Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g20 na. 2 uku. 14-15
  • 5. Mateso Itaishaka?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 5. Mateso Itaishaka?
  • Amuka!—2020
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Juu ya Nini Ni Muzuri Kujiuliza Vile?
  • Jambo la Kufikiria
  • Mambo Yenye Biblia Inasema
  • Biblia Inasema Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Mambo Biblia Inasema Juu ya Mateso
    Amuka!—2015
  • Ulizo la 3: Sababu Gani Mungu Anaacha Niteseke?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Mungu Anajisikia Namna Gani Juu ya Mateso Yako?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2018
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2020
g20 na. 2 uku. 14-15
Familia iko inajifurahisha pembeni ya maji. Wako wanacheka na kupitisha wakati pamoja.

5. Mateso Itaishaka?

Juu ya Nini Ni Muzuri Kujiuliza Vile?

Juu kama kuko sababu ya kuamini kuwa mateso itaishaka, ile itafanya tukuwe na mawazo ya muzuri kuhusu maisha na kumuhusu Mungu.

Jambo la Kufikiria

Watu wengi wangependa kumaliza mateso, lakini hawana uwezo wa kutosha wa kufanya vile. Ona mifano yenye kufuata:

Hata kama kumekuwa maendeleo mu mambo ya kinganga . . .

  • Ugonjwa wa moyo unaendelea kuua watu wengi sana.

  • Kansere inaua mamilioni ya watu kila mwaka.

  • Katika gazeti moja (Frontiers in Immunology), David Bloom, mutu mwenye elimu mingi, aliandika hivi: “Watu wanaendelea kupambana na magonjwa ya zamani na ya sasa, na hata wanapambana na magonjwa ingine yenye haijakuwaka tangu zamani.”

Hata kama inchi fulani ziko na utajiri mwingi . . .

  • Kila mwaka, mamilioni ya watoto wanakufa, zaidi sana mu maeneo kwenye watu wako maskini.

  • Mamiliare ya watu wanaishi mu maeneo yenye haiko safi.

  • Mamia ya mamilioni hawana maji safi.

Hata kama watu wengi wanajua haki za wanadamu . . .

  • Ripoti moja ya Umoja wa Mataifa inasema kama, biashara ya kuuzisha watu inaendelea katika inchi na maeneo mingi, na watu wenye wanafanya vile hawapewe malipizi. Ile ni kwa sababu wenye mamlaka ao “hawajue mambo yenye iko inafanyika, ao hawana uwezo wa kutosha wa kumaliza tatizo hilo.”

    IKIWA UNAPENDA KUJUA MINGI ZAIDI

    Angalia video Ufalme wa Mungu Ni Nini? yenye kuwa ku jw.org.

Mambo Yenye Biblia Inasema

Mungu anatuhangaikia.

Anahangaikia maumivu na huzuni yetu.

“[Mungu] hajazarau wala kuchukizwa na mateso ya ule mwenye kukandamizwa; hajamuficha uso wake. Wakati alimulilia amusaidie, alisikia.”​—ZABURI 22:24.

“Mumutupie mahangaiko yenu yote, kwa sababu yeye anawahangaikia ninyi.”​—1 PETRO 5:7.

Mateso haitaendelea milele.

Biblia inatuambia kama kusudi la Mungu litatimia.

“Mungu . . . atapanguza kila chozi katika macho yao, na kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu havitakuwa tena.”​—UFUNUO 21:3, 4.

Mungu atamaliza mambo yenye inafanya wanadamu wateseke.

Atafanya vile kupitia Ufalme wake, wenye Biblia inaonyesha kama ni serikali ya kweli.

“Mungu wa mbinguni atasimamisha ufalme wenye hautaharibiwa hata siku moja. Na ufalme huo hautapewa watu wengine wowote. . . . Ufalme huo peke yake utasimama milele.”​—DANIELI 2:44.

Mateso Itaishaka?

Ndiyo, lakini hapana kwa nguvu ya wanadamu. Serikali za wanadamu zinaweza tu kujaribu kutuliza mateso yetu, lakini Mungu atamaliza mambo yenye inafanya tuteseke. Atafanya vile kupitia Ufalme wake.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine