Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g23 na. 1 uku. 15
  • Mungu Anaahidi Kama Dunia Itaokoka Kabisa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mungu Anaahidi Kama Dunia Itaokoka Kabisa
  • Amuka!—2023
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Habari Zenye Kuwa mu Hii Gazeti
    Amuka!—2023
  • Watu Wataharibisha Dunia Kabisa-Kabisa?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Dunia Itaharibiwa?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Utangulizi
    Amuka!—2023
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2023
g23 na. 1 uku. 15
Milima na mapori inazunguka mutoni.

Oleh_Slobodeniuk/E+ via Getty Images

Mungu Anaahidi Kama Dunia Itaokoka Kabisa

“Dunia haiwezi kuharibika tu hivi-hivi sawa vile tunawaza.”

Ile njo jambo yenye kikundi ya watafiti wa mu dunia wenye kuhangaikia mambo ya hali ya hewa walifikia kusema. Ikiwa unaamini kama kuko Muumbaji mwenye anahangaikia wanadamu, jambo yenye wale watafiti walifikia kusema inaweza kukukumbusha mambo mingi yenye kuonyesha kama Mungu aliumba dunia na uwezo wa kujitunza ayo peke.

Juu wanadamu walishaharibisha sana dunia, haiwezi kujirudisha mu hali yenye ilikuwa zamani. Nini njo inatuhakikishia kama Mungu atarudisha dunia mu hali ya muzuri?

Ona hii maandiko yenye kuwa mu kisanduku yenye kuonyesha kama dunia itaokoka na itakuwa tena mu hali ya muzuri zaidi.

  • Mungu njo aliumba dunia. “Katika mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia.”—Mwanzo 1:1

  • Mungu njo mwenye dunia. “Dunia na vyote vyenye kuwa ndani yake ni vya Yehovaa.”—Zaburi 24:1

  • Mungu aliumba dunia juu iendelee kuwa. “Ameweka dunia imara juu ya misingi yake; Haitahamishwa kutoka mahali pake milele na milele.”—Zaburi 104:5

  • Mungu anaahidi kama maisha itaendelea kuwa ku dunia milele. “Mungu wa kweli, Mwenye alifanya dunia, . . . hakuiumba tu bila sababu, lakini aliifanya ili ikaliwe na watu.”—Isaya 45:18

  • Mungu anaahidi kama wanadamu wataishi milele ku dunia. “Wenye haki watariti dunia, na wataishi milele juu yake.”—Zaburi 37:29

Mungu aliumba dunia juu wanadamu wafurahie maisha bila kuharibisha dunia. Biblia ilitabiri kama kwa wakati wenye kufaa Yehova Mungu ataharibu wanadamu wenye pupa wenye kuharibu dunia.—Ufunuo 11:18

Biblia inaahidi kama kisha, Mungu atageuza dunia ikuwe paradiso ya muzuri na yenye kuwa safi. Na tena, atafungula mukono wake juu ya “kutimiza tamaa ya kila kitu chenye uzima.”—Zaburi 145:16

a Yehova njo jina ya pekee ya Mungu.—Zaburi 83:18.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine