Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g21 na. 1 uku. 12-13
  • Mafundisho Yenye Inatupatia Tumaini

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mafundisho Yenye Inatupatia Tumaini
  • Amuka!—2021
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mungu Atatosha Watu Wabaya
  • Mungu Atamuharibu Shetani
  • Mungu Atamaliza Magonjwa na Kifo
  • Muumbaji Wetu Atageuza Hii Dunia Kuwa Paradiso
  • Mungu Atafufula Wafu
  • Kusudi la Mungu Ni Nini Kuhusu Dunia?
    Mungu Anataka Nini Kwetu?
  • Mungu Ana Kusudi Gani juu ya Dunia?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Marafiki Wa Mungu Wataishi Katika Paradiso
    Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!
  • Mwisho wa Mateso Unakaribia!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2021
g21 na. 1 uku. 12-13
Watu wanaishi kwa amani na wanyama, wako mu paradiso ya muzuri na wako na chakula ya mingi.

Mafundisho Yenye Inatupatia Tumaini

Mungu alishalaga kama mu masiku ya mbele kutakuwa mabadiliko ya ajabu. Atamaliza mateso na kupatia wanadamu maisha ya furaha hapa ku dunia. (Zaburi 37:11) Juu ya nini tuamini ile mambo? Ni juu “Mungu haiko mwanadamu bure mwenye anasemaka uongo.” (Hesabu 23:19) Tuone mambo ya muzuri yenye Muumbaji wetu atafanya.

Mungu Atatosha Watu Wabaya

“Wakati waovu wanachipuka kama magugu na wakati wakosaji wote wanasitawi, ni ili waharibiwe milele.”​—ZABURI 92:7.

Vile tuliona mu habari yenye ilipita, mambo ya mubaya iko naendelea kuongezeka. Ile haipaswe kutushangaza. Mu 2 Timoteo 3:1-5, Biblia ilikuwa ilishaonyesha kama mu “siku za mwisho” watu wangekuwa wabaya sana. Siku za mwisho za nini? Siku za mwisho za watu wenye hawamuogope Mungu. Mungu iko karibu kuharibu watu wote wenye wanakatala kubadilisha mwenendo yao ya mubaya. Ni watu wazuri tu, ni kusema wale wenye wanamutii Mungu, njo watabakia ku dunia. “Wenye haki watariti dunia, na wataishi milele juu yake.”​—Zaburi 37:29.

Mungu Atamuharibu Shetani

“Mungu mwenye anatoa amani atamuponda Shetani.”​—WAROMA 16:20.

Wakati Shetani na pepo wachafu hawatakuwa tena, na wakati mambo yote ya mubaya haitakuwa tena, amani itayala mu dunia yote. Muumbaji wetu anasema hivi: ‘Hakuna mutu mwenye atakuogopesha.’​—Mika 4:4.

Mungu Atamaliza Magonjwa na Kifo

“Hema ya Mungu iko pamoja na wanadamu . . . Na atapanguza kila chozi katika macho yao, na kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu havitakuwa tena.”​—UFUNUO 21:3, 4.

Mateso na magonjwa itaisha sababu Mungu atatosha mambo yote ya mubaya yenye iko natupata juu ya Shetani, Adamu, Eva, na juu ya hali yetu ya kukosa kukamilika. Na hata “kifo hakitakuwa tena.” Watu wenye wanamupenda Muumbaji wetu na kumutii, wataishi milele. Wataishi milele wapi?

Muumbaji Wetu Atageuza Hii Dunia Kuwa Paradiso

“Jangwa na inchi yenye kukauka vitafurahi, jangwa tambarare litashangilia na kutoa maua kama zafarani.”​—ISAYA 35:1.

Wakati Mungu atatosha mambo yote ya mubaya, dunia itakuwa paradiso! Mu dunia mutakuwa mabustani ya mingi ya muzuri na kutakuwa chakula ya mingi. (Zaburi 72:16) Bahari na mitoni itakuwa na maji yenye kuwa safi. Na mu ile maji mutakuwa viumbe mingi vyenye kuwa na uzima. Watu hawatakumbuka tena kama dunia ilikuwaka buchafu. Watu wataishi mu manyumba yenye wao wenyewe walijijengea. Hakuna tena mutu mwenye atakosaka nyumba, mwenye atakuwaka na njaa, ao mwenye atakuwaka maskini.​—Isaya 65:21, 22.

Mungu Atafufula Wafu

“Kutakuwa ufufuo.”​—MATENDO 24:15.

Utapenda kuona tena wapendwa wako wenye walishakufa? Mungu Mweza-Yote atawapatia tena uzima, ni kusema, atawafufula na wataishi mu paradiso hapa ku dunia. Utawajua na wao watakujua. Wazia namna mutafurahi wakati mutaonana tena! Juu ya nini tuko hakika kama ile jambo itatimia kabisa? Ni juu Biblia inatutolea mifano ya watu wakubwa na watoto wenye walifufuliwaka, na wakaonana tena na watu wa familia yao. Zaidi ya ile, mara mingi Yesu alifufua watu mbele ya mashahidi wengi.​—Luka 8:49-56; Yohana 11:11-14, 38-44.

Niko Sasa Mwenye Furaha Kabisa

“Nakumbuka wakati nilisikia kwa mara ya kwanza kama kutakuwa paradiso mu dunia. Na mu ile paradiso hamutakuwa mateso, hamutakuwa magonjwa na hamutakuwa kifo. Niliwazaka kama mambo ya vile haitawezekana hata kidogo! Lakini wakati nilijifunza Biblia, nilielewa kabisa sababu gani napaswa kuamini mambo yenye ile kitabu inasema juu ya wakati wenye kuja. Niko hakika kabisa kama Biblia ilitoka kwa Mungu. Zamani, nilikuwa mutu wa kuogopa-ogopa na mwenye kuwa na huzuni. Lakini sasa, niko mwenye furaha kabisa. Hata watu wa familia yangu na marafiki wangu wanaweza kuona kabisa kama nilishakuwa mutu mwenye furaha.”​—Ravi.

Ravi.

Ikiwa unapenda kujua mingi zaidi:

Ukipenda kujua mambo ingine yenye Muumbaji atafanyia wanadamu wenye wataishi milele mu dunia paradiso, fungua jw.org chini ya kichwa MAFUNDISHO YA BIBLIA > MAJIBU YA MAULIZO JUU YA BIBLIA > UZIMA NA KIFO.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine