Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lv sura 2 uku. 14-24
  • Unaweza Kufanya Nini ili Zamiri Yako Iendelee Kuwa Safi?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Unaweza Kufanya Nini ili Zamiri Yako Iendelee Kuwa Safi?
  • Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ZAMIRI NI NINI, NA INATUMIKA NAMNA GANI?
  • NAMNA GANI TUNAWEZA KUIFUNDISHA ZAMIRI YETU?
  • NI VIZURI KUFIKIRIA PIA ZAMIRI ZA WENGINE
  • FAIDA YA KUWA NA ZAMIRI SAFI
  • Kuwa na Zamiri ya Muzuri Mbele ya Mungu
    Namna ya Kubakia Katika Upendo wa Mungu
  • Namna gani Ninaweza Kuzoeza Zamiri Yangu?
    Vijana Wanauliza
  • Zamiri Yako Ni Kiongozi Mwenye Kutumainika?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
lv sura 2 uku. 14-24
Busole na  karte

SURA YA 2

Unaweza Kufanya Nini ili Zamiri Yako Iendelee Kuwa Safi?

‘Muwe na zamiri njema [ao safi].ʼ—1 PETRO 3:16.

1, 2. Sababu gani ni jambo la lazima mutu awe na taa anapotembea katika giza, na taa ao boussole inaweza kufananishwa na zamiri katika njia gani?

WAZIA kwamba ni usiku na unalazimishwa kutembea katika giza. Utakuwa na lazima ya nini ili usijikwae na ili jambo mbaya lisikupate? Ni jambo la lazima uwe na taa ili kuangazia njia yako, sivyo?

2 Mutu akitembea katika giza bila taa, anaweza kujikwaa, kuanguka ao hawezi kuona hatari iliyo mbele yake. Taa inamuangazia mutu njia na inaweza kuokoa uzima. Katika njia fulani, zamiri inaweza kufananishwa na taa ao chombo kinachoitwa boussole. Zamiri ni zawadi ya bei ambayo Yehova ametupatia. (Yakobo 1:17) Bila zamiri, tungepotea kabisa. Zamiri ikitumiwa vizuri inaweza kumusaidia mutu kuona njia vizuri katika maisha yake na kuifuata. Kwa hiyo, acha tuone zamiri ni nini na inatumika namna gani. Kisha tutazungumuzia mambo haya matatu: (1) Namna gani tunaweza kufundisha zamiri yetu? (2) Sababu gani ni vizuri kufikiria pia zamiri za wengine? (3) Kuna faida gani ya kuwa na zamiri safi?

ZAMIRI NI NINI, NA INATUMIKA NAMNA GANI?

3. Neno la kigiriki linalotafsiriwa ‘zamiri’ linamaanisha nini, na neno hilo linaonyesha kama wanadamu wana uwezo gani wa pekee?

3 Katika Biblia, neno la Kigiriki linalotafsiriwa ‘zamiri’ linamaanisha “kujijua mwenyewe.” Hapa duniani, ni wanadamu tu ndio Mungu amepatia uwezo wa kujijua. Tuseme, ni kama vile mutu ana uwezo wa kujiona, anaona namna alivyo na pia anaona ikiwa ana mwenendo unaofaa ao hapana. Zamiri inatumika kama shahidi wetu wa ndani, ao muamuzi, na inaweza kuchunguza matendo yetu, mawazo yetu, na mambo tunayopenda. Inaweza kutuongoza tuchukue uamuzi muzuri ao kutuonya ili tusichukue uamuzi mubaya. Ikiwa tulichukua uamuzi muzuri, zamiri yetu inaweza kutufariji, na ikiwa tulichukua uamuzi mubaya inaweza kutusumbua sana ao kutuhukumu.

4, 5. (a) Namna gani tunajua kama Adamu na Eva walikuwa na zamiri, na walipata matokeo gani kwa kuvunja sheria ya Mungu? (b) Ni mifano gani inayoonyesha kama wanadamu fulani wa zamani walitumia vizuri zamiri yao?

4 Mwanaume na mwanamuke wa kwanza waliumbwa na zamiri. Tunajua kama Adamu na Eva walikuwa na zamiri, kwa sababu kisha tu kufanya zambi waliona haya. (Mwanzo 3:7, 8) Lakini, jambo la huzuni ni kwamba hata ikiwa zamiri yao iliwasumbua, haingeweza tena kuwasaidia wakati huo. Walikuwa wamevunja sheria ya Mungu kimakusudi. Kwa kupuuza zamiri yao na kuvunja sheria ya Mungu, walichagua wenyewe kuwa waasi na wapinzani wa Yehova Mungu. Walikuwa watu wenye kukamilika, na kwa hiyo, walijua vizuri kama jambo wanalofanya ni mbaya na hawangeweza tena kumurudilia Mungu.

5 Adamu na Eva hawakusikiliza zamiri yao, lakini kumekuwa na wanadamu wengi wasio wakamilifu ambao wamesikiliza zamiri yao. Tuchukue mufano wa mwanaume mwaminifu Ayubu. Yeye aliweza kusema hivi: ‘Nimeishikilia haki yangu, nami sitaiachilia; moyo wangu hautanizihaki kwa ajili ya yoyote ya siku zangu.’a (Ayubu 27:6) Ayubu alisikiliza kabisa zamiri yake; aliiacha iongoze matendo na maamuzi yake. Kwa hiyo, alifurahia kabisa hali yake na aliweza kusema kama zamiri yake haikumuzihaki ao kumusumbua; hakufanya jambo lolote ambalo lingemufanya aone haya na kujilaumu. Sasa ona tofauti kati ya Ayubu na Daudi. Wakati Daudi alifanya jambo fulani lililoonyesha kama alimukosea heshima Sauli mufalme mutiwa-mafuta wa Yehova, ‘baadaye moyo wa Daudi ukaendelea kumuchoma.’ (1 Samweli 24:5) Kwa sababu zamiri ya Daudi ilimusumbua, bila shaka ilimusaidia, kwa kuwa wakati ujao hangeweza tena kumukosea heshima mufalme.

6. Ni nini inayoonyesha kama Mungu amewapatia wanadamu wote zawadi hiyo ya zamiri?

6 Ni watumishi wa Yehova tu ndio wana zamiri? Ili kujibu ulizo hilo, tuchunguze maneno mutume Paulo aliandika kwa uongozi wa roho takatifu: ‘Wakati watu wa mataifa wasio na sheria wanapofanya kwa asili mambo ya sheria, watu hawa, ijapokuwa hawana sheria, wao ni sheria kwao wenyewe. Wao ndio wanaoonyesha kuwa yaliyomo katika sheria yameandikwa ndani ya mioyo yao, huku zamiri yao ikiwatolea ushahidi na, katikati ya fikira zao wenyewe, wanashitakiwa ao hata kutetewa.’ (Waroma 2:14, 15) Wakati fulani, hata wale wasiojua hata kidogo sheria za Yehova wanaweza kusukumwa na shahidi wao wa ndani, ni kusema, zamiri yao, ili watende kupatana na kanuni za Mungu.

7. Sababu gani wakati fulani zamiri inaweza kutumika vibaya?

7 Hata hivyo, wakati fulani zamiri inaweza kutumika vibaya. Sababu gani? Kumbuka tena mufano wa taa tuliozungumuzia mwanzoni. Petrole ikiisha ndani ya taa, taa hiyo haiwezi tena kutoa mwangaza. Jambo kama hilo linaweza kufikia zamiri yetu; ikiwa hatujifunze Neno la Mungu, hatuwezi kutofautisha mema na mabaya. Vilevile, ikiwa moyo wetu unajaa tamaa mbaya, zamiri yetu inaweza kuharibika na kwa hiyo haiwezi tena kutuongoza vizuri. Na tukifuata zamiri yetu bila kuchunguza Neno la Mungu, inaweza kuwa vigumu kwetu kutofautisha mema na mabaya katika mambo mengi ya lazima. Kwa kweli, ili zamiri yetu itumike vizuri, tunapaswa kufuata uongozi wa roho takatifu ya Yehova. Mutume Paulo aliandika hivi: ‘Zamiri yangu inanitolea ushahidi katika roho takatifu.’ (Waroma 9:1) Basi, tunaweza kufanya nini ili zamiri yetu ifuate uongozi wa roho takatifu ya Yehova? Inaomba tuifundishe.

NAMNA GANI TUNAWEZA KUIFUNDISHA ZAMIRI YETU?

8. (a) Namna gani tamaa za moyo zinaweza kuharibisha zamiri ya mutu, na tunapaswa kwanza kujiuliza nini mbele ya kuamua jambo fulani? (b) Sababu gani Mukristo hapaswe kufikiri kama uamuzi aliochukua si mubaya kwa sababu tu zamiri yake haimusumbue? (Soma maelezo yaliyo chini.)

8 Namna gani unaweza kutumia zamiri yako ili kuchukua uamuzi? Inaonekana kama watu wengine wanafuata tu mawazo ya moyo wao ao jinsi wanavyojisikia, na kisha wanaamua kile watafanya. Kisha wanaweza kusema, “Kulingana na zamiri yangu sione ubaya wowote.” Tamaa za moyo wa mutu zinaweza kuwa na nguvu sana hata kufikia kuharibisha zamiri yake. Biblia inasema hivi: “Moyo ni wenye hila kuliko kitu kingine chochote nao ni hatari. Ni nani anayeweza kuujua?” (Yeremia 17:9) Kwa hiyo, hatupaswe kufuata haraka-haraka tamaa ya moyo wetu. Tunapaswa kwanza kujiuliza ikiwa yale moyo wetu unatamani yatamupendeza Yehova ao hapana.b

9. Kuogopa Mungu kunamaanisha nini, na namna gani woga huo unaweza kutusaidia tuwe na zamiri safi tunapochukua maamuzi?

9 Ikiwa tunachukua uamuzi kwa sababu tunaongozwa kabisa na zamiri iliyofundishwa, hilo litaonyesha kama sisi ni watu wenye kumuogopa Mungu na hatufuate tamaa zetu za kichoyo. Ili kuelewa jambo hilo, tuchukue mufano wa liwali (ao guvernere) mwaminifu Nehemia. Kwa sababu alikuwa guvernere, alikuwa na haki ya kuomba watu wa Yerusalemu watoe kodi na michango fulani. Lakini hakufanya hivyo. Sababu gani? Hakutaka kuwatesa watu wa Mungu na hivyo kumuchukiza Yehova. Alisema hivi: ‘Mimi sikufanya hivyo kwa sababu ya kumuogopa Mungu.’ (Nehemia 5:15) Ni jambo la lazima kumuogopa Mungu bila unafiki, ni kusema, kuogopa kwa moyo wote kufanya jambo lolote linaloweza kumuchukiza Baba yetu wa mbinguni. Heshima na woga kama huo vitatusukuma kutafuta uongozi wa Neno la Mungu kila wakati tunapotaka kuchukua maamuzi.

10, 11. Ni kanuni gani za Biblia tunazopaswa kufikiria katika jambo la kunywa pombe, na tunaweza kufanya nini ili kuonyesha kama tunapenda Mungu atuongoze ili tutumie kanuni hizo?

10 Kwa mufano, acha tuzungumuzie jambo la kunywa pombe. Tunapojifurahisha na marafiki, mara nyingi tunapaswa kuamua ikiwa tutakunywa pombe ao hapana. Kwanza, lazima tufundishe zamiri yetu. Ni kanuni gani za Biblia tunazopaswa kufikiria katika jambo hilo? Biblia haikataze kunywa pombe kwa kiasi. Divai inafanya Yehova asifiwe, kwa sababu ni yeye aliyetupatia zawadi hiyo. (Zaburi 104:14, 15) Hata hivyo, Biblia inakataza ulevi na karamu za kupindukia, ni kusema, watu wanaokunywa pombe sana na wanaofanya makelele kwa sababu ya ulevi. (Luka 21:34; Waroma 13:13) Tena, Biblia inataja ulevi kati ya zambi nzito, kama vile uasherati na uzinzi.c—1 Wakorintho 6:9, 10.

11 Mukristo anafundisha zamiri yake kwa kutumia kanuni kama hizo katika maisha yake. Hivyo, zamiri yake inakuwa tayari kumuonya juu ya mema na mabaya. Kwa hiyo, anapoamua ikiwa atakunywa pombe ao hapana kwenye karamu fulani, atajiuliza maulizo haya: ‘Ni karamu gani? Je, inaweza kuvuka mipaka na kugeuka kuwa karamu ya kupindukia? Mimi mwenyewe ninapenda pombe sana? Mimi ni mutumwa wa pombe, na ninaitumia ili kusahau magumu yangu ao kuondoa haya? Je, ninaweza kabisa kujizuiza ili nikunywe kwa kiasi?’ Mutu anapofikiria maulizo hayo na kanuni za Biblia juu ya jambo hilo, ni vizuri amuombe Yehova ili amuongoze. (Zaburi 139:23, 24) Kwa kufanya hivyo, tutaonyesha kama tunapenda Yehova atuongoze kupitia roho yake takatifu, pia tunaifundisha zamiri yetu ipatane na kanuni zake. Lakini kuna jambo lingine ambalo tunapaswa kufikiria sana wakati tunachukua maamuzi.

NI VIZURI KUFIKIRIA PIA ZAMIRI ZA WENGINE

 Mwanaume mumoja anaamua ikiwa atakunywa ao hapana kilauri cha divai kwenye nafasi ya kujifurahisha

Zamiri yenye kuzoezwa na Biblia inaweza kukusaidia kuamua ikiwa utakunywa pombe ao hapana

12, 13. Sababu gani zamiri za Wakristo zinatofautiana, na namna gani tunapaswa kuona tofauti hizo?

12 Wakati fulani labda unaweza kushangaa kuona zamiri ya Mukristo fulani inatofautiana na zamiri ya Mukristo mwengine. Mukristo fulani anaweza kuchukizwa na jambo ao tabia fulani; lakini mwengine anaweza kupendezwa na jambo hilo na kuona kama hakuna sababu ya kulaumu jambo hilo. Tuchukue mufano wa kunywa pombe; ndugu fulani anaweza kuona kuwa si vibaya kunywa pombe pamoja na marafiki wanapojifurahisha mangaribi fulani; lakini ndugu mwengine anaweza kukwazika na jambo hilo. Sababu gani mawazo yao yanatofautiana, na tunaweza kuliona jambo hilo namna gani?

13 Watu wanatofautiana kwa sababu ya mambo mbalimbali. Hali ambamo watu wamekomalia zinaweza kutofautiana sana. Kwa mufano, wengine wanajua kama walipiganisha uzaifu fulani zamani na labda wanaogopa kama wanaweza tena kuangukia katika uzaifu huo. (1 Wafalme 8:38, 39) Ikiwa walikuwa na uzaifu juu ya pombe, wanaweza kuwa macho sana juu ya pombe. Mutu kama huyo akikutembelea, labda zamiri yake inaweza kumukataza kunywa pombe. Utakasirika? Utamukaza tu mupaka akunywe? Hapana. Iwe unajua ao haujue sababu gani anakataa kunywa pombe, na labda hataki kukuelezea sababu hizo wakati huo, upendo utakuzuia kumukaza.

14, 15. Ni katika jambo gani zamiri za Wakristo fulani zilitofautiana, na mutume Paulo alitoa shauri gani juu ya jambo hilo?

14 Mutume Paulo aliona pia kama mara nyingi zamiri za Wakristo wa wakati wake zilitofautiana. Wakati huo, Wakristo fulani walisumbuliwa na zamiri zao kwa sababu ya vyakula fulani vilivyokuwa vimetolewa zabihu kwa sanamu. (1 Wakorintho 10:25) Lakini zamiri ya mutume Paulo haikumukataza kula vyakula hivyo; vyakula ambavyo kisha kutolewa zabihu kwa sanamu viliuzishwa katika soko. Yeye aliona hizo sanamu kuwa si kitu; kwa sababu ni Yehova ndiye aliyeumba chakula, kwa hiyo, chakula hicho ni mali yake na si chakula cha sanamu. Hata hivyo, Paulo alielewa kama ndugu wengine hawakuwa na mawazo kama yake. Inawezekana ndugu wengine walikuwa wakiabudu sanamu hizo mbele ya kuwa Wakristo. Kwa ndugu hao, kila kitu kilichotumiwa katika ibada hiyo ya sanamu kilikuwa chenye kuchukiza. Mutume Paulo alifanya nini ili kumaliza tatizo hilo?

15 Mutume Paulo alisema hivi: ‘Ingawa hivyo, sisi tulio na nguvu tunapaswa kuchukua uzaifu wa wale wasio na nguvu, na tusiwe tukijipendeza wenyewe. Kwa maana hata Kristo hakujipendeza mwenyewe.’ (Waroma 15:1, 3) Kwa hiyo, alionyesha kama tunapaswa kutia faida za ndugu zetu mbele ya faida zetu, kama Kristo alivyofanya. Katika mazungumuzo mengine juu ya jambo hilo, Paulo alisema kama ingekuwa vizuri asikule nyama ikiwa jambo hilo litakwaza kondoo ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake.​—1 Wakorintho 8:13; 10:23, 24, 31-33.

16. Sababu gani ndugu walio na zamiri inayowakataza kufanya jambo fulani hawapaswe kuwahukumu ndugu wengine ambao wana zamiri tofauti na yao?

16 Kwa upande mwengine, wale walio na zamiri inayowakataza kufanya jambo fulani hawapaswe kuwahukumu ndugu wengine, wala kuwakaza waone mambo hayo ya zamiri kama wao. (Waroma 14:10) Zamiri ya mutu inapaswa kufanya kazi ya kumuhukumu yeye mwenyewe, wala si kuwahukumu wengine. Kumbuka maneno haya ya Yesu: ‘Acheni kuhukumu ili musihukumiwe.’ (Mathayo 7:1) Sisi wote katika kutaniko tunapaswa kuepuka mabishano juu ya mambo ya zamiri. Kuliko kubishana tujikaze kuwa na upendo na umoja, tujengane na tusibomoane.—Waroma 14:19.

FAIDA YA KUWA NA ZAMIRI SAFI

Mwanamuke anatembea katika shamba lenye kuwa na majani wakati hali iko muzuri

Zamiri yenye kuwa safi inaweza kutuongoza katika safari ya maisha, kutuletea furaha na amani ya moyoni

17. Zamiri za watu wengi zimekuwa namna gani leo?

17 Mutume Petro aliandika: ‘Muwe na zamiri njema [ao safi].ʼ (1 Petro 3:16) Ndugu ao dada aliye na zamiri safi machoni pa Yehova Mungu anabarikiwa kabisa. Watu wengi hawana zamiri kama hiyo leo. Mutume Paulo alisema kama kuna watu ‘waliotiwa alama katika zamiri zao kama kwa chuma cha kutilia alama.’ (1 Timotheo 4:2) Chuma cha kutilia alama kinaunguza mwili na kuutia kovu, na kovu hilo linamufanya mutu asisikie maumivu nafasi hiyo. Zamiri za watu wengi ziko hivyo, ni kama vile zimekwisha kufa ao zina makovu mengi na hazisikie lolote. Zamiri zao zimeacha kuwaonya na kuwalaumu, hawana tena haya wanapofanya mambo mabaya, mawazo yao hayawasumbue tena wanapofanya makosa. Leo, kufanya mabaya kunawafurahisha watu wengi na hawapendi zamiri zao ziwasumbue tena.

18, 19. (a) Kujisikia kama umefanya vibaya ao kujisumbua kunaweza kuwa na faida gani? (b) Tunaweza kufanya nini ikiwa zamiri inaendelea kutusumbua kwa sababu ya zambi tuliyofanya zamani na ambayo tumekwisha kutubu?

18 Kwa kweli, mutu kujisikia kama alifanya kosa inaweza kuwa njia ambayo zamiri inatumia ili kumujulisha kama amefanya vibaya. Kujisikia hivyo kunaweza kumusukuma mutu aliyefanya zambi atubu, na Mungu anaweza kumusamehe mutu kama huyo hata ikiwa alifanya zambi nzito sana. Kwa mufano, Mufalme Daudi alijisikia vibaya ao kujisumbua kwa sababu ya kosa kubwa alilofanya, lakini Mungu alimusamehe kwa sababu alitubu kwelikweli. Kwa kuwa alichukia zambi aliyofanya na akaazimia kutii sheria za Yehova kuanzia wakati huo, jambo hilo lilimusaidia aone mara moja kama Yehova ‘ni mwema na yuko tayari kusamehe.’ (Zaburi 51:1-19; 86:5) Lakini, mutu atafanya nini ikiwa zamiri inaendelea kumusumbua sana ijapokuwa ametubu na kusamehewa?

19 Wakati fulani, zamiri inaweza kuendelea kumuchoma kupita kiasi mutu aliyefanya zambi, kumufanya ajisikie kama zambi hiyo iko tu hata ikiwa amekwisha kusamehewa. Katika hali kama hizo, ni lazima mutu ahakikishie moyo wake kama Yehova ni mukubwa kabisa kuliko mawazo ya moyo wa mwanadamu. Kwa kawaida, sisi tunawatia wengine moyo waamini kama Mungu anawapenda na iko tayari kuwasamehe; sisi pia tunapaswa kuamini hivyo. (1 Yohana 3:19, 20) Tofauti na zamiri ya inayoendelea kuchoma, zamiri iliyo safi inamufanya mutu awe na amani ya moyo, mwenye kutulia, na mwenye furaha sana; mambo ambayo watu wa dunia hii wanakosa. Ndugu wengi ambao hapo zamani walikuwa wanafanya zambi nzito wamepata amani hiyo ya ajabu, na leo wanamutumikia Yehova Mungu na zamiri safi.—1 Wakorintho 6:11.

20, 21. (a) Kitabu hiki kiliandikwa kwa kusudi gani? (b) Wakristo wana uhuru gani, na wanapaswa kutumia uhuru huo namna gani?

20 Kitabu hiki kimeandikwa ili kukusaidia upate furaha, na kuendelea kuwa na zamiri safi katika siku hizi za mwisho za ulimwengu huu muovu wa Shetani. Ni kweli kwamba kitabu hiki hakiwezi kuzungumuzia sheria na kanuni zote za Biblia ambazo unapaswa kufikiria na kutumia katika hali zinazotokea kila siku katika maisha yako. Tena, haupaswe kutazamia kama Biblia itakupatia sheria kuhusu kila jambo linalotegemea zamiri yako. Kusudi la kitabu hiki ni kukusaidia ufundishe zamiri yako na kuifanya iwe yenye kutenda; unaweza kufanya hivyo kwa kujifunza na kutumia neno la Mungu kila siku maishani mwako. Sheria ya Musa inatofautiana na “sheria ya Kristo.” Sheria ya Kristo inatuomba sisi Wakristo tutumie zaidi zamiri na kanuni katika maisha yetu kuliko kutumia sheria zilizoandikwa. (Wagalatia 6:2) Jambo hilo linaonyesha kama Yehova anawapatia Wakristo uhuru mwingi. Hata hivyo, Neno lake linatukumbusha kama hatupaswe kutumikisha uhuru huo kama “kifuniko cha ubaya.” (1 Petro 2:16) Lakini, uhuru huo unatutolea nafasi nzuri ya kumuonyesha Yehova kama tunamupenda.

21 Ukisali na kufikiria sana namna ya kutumia vizuri zaidi kanuni za Biblia katika maisha yako na kutenda kupatana na uamuzi wako, utaendelea kufanya jambo la lazima ambalo ulianza kufanya wakati ulianza kumujua Yehova. ‘Nguvu zako za ufahamu’ zitazoezwa kadiri ‘unavyozitumia.’ (Waebrania 5:14) Zamiri yako iliyofundishwa kupitia Biblia itakuletea faida kila siku. Kama taa inayoangazia mutu njia, zamiri yako itakusaidia kuchukua maamuzi yatakayomupendeza Baba yako wa mbinguni. Hilo litakusaidia kabisa ubaki katika upendo wa Mungu.

a Neno ‘zamiri’ halipatikane katika maandiko ya Kiebrania. Lakini, mufano wa Ayubu unaonyesha wazi kama watu wengi walitumia zamiri. Mara nyingi neno “moyo” linaonyesha mutu wa ndani. Linapotumiwa katika maana hiyo linamaanisha zamiri yake. Katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, neno la Kigiriki linalotafsiriwa ‘zamiri’ linapatikana humo mara 30 hivi.

b Biblia inaonyesha kama haitoshe tu kufikiri kama uamuzi ambao ulichukua si mubaya kwa sababu tu zamiri yako haikusumbue. Kwa mufano, mutume Paulo alisema hivi: ‘Sifahamu kitu chochote zidi yangu mwenyewe. Lakini kwa hilo sionyeshwe kuwa mwadilifu, bali yeye anayenichunguza ni Yehova.’ (1 Wakorintho 4:4) Watu fulani wanaweza kuwatesa Wakristo, kama vile Paulo alivyofanya hapo zamani, lakini zamiri yao haiwasumbue kwa sababu wanawaza kama Mungu anakubali matendo yao. Ni jambo la lazima kwamba zamiri yetu isitusumbue, lakini zamiri hiyo inapaswa pia kuwa safi machoni pa Mungu.—Matendo 23:1; 2 Timotheo 1:3.

c Ni vizuri kujua kama wanganga wengi wanasema haiwezekane kwa watu wanaozoea kulewa kunywa kwa kiasi; kwa watu hao, kunywa kwa “kiasi” kunamaanisha kutokunywa hata kidogo.

UNAWAZA NAMNA GANI?

  • Namna gani kujua kama Yehova anatuona kila wakati kunapaswa kuchochea zamiri yetu?—Waebrania 4:13.

  • Namna gani zamiri ya Yosefu ilimusaidia kushinda vishawishi?—Mwanzo 39:1, 2, 7-12.

  • Sababu gani ni lazima kuwa na zamiri safi ili kumukaribia Yehova?—Waebrania 10:22.

  • Sababu gani ni vizuri kufikiria pia zamiri za watu wengine wasio Mashahidi?—2 Wakorintho 4:1, 2.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine