Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g21 na. 3 uku. 14-15
  • Juu ya Nini Ni Jambo ya Maana Kuamini Kama Kuko Muumbaji?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Juu ya Nini Ni Jambo ya Maana Kuamini Kama Kuko Muumbaji?
  • Amuka!—2021
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Utafurahia maisha zaidi
  • Utapata mashauri ya muzuri, yenye inaweza kukusaidia mu maisha
  • Utapata majibu ya maulizo yako
  • Utakuwa na tumaini
  • Mungu Anakuwaka? Faida 4 za Kujua Hivyo
    Amuka!—2015
  • Biblia Inafundisha Nini juu ya Mungu?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Bhayibele yi re ku Mahlong go sa Nyoko Natefa
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Biblia Inatupatia Tumaini
    Furahia Maisha Milele!—Anza Kujifunza Biblia
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2021
g21 na. 3 uku. 14-15
Marafiki wanafurahia kuangalia wanyama wenye wako ku muti.

Juu ya Nini Ni Jambo ya Maana Kuamini Kama Kuko Muumbaji?

Juu ya nini ni jambo ya maana kujua jibu ya ile ulizo? Kama ushuhuda mbalimbali unakusaidia uamini kama kuko Mungu, unaweza pia kupenda kuchunguza mambo yenye kuhakikisha kama yeye njo aliandikishaka Biblia. Na kama unaamini mambo yenye Biblia inasema, unaweza kufikia kupata faida mbalimbali zenye kuwa hapa chini.

Utafurahia maisha zaidi

BIBLIA INASEMA: ‘[Mungu] alitenda mema, aliwapatia ninyi mvua kutoka mbinguni na vipindi vya kuzaa matunda, na kuwapatia chakula kwa wingi na kujaza mioyo yenu furaha.’​—Matendo 14:17.

ILE IKO NA MAANA GANI?: Kila kitu yenye unafurahia mu vitu vyenye viliumbwa vyenye viko mu dunia, ni zawadi yenye Muumbaji ametupatia. Utafurahia zile zawadi hata zaidi, kama unafikia kuelewa namna mwenye alitupatia zile zawadi anakuhangaikia kabisa.

Utapata mashauri ya muzuri, yenye inaweza kukusaidia mu maisha

BIBLIA INASEMA: “Utaelewa mambo ya uadilifu na ya haki na yenye kunyooka; njia yote ya mambo ya muzuri.”​—Mezali 2:9.

ILE IKO NA MAANA GANI?: Juu Mungu njo alituumba, yeye njo anajua mambo yenye tuko nayo lazima juu tukuwe na furaha. Kama unachunguza mambo yenye Biblia inafundisha, unaweza kujifunza mambo mingi yenye itakusaidia mu maisha.

Utapata majibu ya maulizo yako

BIBLIA INASEMA: “Utapata ujuzi juu ya Mungu.”​—Mezali 2:5.

ILE IKO NA MAANA GANI?: Kujua kama kuko Muumbaji, kunaweza kukusaidia upate majibu ya maulizo ya maana, yenye watu wanajiulizaka. Kwa mufano: Juu ya nini tunaishi? Juu ya nini kuko mateso ya mingi? Mutu mwenye anakufa iko mu hali gani? Unaweza kupata majibu ya kweli mu Biblia.

Utakuwa na tumaini

BIBLIA INASEMA: “‘Ninajua muzuri mawazo yenye ninafikiria kuwaelekea ninyi,’ ni vile Yehova anasema, ‘mawazo ya amani, na hapana ya musiba, ili kuwapatia ninyi wakati wenye kuja wa muzuri na tumaini.’”​—Yeremia 29:11.

Ona video Namna Gani Tunaweza Kuwa Hakika Kama Biblia Inasema Kweli? na Ni Nani Aliandikisha Biblia? ku jw.org. Juu ya kupata zile video, kwenye sehemu ya kutafutia, andika maneno “Biblia inasema kweli” ao “nani aliandikisha Biblia.”

ILE IKO NA MAANA GANI?: Mungu anatuambia kama mu siku zenye ziko nakuya atamaliza mambo ya mubaya, mateso, na hata kifo. Wakati unaamini ahadi ya Mungu, utatumaini kama maisha itakuwa muzuri mu siku zenye ziko nakuya. Na ile itakusaidia ukuwe na nguvu ya kupiganisha magumu yenye uko napata.

Faida zenye watu fulani wamepata juu wameamini kama kuko Muumbaji

Cyndi.

“Nakuwaka nashangaa kila mara wakati naona namna Mungu iko natusaidia mu mambo mbalimbali mu maisha. Kwa mufano, anatusaidia tujue mambo ya maana mu maisha, tujue namna ya kuishi muzuri na wengine, na tujue mambo yenye tunaweza kufanya juu tukuwe marafiki wake.”​—Cyndi, Amerika.

Elise.

“Juu naamini kama kuko Muumbaji, niko na maisha ya muzuri, na yenye furaha. Sijisikiake kuwa nakosa mambo ya kufanya, sababu kuko mambo mingi yenye naweza kujifunza juu ya Muumbaji, juu ya vitu vyenye aliumba, na juu ya Neno yake.”​—Elise, Ufaransa.

Peter.

“Kutumikisha mambo yenye Muumbaji anatuambia mu Biblia, inanisaidia nikuwe na furaha. Inanisaidia nisikuwe mutu wa kuchambua-chambua mambo, nikuwe nahangaikia wengine, na nikuwe mwenye kutosheka zaidi. Tena, imenisaidia nikuwe baba muzuri zaidi.”​—Peter, Hollande.

Liz.

“Mbele, maisha yangu ilikuwa tu ni kula, kulala, na kujikaza juu nisichelewe ku kazi. Sikuwaka nafurahia maisha. Lakini sasa, naona uzima kuwa zawadi ya muzuri, yenye tunapaswa kufurahia na kuona kuwa ya maana.”​—Liz, Estonia.

Adrien.

“Nakuwaka na mahangaiko sana. Lakini, kujua kama mambo ya mubaya, ukosefu wa haki, na mateso vitaishaka inanisaidia nivumilie.”​—Adrien, Ufaransa.

Ona namna Biblia inajibia maulizo ya maana yenye watu wanajiulizaka mu maisha. Angalia video Sababu Gani Ujifunze Biblia?​—Video Yote.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine