Georgette Douwma/Stone via Getty Images
DUNIA ITAOKOKA KABISA?
BAHARI
BAHARI haitupatiake tu chakula yenye tunakulaka, lakini inatupatiaka pia vitu mbalimbali vyenye tuko navyo lazima ili kufanya dawa. Zaidi ya nusu ya oksijeni yenye kuwa mu ulimwengu inatokaka mu bahari, na bahari inakokotaka gaze za karbone zenye kuwa hatari kwa mwanadamu. Tena, bahari inasaidiaka hali ya hewa iendelee kuwa muzuri.
Mambo Yenye Kuharibisha Bahari
Kubadilika kwa hali ya hewa ni hatari kwa viumbe vya kidogo-kidog vyenye kuwa mu maji, sawa vile matumbawe (récifs coralliens), samaki-gamba (mollusques), na viumbe vingine vyenye kuwa mu maji. Wanasayansi wanasema kama karibu vile viumbe vyote vya kidogo-kidogo, vyenye vinategemeza asilimia 25 (25%) hivi ya viumbe vyenye uzima vyenye kuwa mu bahari, vinaweza kufa mu miaka 30 yenye iko nakuya.
Wanasayansi wanasema kama asilimia 90 (90%) hivi ya ndege wenye wanakulaka chakula mu bahari inawezekana walishakakula pia plastike. Na wanawaza kama plastike zenye kuwa mu bahari zinauaka mamilioni ya wanyama wenye kuwa mu bahari kila mwaka.
António Guterres, Katibu Mukubwa wa Umoja wa Mataifa (Secrétaire Générale des Nations Unis), alisema hivi mu 2022: “Hatuhangaikie kabisa bahari. Na leo, naweza kusema kama bahari iko mu hatari.”
Dunia Iliumbwa juu Iendelee Kuwa
Bahari na viumbe vyenye kuwa ndani viliumbwa juu viendelee kuwa safi na viendelee kuwa mu hali ya muzuri kama wanadamu hawaviharibishe. Kitabu fulani inafasiria kama, wakati wanadamu hawaharibishe bahari, inaweza kuendelea kujisafisha ayo peke (Regeneration: Ending the Climate Crisis in One Generation). Fikiria mifano fulani:
Mimea ya kidogo-kidogo yenye kuitwa phytoplancton inakokotaka na kuchunga diokside ya karbone, yenye ni gaze yenye kujulikana kuwa hatari mu dunia yote. Phytoplancton ayo peke inachungaka karibu kiasi ileile ya diokside ya karbone sawa ile yenye inachungiwaka na miti, majani, na mimea ingine yote ya mu dunia kama inatiwa pamoya.
Mikrobe inakulaka mwili, miiba, ao mifupa ya samaki zenye zilishakufa zenye zinaweza kuchafula bahari. Kisha, ile mikrobe nayo ni chakula ya viumbe vingine vyenye kuwa mu maji. Ile mupango inafanya bahari isiharibike na isichafuke. (Kulingana na Smithsonian Institution Ocean Portal)
Viumbe vingi vya mu bahari vinatumia uwezo wao wa kusaga chakula juu ya kubadilisha maji ya bahari yenye kuwa na acide yenye inafanya mubaya matumbawe, samaki-gamba, na viumbe vingine ili kuigeuza kuwa maji ya muzuri.
Mambo Yenye Iko Nafanyika
Kama tunatumia sac na chupa zenye haziko za plastike zenye tunaweza kutumia tena, ile inaweza kufanya plastike za mingi zisiende mu bahari na kuiharibisha
Kama uchafu hauingie mu bahari, hakutakuwa lazima ya kuisafisha. Njo maana, wanasanyansi wanatia moyo watu kutumia sac, vyombo mbalimbali, na boîte, vyenye tunaweza kutumia mara mingi kuliko kutumia vitu vyenye kufanywa na plastike vyenye tunatumia tu mara moya na kisha tunatupa.
Lakini kuko mambo ingine yenye inaomba kufanya. Hivi karibuni mu mwaka moya, tengenezo fulani yenye inatumika juu ya kulinda hali ya hewa, ilikusanya kilo 9 200 000 ya uchafu yenye bahari ilitupa pembeni mu inchi 112. Lakini, ile ilikuwa hesabu ya kidogo sana tena sana ya uchafu yenye inaingiaka kila mwaka mu bahari.
Wanadamu wako nachoma sana vitu mbalimbali sawa vile mafuta, pétrole, makala (charbon), na vitu vingine. Ile inafanya viumbe vyenye kuwa mu bahari vishindwe kufanya bahari iendelee kuwa safi sawa vile waliumbwa kufanya. (Ripoti ya National Geographic)
Sababu Zenye Kutupatia Tumaini—Mambo Yenye Biblia Inasema
“Dunia imejaa vitu vyenye umefanya. Kuko bahari, kubwa sana na pana, inajaa viumbe vyenye uzima vyenye havina hesabu, vidogo na vikubwa.”—Zaburi 104:24, 25.
Muumbaji wetu aliumba bahari na uwezo wa kujisafisha. Waza kidogo: Kama anajua mambo mingi sana kuhusu bahari na viumbe vyenye kuwa mu bahari, hauone kama anaweza kutengeneza mambo yote yenye wanadamu wamefanya juu ya kuharibisha bahari? Ona habari “Mungu Anaahidi Kama Dunia Itaokoka Kabisa,” ku ukurasa wa 15.