
“Kupitia mutu mumoja zambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia zambi, na ni vile kifo kilienea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya zambi.”—WAROMA 5:12.a
Mungu hakutuumba na uwezo wa kujiongoza.
Sawa vile tu haiwezekane wanadamu kuishi ndani ya maji, ni vile pia haiwezekane wao wenyewe kujitawala.
“Mwanadamu mwenye kutembea hana hata uwezo wa kuongoza hatua yake.”—YEREMIA 10:23.
Mungu hapendi tuteseke.
Anapenda tuepuke matatizo kwa kadiri inawezakana.
“Kama tu ungesikiliza amri zangu! Basi amani yako ingekuwa kama vile muto.”—ISAYA 48:18.
a Katika Biblia, neno “zambi” halimaanishe tu jambo la mubaya, lakini linamaanisha pia hali yenye wanadamu wotewameriti.