Somo 12
Kuonyesha Heshima kwa Uhai na Damu
Namna gani tunapaswa kuuona uhai? (1) kuharibu mimba? (1)
Namna gani Wakristo wanaonyesha kwamba wanahangaikia usalama? (2)
Je! ni kosa kuua wanyama? (3)
Ni nini mojawapo wa mazoea ambayo yanaonyesha kukosa heshima kwa uhai? (4)
Nini iliyo sheria ya Mungu juu ya damu? (5)
Je! jambo hilo linatia ndani kutia damu mishipani? (6)
1. Yehova ndiye Chemchemi ya uhai. Uhai wa vitu vyote vyenye kuishi ni wa Mungu. (Zaburi 36:9) Uhai ni kitu kitakatifu kwa Mungu. Hata uhai wa mutoto asiyezaliwa bado anayepatikana ndani ya tumbo la mama yake ni wenye bei kwa Yehova. Kuua kwa kukania kitoto kama hicho kinachoendelea kukua ni kosa machoni pa Mungu.—Kutoka 21:22, 23; Zaburi 127:3.
2. Wakristo wa kweli wanahangaikia usalama. Wao wanahakikisha kwamba motokaa zao na nyumba zao si vyenye kuhatarisha. (Kumbukumbu la Torati 22:8) Watumishi wa Mungu hawatii maisha zao katika hatari isiyo ya lazima kwa sababu ya raha tu au ya kupenda kufanya jambo lenye kusisimua. Kwa hiyo wao hawashiriki michezo ya jeuri ambayo kwa makusudi mutu anaweza kumuumiza mutu mwengine. Wanaepuka viburudisho vinavyotia moyo kufanya mambo ya jeuri.—Zaburi 11:5; Yoane 13:35.
3. Uhai wa munyama pia ni kitu kitakatifu kwa Muumbaji. Mkristo anaweza kuua wanyama ili kupata chakula au nguo au kwa kujikinga na magonjwa na pia hatari. (Mwanzo 3:21; 9:3; Kutoka 21:28) Lakini ni kosa kutesa wanyama au kuwaua kwa sababu ya muchezo tu au kusikia raha.—Mezali 12:10.
4. Kuvuta tumbako, kutumia ugoro na pia dawa za kulevya ili mutu asikie raha tu si kwa Wakristo. Mazoea hayo ni mabaya kwa sababu (1) yanatufanya sisi kuwa watumwa wayo, (2) yanaumiza miili yetu, na (3) ni vitu visivyo safi. (Waroma 6:19; 12:1; 2 Wakorinto 7:1) Inaweza kuwa vigumu kuachana kabisa na tabia hizo. Lakini tunapaswa kufanya hivyo ili kumupendeza Yehova.
5. Damu pia ni kitu kitakatifu machoni pa Mungu. Mungu anasema kwamba nafsi, au uhai, ni katika damu. Kwa hiyo ni vibaya kula damu. Ni vibaya pia kula nyama ya munyama ambaye damu haikumwangwa vizuri. Ikiwa munyama amenyongwa au amekufa katika mutego, hapaswi kuliwa. Ikiwa amechomwa mukuki au kupigwa risasi, anapaswa kumwangwa damu haraka ikiwa ataliwa.—Mwanzo 9:3, 4; Walawi 17:13, 14; Matendo 15:28, 29.
6. Je! ni kosa kukubali kutiwa damu mishipani? Kumbuka, Yehova anataka sisi tujiepushe na damu. Hilo maana yake hatupaswi hata kidogo hata kwa njia gani kutia katika miili yetu damu ya watu wengine au hata damu yetu wenyewe ambayo imechungwa. (Matendo 21:25) Kwa hiyo Wakristo wa kweli hawatakubali kutiwa damu mishipani. Wao watakubali aina zingine za matunzo ya kiganga, kama vile kutiwa mishipani dawa zingine zisizokuwa na damu ndani yazo. Wanapenda kuishi, lakini hawatajaribu kuokoa uhai wao kwa kuvunja sheria za Mungu.—Matayo 16:25.
[Picha katika ukurasa wa 25]
Kumupendeza Mungu tunapaswa kuepuka kutiwa damu mishipani, tabia zisizo safi, na pia kujitia katika hatari zisizo za lazima