Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • rq somo 3 uku. 6-7
  • Yesu Kristo Ni Nani?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yesu Kristo Ni Nani?
  • Mungu Anataka Nini Kwetu?
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Yesu Kristo Ni Nani?
    Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
  • Yesu Kristo Ni Nani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Sababu Gani Yesu Aliteseka na Kufa?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Sababu Gani Yesu Alikufa?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
Ona Habari Zaidi
Mungu Anataka Nini Kwetu?
rq somo 3 uku. 6-7

Somo 3

Yesu Kristo Ni Nani?

Kwa nini Yesu anaitwa Mwana “muzaliwa wa kwanza” wa Mungu? (1)

Kwa nini yeye anaitwa “Neno”? (1)

Kwa nini Yesu alikuja duniani kama binadamu? (2-4)

Kwa nini yeye alifanya miujiza? (5)

Yesu atafanya nini katika wakati ujao ulio karibu? (6)

1. Yesu aliishi mbinguni akiwa mutu wa kiroho kabla ya yeye kuja duniani. Yeye alikuwa kiumbe cha kwanza cha Mungu, na ndiyo sababu anaitwa “Mwana muzaliwa wa kwanza” wa Mungu. (Wakolosayi 1:15; Ufunuo 3:14) Yesu ndiye Mwana pekee ambaye Mungu aliumba yeye mwenyewe. Yehova alimutumia Yesu aliyeishi kabla ya kuwa binadamu, kama “fundi mufanya-kazi” wake katika kuumba vitu vingine vyote mbinguni na duniani. (Mezali 8:​22-31; Wakolosayi 1:​16, 17) Pia Mungu alimutumia kama musemaji Wake mukuu. Hiyo ndiyo sababu Yesu anaitwa “Neno.”​—⁠Yoane 1:​1-3; Ufunuo 19:⁠13.

2. Mungu alituma mwana Wake duniani kwa kuhamisha uhai wake na kuutia katika tumbo la uzazi la Maria. Hivyo Yesu hakuwa na baba wa kibinadamu. Hiyo ndiyo sababu hakuriti zambi yoyote au kutokukamilika. Kuna sababu tatu zilizomufanya Yehova amutume Yesu duniani: (1) Kutufundisha sisi ile kweli juu ya Mungu (Yoane 18:37), (2) kuchunga ushikaji-ukamilifu kabisa, akitoa hivyo kielelezo (kitu cha kuiga) kwetu kufuata (1 Petro 2:21), na (3) kutoa uhai wake ili kutufungua kutoka katika zambi na kifo. Kwa nini jambo hilo lilihitajiwa?​—⁠Matayo 20:⁠28.

3. Kwa kutotii amri ya Mungu, mwanaume wa kwanza, Adamu, alitenda kile Biblia inaita “zambi.” Hivyo Mungu alimuhukumia kifo. (Mwanzo 3:​17-19) Yeye hakuweza tena kufikia viwango vya Mungu, hivyo hakuwa tena mukamilifu. Polepole alianza kuzeeka na baadaye alikufa. Adamu aliambukiza zambi watoto wake wote. Hiyo ndiyo sababu sisi pia tunazeeka, tunapatwa na ugonjwa, na tunakufa. Binadamu wangeweza kuokolewa namna gani?​—⁠Waroma 3:23; 5:⁠12.

4. Yesu alikuwa binadamu mwenye kukamilika kama Adamu kabisa. Lakini, tofauti na Adamu ni kwamba Yesu alikuwa na utii mukamilifu kwa Mungu chini ya jaribu hata lililo kubwa zaidi. Yeye alikuwa hivyo na uwezekano wa kutoa uhai wake mukamilifu wa kibinadamu kama zabihu ili kulipia zambi ya Adamu. Biblia yalizungumuzia jambo hilo kuwa “ukombozi.” Wana wa Adamu walikuwa hivyo na uwezekano wa kufunguliwa kutoka hukumu ya kifo. Wale wote wanaotia imani yao katika Yesu wanaweza kuona zambi zao zikisamehewa na kupata uhai wa milele.​—⁠1 Timoteo 2:​5, 6; Yoane 3:16; Waroma 5:​18, 19.

5. Alipokuwa duniani Yesu aliponyesha wagonjwa, alilisha wenye njaa, na alituliza zoruba. Yeye aliinua hata wafu. Kwa nini alifanya miujiza? (1) Yeye alisikilia huruma watu waliokuwa wanateseka, na alipenda kuwasaidia. (2) Miujiza yake ilitoa uhakikisho kwamba yeye alikuwa Mwana wa Mungu. (3) Ilionyesha yale yeye atafanya kwa ajili ya binadamu watiifu wakati atatawala dunia akiwa Mufalme.​—⁠Matayo 14:14; Marko 2:​10-12; Yoane 5:​28, 29.

6. Yesu alikufa na akafufuliwa na Mungu akiwa kiumbe roho, na akarudi mbinguni. (1 Petro 3:18) Tangu hapo, Mungu amemufanya yeye kuwa Mufalme. Karibuni Yesu ataondoa kwenye dunia hii ubaya wote na mateso yote.​—⁠Zaburi 37:​9-11; Mezali 2:​21, 22.

[Picha katika ukurasa wa 7]

Huduma ya Yesu ilitia ndani kufundisha, kufanya miujiza, na hata kutolea uhai wake kwa ajili yetu

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine