Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g20 na. 2 uku. 12-13
  • 4. Mungu Alituumba Juu Tuteseke?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 4. Mungu Alituumba Juu Tuteseke?
  • Amuka!—2020
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Juu ya Nini Ni Muzuri Kujiuliza Vile?
  • Jambo la Kufikiria
  • Mambo Yenye Biblia Inasema
  • Mambo Biblia Inasema Juu ya Mateso
    Amuka!—2015
  • Habari Zenye Kuwa Ndani
    Amuka!—2020
  • Biblia Inasema Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Ulizo la 3: Sababu Gani Mungu Anaacha Niteseke?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2020
g20 na. 2 uku. 12-13
Familia inapiga kambi ku mulima. Familia iko inajikamata picha na mulima uko nyuma yao.

4. Mungu Alituumba Juu Tuteseke?

Juu ya Nini Ni Muzuri Kujiuliza Vile?

Juu jibu la ulizo hilo linaweza kubadilisha namna yetu ya kuona maisha.

Jambo la Kufikiria

Juu ya nini Mungu mwenye aliumba vitu vyenye kupendeza anaruhusu mateso?

Watu wenye hawapendezwe na mambo ya dini wanaona mateso kuwa sababu ya kushakia mipango ya Mungu, na hata kuwa na mashaka kama yeye iko. Wanaamini kuwa mateso inaonyesha kama, ao (1) Mungu hana nguvu ya kumaliza mateso, ao (2) Mungu hahangaike kumaliza mateso, ao (3) Mungu hakuwake.

Kwa kweli, zile njo sababu zenye zinafanya watu wateseke?

IKIWA UNAPENDA KUJUA MINGI ZAIDI

Angalia video Namna Gani Tunaweza Kuwa Hakika Kama Biblia Inasema Kweli? yenye kuwa ku jw.org.

Mambo Yenye Biblia Inasema

Mungu hakutuumba juu tuteseke.

Anapenda tufurahie maisha.

“Hakuna jambo la muzuri zaidi [kwa watu] kuliko kufurahi na kufanya mema wakati wa maisha yao, na kwamba kila mutu anapaswa kula na kunywa na kufurahia kazi yake yote ya nguvu. Ni zawadi ya Mungu.”​—MUHUBIRI 3:12, 13.

Mungu alipatia wanadamu wawili wa kwanza kila kitu chenye walikuwa nacho lazima ili waishi bila mateso.

Hakuwaumba juu wao ao watoto wao wateseke.

“Mungu akawaambia: ‘Muzae na mukuwe wengi, mujaze dunia na kuitawala.’”​—MWANZO 1:28.

Wanadamu wa kwanza wawili walichagua kukosa kumutii Mungu

Matokeo ni kuwa walijeletea mateso wao wenyewe na watoto wao wote.

“Kupitia mutu mumoja zambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia zambi, na ni vile kifo kilienea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya zambi.”​—WAROMA 5:12.a

Mungu hakutuumba na uwezo wa kujiongoza.

Sawa vile tu haiwezekane wanadamu kuishi ndani ya maji, ni vile pia haiwezekane wao wenyewe kujitawala.

“Mwanadamu mwenye kutembea hana hata uwezo wa kuongoza hatua yake.”​—YEREMIA 10:23.

Mungu hapendi tuteseke.

Anapenda tuepuke matatizo kwa kadiri inawezakana.

“Kama tu ungesikiliza amri zangu! Basi amani yako ingekuwa kama vile muto.”​—ISAYA 48:18.

a Katika Biblia, neno “zambi” halimaanishe tu jambo la mubaya, lakini linamaanisha pia hali yenye wanadamu wotewameriti.

Mungu alituumba juu tuteseke?

Hapana. Mateso haikukuwaka hata kidogo katika kusudi la Mungu kwa wanadamu. Mateso ilianza wakati wanadamu wa kwanza wawili walichagua kukosa kumutii Mungu. Lakini, ile haimaanishe kama wanadamu wataendelea kuteseka milele.

Mateso yetu itaishaka?

Pata jibu kwenye ulizo la 5.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine