Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lv sura 12 uku. 133-143
  • Sema Maneno Mazuri ili Kujenga

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Sema Maneno Mazuri ili Kujenga
  • Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • SABABU GANI TUNAPASWA KUFANYA ANGALISHO NA MANENO YETU
  • MANENO YANAYOBOMOA
  • MANENO MAZURI ILI KUJENGA
  • Sema Maneno ya ‘Muzuri ili Kujenga’
    Namna ya Kubakia Katika Upendo wa Mungu
  • Uko “Mufano ... Katika Kusema”?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Useme Maneno Yenye Inamufurahisha Yehova
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Jinsi ya Kuepuka Maneno Yenye Kuumiza
    Amuka!—2013
Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
lv sura 12 uku. 133-143
Majani ya muti yenye kuwa na maji

SURA YA 12

Sema Maneno Mazuri ili Kujenga

‘Neno lililooza lisitoke katika kinywa chenu, bali neno lolote ambalo ni njema ili kujenga’​—WAEFESO 4:29.

1-3. (a) Ni zawadi gani Yehova ametupatia, na namna gani tunaweza kuitumia vibaya? (b) Ili tubaki katika upendo wa Mungu, namna gani tunapaswa kutumia zawadi hiyo ya kusema?

UTAJISIKIA namna gani ikiwa unaona rafiki yako anatumia vibaya na kwa makusudi zawadi uliyomutolea? Kwa mufano, ulimupatia motokari, na kisha unapata habari kama anaitembeza vibaya, na amewagonga watu. Je, utafurahi?

2 Uwezo tulio nao wa kusema maneno yenye kueleweka ni zawadi ambayo Yehova ametupatia. Yeye ni Mutoaji wa ‘kila zawadi nzuri na kila tuzo kamilifu.’ (Yakobo 1:17) Zawadi hiyo inatutofautisha sana na wanyama; inatusaidia kuwajulisha wengine mawazo yetu na pia namna tunavyojisikia. Hata hivyo, zawadi ya kusema inaweza kutumiwa vibaya kama motokari tuliozungumuzia. Basi, wakati tunatumia maneno yetu vibaya kwa kuwaumiza wengine, hilo halimufurahishe Yehova hata kidogo!

3 Ili tubaki katika upendo wa Mungu, tunapaswa kutumia zawadi ya uwezo wa kusema kama ilivyokusudiwa na Mungu. Yehova anatujulisha waziwazi ni maneno gani yanayomupendeza na yale yasiyomupendeza. Neno lake linasema hivi: ‘Neno lililooza lisitoke katika kinywa chenu, bali neno lolote ambalo ni njema [ao nzuri] ili kujenga kulingana na uhitaji, ili liwape wasikiaji lile linalofaa.’ (Waefeso 4:29) Sasa, sababu gani tunapaswa kufanya angalisho na maneno yetu? Ni maneno gani tunapaswa kuepuka kutumia, na namna gani tunaweza kutumia maneno mazuri ili “kujenga?”

SABABU GANI TUNAPASWA KUFANYA ANGALISHO NA MANENO YETU

4, 5. Namna gani maandiko fulani ya Methali yanaonyesha kama maneno yana nguvu?

4 Sababu ya kwanza ni hii: maneno yana nguvu. Andiko la Methali 15:4 linasema hivi: ‘Utulivu wa ulimi ni muti wa uzima, lakini upotovu wake unamaanisha kuvunjika katika roho.’a Muti wenye kukauka ukipata maji unakuwa na uzima tena, vilevile, maneno yanayosemwa na ulimi wenye kutulia yanaweza kutuliza roho ya wale wanaoyasikia. Lakini, maneno yenye kuumiza yanayosemwa na ulimi wenye kupotoka yanaweza kuwavunja wengine moyo. Kwa kweli, maneno tunayosema yana uwezo wa kuumiza ao kuponyesha.—Methali 18:21.

5 Ili kuonyesha tena kama maneno yana nguvu, Methali nyingine inasema hivi: ‘Kuna mutu anayesema bila kufikiri kama kwa upanga unaochoma.’ (Methali 12:18) Mutu anaposema haraka-haraka na bila kufikiri, anaweza kuumiza wengine moyoni na kuharibisha urafiki wake na wengine. Je, moyo wako umekwisha kuumizwa na maneno yaliyochoma kama upanga? Kwa upande mwengine, Methali hiyo inashauri pia moyo hivi: ‘Ulimi wa mwenye hekima unaponya.’ Maneno yenye kufikiriwa vizuri na mutu anayeonyesha hekima inayotoka kwa Mungu yanaweza kuponyesha moyo unaoumizwa na kurudisha urafiki ulioharibika. Je, umekwisha kujionea namna maneno mazuri yalivyo na nguvu ya kuponyesha? (Methali 16:24) Ikiwa tunaelewa kama maneno tunayosema yana nguvu, basi tutayatumia ili kuwaponyesha wengine, wala si kuwaumiza.

Maneno ya upole yanatuliza

6. Sababu gani hatuwezi kabisakabisa kuzuia ulimi wetu?

6 Hata ikiwa tunajikaza namna gani, hatuwezi kabisakabisa kuzuia ulimi wetu. Kwa hiyo, sababu ya pili inayotuchochea kufanya angalisho na maneno yetu ni hii: Zambi na kukosa kukamilika vinatufanya tutumie vibaya ulimi wetu. Maneno tunayosema yanatoka katika moyo, nao ‘muelekeo wa moyo wa mwanadamu ni mubaya.’ (Mwanzo 8:21; Luka 6:45) Kwa hiyo, kuzuia ulimi wetu ni vita kabisa. (Yakobo 3:2-4) Hata ikiwa hatuwezi kabisakabisa kuzuia ulimi wetu, tunaweza kufanya nguvu ya kuutumia katika njia inayofaa. Mutu anayeogelea katika mutoni akipanda upande maji yanatoka anapaswa kufanya nguvu sana; vilevile, tunapaswa kupiganisha kabisa muelekeo wa zambi unaotusukuma kutumia ulimi wetu vibaya.

7, 8. Namna gani maneno yetu yanaweza kufanya Yehova atukubali ao asitukubali?

7 Sababu ya tatu inayotuchochea kufanya angalisho na maneno yetu ni kwamba maneno yetu yatafanya tukubaliwe ao tusikubaliwe na Yehova. Namna tunavyotumia ulimi wetu inaweza kufanya urafiki wetu pamoja na wengine uwe muzuri ao mubaya. Ni hivyo pia juu ya urafiki wetu pamoja na Yehova. Andiko la Yakobo 1:26 linasema hivi: ‘Ikiwa mutu yeyote anajiona kuwa muabudu anayeshikilia vizuri namna ya ibada na bado haongoze [ao hazuie] ulimi wake, bali anaendelea kuundanganya moyo wake mwenyewe, namna ya ibada ya mutu huyo ni ya ubatili.’b Kama tulivyoona katika Sura ya 11, maneno yetu na ibada yetu vinatembea pamoja. Ikiwa hatuzuie ulimi wetu, ikiwa unatoa kila mara maneno yenye kuumiza, maneno yaliyo kama sumu, basi, mambo yote tunayofanya ili kumutumikia Mungu ni bure machoni pake. Tunapaswa kufikiria sana jambo hilo, sivyo?—Yakobo 3:8-10.

8 Ni wazi kama tuna sababu za lazima zinazotuchochea kufanya angalisho ili tusitumie vibaya zawadi ya kusema. Mbele ya kuzungumuzia maneno mazuri yanayoweza kujenga, acha kwanza tuzungumuzie namna fulani ya maneno ambayo Wakristo wa kweli wanapaswa kuepuka katika maisha yao.

MANENO YANAYOBOMOA

9, 10. (a) Leo, watu wanatumia maneno ya namna gani katika mazungumuzo yao ya kila siku? (b) Sababu gani tunapaswa kutupilia mbali maneno machafu? (Soma pia maelezo yaliyo chini.)

9 Maneno machafu. Leo, kila siku watu wanatumia sana matusi na maneno mengine machafu katika mazungumuzo yao. Watu wengi wanatumia maneno yasiyofaa ili kuvutia uangalifu wa wengine ao kwa sababu hawajue maneno ya kutumia. Mara nyingi watu wanaofanya mambo ya teatre wanatumia maneno yasiyo ya adabu na machafu ili kuchekesha watu. Lakini maneno machafu si jambo la muzaha. Kumekwisha kupita miaka karibu 2000, mutume Paulo alitolea Wakristo wa kutaniko la Kolosai shauri la kutupilia mbali “maneno machafu.” (Wakolosai 3:8) Mutume Paulo aliwaambia Wakristo wa kutaniko la Efeso kwamba “mizaha michafu” ni kati ya mambo ambayo hayapaswe ‘kutajwa hata kidogo katikati’ ya Wakristo wa kweli.—Waefeso 5:3, 4.

10 Maneno machafu yanamukasirisha Yehova. Yanakasirisha pia wale wanaomupenda. Basi, ni upendo wetu kwa Yehova ndio unatuchochea tuachane na maneno machafu. Mutume Paulo alipozungumuzia “matendo ya mwili” alitaja “uchafu;” neno hilo linaweza pia kumaanisha uchafu katika maneno. (Wagalatia 5:19-21) Hilo si jambo la muchezo. Ndugu ao dada anaweza kutengwa na kutaniko ikiwa baada ya kushauriwa mara kwa mara anakosa kutubu na anaendelea kutumia maneno machafu ya kukosea wengine adabu na mapotovu.c

11, 12. (a) Kuteta ni nini, na sababu gani kumuteta mutu ni vibaya? (b) Sababu gani watumishi wa Yehova wanapaswa kuepuka kusingizia wengine?

11 Kumuteta mutu ili kumuharibishia sifa, kumusingizia mutu. Kuteta ni kusema vibaya juu ya mutu fulani ao maisha yake. Je, kila kusema juu ya mutu ni vibaya? Hapana. Ikiwa tunazungumuza mambo mazuri juu ya mutu fulani, ao habari zinazoweza kutia moyo, si vibaya. Kwa mufano, tunaweza kuzungumuza juu ya mutu ambaye amebatizwa hivi karibuni ao mutu ambaye ana lazima ya kutiwa moyo. Wakati wa mitume, Wakristo walikuwa wanahangaikiana sana na walikuwa wanapashana habari juu ya waamini wenzao. (Waefeso 6:21, 22; Wakolosai 4:8, 9) Lakini, ikiwa hatuseme ukweli juu ya mutu fulani ao tunafunua mambo yake ya siri, hapo tunamuteta. Na zaidi tena, jambo hilo linaweza kugeuka kuwa kusingizia, na kusingizia ni vibaya kila mara. Kusingizia ni “kumusemea mutu fulani mambo ya uongo, na jambo hilo linaharibisha sifa ya mutu huyo.” Tuchukue mufano wa Mafarisayo, walikuwa wakimusemea Yesu mambo mabaya ya uongo, ili kumuharibishia sifa. (Mathayo 9:32-34; 12:22-24) Kila mara kusingizia kunatokeza ugomvi.—Methali 26:20.

12 Yehova anachukia sana watu wanaotumia zawadi ya kusema ili kuharibishia wengine sifa ao kuingiza migawanyiko. Anachukia wale wanaotokeza “ugomvi kati ya ndugu.” (Methali 6:16-19) Neno la Kigiriki linalotafsiriwa na “musingiziaji” ni diabolos, ambalo pia linatumiwa kuwa jina la cheo la Shetani. Yeye ni “Ibilisi,” ambaye anamusingizia Mungu mambo maovu. (Ufunuo 12:9, 10) Kwa kweli, tunapaswa kuepuka maneno ambayo yanaweza kutufanya tuwe kabisa kama Ibilisi. Katika kutaniko, tabia ya kusingizia wengine haikubaliwe, kwa sababu hilo linachochea kazi za mwili, kama vile “ugomvi” na “migawanyiko.” (Wagalatia 5:19-21) Kwa hiyo, mbele ya kusambaza habari unayosikia juu ya ndugu fulani, ujiulize: “Je, habari hiyo ni ya kweli? Je, ni vizuri kusambaza habari hiyo? Je, ni jambo la lazima kabisa ao inafaa kuwaelezea wengine habari hiyo?”​—1 Wathesalonike 4:11.

13, 14. (a) Mutu anaweza kujisikia namna gani anapotukanwa? (b) Matukano ni nini, na sababu gani mutu anayezoea kutukana wengine anajitia katika hatari?

13 Matukano. Kama tulivyosema hapo mwanzoni, maneno yana nguvu ya kuumiza. Ni kweli kwamba, kwa sababu sisi ni watu wasio wakamilifu wakati fulani tunasikitika kwa sababu tulisema mambo fulani yasiyofaa. Hata hivyo, Biblia inatuonya juu ya tabia ya kusema maneno fulani yasiyofaa kabisa katika familia yetu ao katika kutaniko. Mutume Paulo aliwaonya Wakristo hivi: ‘Uchungu wote wenye uovu na hasira na gazabu na kupiga kelele na matukano na viondolewe mbali kutoka kwenu pamoja na ubaya wote.’ (Waefeso 4:31) Tafsiri zingine za Bibilia zinatumia maneno kama vile “maneno maovu,” “usemi wenye kuumiza,” na “matusi,” mahali pa neno “matukano.” Matukano, maana yake, matusi na kuchambua-chambua watu kwa ukali; yanaweza kuwaharibishia wengine sifa na kuwafanya wajisikie kuwa watu wa bure. Watoto wanaamini mambo kwa haraka na wana moyo unaoguswa kwa haraka, kwa hiyo wanapotukanwa wanaumia zaidi moyoni.—Wakolosai 3:21.

14 Biblia inatukataza kabisa kuwatukana wengine, ni kusema, inakataza mazoea ya kuwaharibishia wengine sifa kwa matusi, maneno ya kuwazarau wengine, ao kuwafezehesha. Mutu anayezoea kuwatukana wengine hivyo anajitia katika hatari; ikiwa anashauriwa mara kwa mara na habadilike, anaweza kutengwa na kutaniko. Anaweza pia kukosa baraka za Ufalme katika dunia mupya. (1 Wakorintho 5:11-13; 6:9, 10) Kwa hiyo, hatuwezi kubaki katika upendo wa Mungu ikiwa tuna mazoea ya kusema maneno machafu, maneno yasiyo ya kweli, ao yenye kuumiza. Maneno kama hayo yanabomoa.

MANENO MAZURI ILI KUJENGA

15. Kusudi maneno yawe ‘mazuri ili kujenga’ yanapaswa kuwa namna gani?

15 Namna gani tunaweza kutumia zawadi ya kusema kama vile Yehova alivyokusudia? Usisahau kama Neno la Mungu linatushauria tutumie ‘neno lolote ambalo ni njema [ao nzuri] ili kujenga.’ (Waefeso 4:29) Yehova anafurahi sana tunapotumia maneno yanayowajenga wengine, yanayowatia moyo na yanayowatia nguvu. Ili kutumia maneno kama hayo, inaomba kufikiri kwanza. Biblia haina mupangilio fulani wa maneno tunayopaswa kutumia; wala haina oroza (liste) ya “maneno yenye afya” yanayokubaliwa. (Tito 2:8) Ili kutumia maneno yaliyo mazuri ili kujenga, tunapaswa kukumbuka mambo matatu mepesi lakini ya maana yanayofanya maneno yetu yawe yenye kujenga: Yanapaswa kuwa safi, ya kweli, na yasiyoumiza. Kwa kuwa tunajua mambo hayo, acheni tuchunguze mifano fulani ya maneno yenye kujenga.—Soma kisanduku “Je, Maneno Yangu Yanawajenga Wengine?”

JE, MANENO YANGU YANAWAJENGA WENGINE?

Mwanamuke mumoja anazungumuza na mwenzake kwa upole

Kanuni: “Maneno yenu na yawe yenye neema sikuzote”—Wakolosai 4:6.

Ujiulize

  • Ni tangu wakati gani nilimupongeza mutu kwa sababu ya jambo fulani?—1 Wakorintho 11:2; Ufunuo 2:1-3.

  • Ninasema asante ao tafazali ili kuonyesha kama ninawaheshimu wengine?—Mwanzo 13:14; Yohana 11:41.

  • Ninapozungumuza na wengine, je, ninapenda mimi niseme tu ao ninasikiliza pia wengine na kupenda kujua mawazo yao?—Wafilipi 2:3, 4; Yakobo 1:19.

  • Ninatumia mambo ninayojua juu ya wengine ili kuwajenga ao kuwavunja moyo?—Methali 15:1, 2.

  • Nina mawazo gani juu ya maneno machafu, na hilo linaonyesha nini juu ya hali ya moyo wangu?—Luka 6:45; Yakobo 3:10, 11.

16, 17. (a) Sababu gani tunapaswa kuwapongeza ao kuwasifu wengine? (b) Ni mambo gani yanayoweza kutusukuma tuwapongeze wengine katika kutaniko? na katika familia?

16 Kumupongeza mutu bila unafiki. Yehova na Yesu wanajua kama kumupongeza mutu na kumufanya ajisikie kuwa anakubaliwa ni jambo la lazima sana. (Mathayo 3:17; 25:19-23; Yohana 1:47) Ni vizuri sisi Wakristo pia tuwapongeze ao tuwasifu wengine bila unafiki. Sababu gani? Andiko la Methali 15:23 linasema hivi: ‘Neno linalosemwa wakati unaofaa ni njema kama nini!” Ujiulize kwanza hivi: “Ninajisikia namna gani watu wanaponipongeza pasipo unafiki? Je, ninajisikia mwenye furaha na kutiwa moyo?’ Kwa kweli, mutu anapokupongeza kwa maneno yasiyo ya unafiki, unajisikia kuwa mutu huyo anakufikiria, anahangaikia yale unayofanya na kwamba mambo yale unayofanya ni ya maana. Maneno ya mutu huyo yanakufanya ujisikie kuwa wewe si mutu wa bure na yanakuchochea kufanya hata zaidi. Kwa sababu wewe unajisikia vizuri unapopongezwa, je, hauone kama inafaa wewe pia ujikaze kabisa kuwapongeza wengine?​—Mathayo 7:12.

17 Ujikaze kuona sifa nzuri za wengine na kisha usisite kuwapongeza. Labda katika kutaniko unaweza kusikia ndugu fulani anatoa hotuba nzuri, unaweza kuona kijana anayefanya maendeleo ili kufikia miradi ya kiroho, ao unaweza kuona ndugu ao dada ambaye anahuzuria kwa ukawaida mikutano hata ikiwa yeye amekwisha kuzeeka kabisa. Kuwapongeza watu kama hao kunaweza kugusa moyo wao na kuwatia nguvu kiroho. Katika familia, bwana anajisikia mwenye furaha anaposikia bibi yake anamupongeza na kumushukuru, na bibi pia anajisikia hivyo anaposikia bwana yake anamupongeza ao kumusifu na kumushukuru. (Methali 31:10, 28) Zaidi sana watoto wanajisikia vizuri wanapoona wazazi wao wanawahangaikia na kuwaona kuwa wa lazima. Mumea unapopata maji na mwangaza wa jua, unakomaa vizuri; vilevile, watoto wanapopongezwa na kuona kuwa wazazi wao wanawaona kuwa watu wa lazima, wanajisikia vizuri na kutiwa nguvu. Kwa hiyo, ninyi wazazi, musikose kuwapongeza watoto wenu kwa sababu ya sifa zao nzuri na nguvu wanazofanya inapoomba kufanya hivyo. Maneno kama hayo yanaweza kuwatia nguvu na kuwafanya wajisikie kuwa watu wa maana na pia yanaweza kuwachochea hata zaidi kutenda mambo mazuri.

18, 19. Sababu gani tunapaswa kufanya yote tuwezayo ili kumufariji na kumutuliza Mukristo mwenzetu ambaye amevunjika moyo, na tunaweza kufanya hivyo namna gani?

18 Maneno yenye kutuliza moyo na kufariji. Yehova anahangaikia sana “watu wa hali ya chini” na “wale wanaopondwa.” (Isaya 57:15) Neno lake linatushauri ‘tuendelee kufarijiana’ na ‘tuseme kwa kuzifariji nafsi zilizohuzunika.’ (1 Wathesalonike 5:11, 14) Kwa hiyo, tunaweza kuwa na uhakika kwamba Mungu anaona na anafurahia nguvu tunazofanya ili kuwatuliza na kuwafariji ndugu na dada zetu ambao mioyo yao inajaa huzuni.

Muzee Mukristo anatolea bibi na bwana mashauri yenye kujenga

Yehova anafurahi wakati tunasema maneno yenye kujenga wengine

19 Kwa hiyo, tunaweza kusema nini ili kumujenga Mukristo mwenzetu ambaye amevunjika moyo ao amehuzunishwa? Usifikiri kwamba unapaswa kumaliza tatizo lake. Mara nyingi, maneno machache tu ya kumutuliza moyo yanaweza kumusaidia sana. Umuonyeshe mutu huyo mwenye kuvunjika moyo kwamba unamuhangaikia na kwamba unajitia mahali pake. Umuombe kusali pamoja naye; unaweza kumuomba Yehova amusaidie kutambua kwamba ndugu na dada wengine wanamupenda sana na pia Mungu anamupenda sana. (Yakobo 5:14, 15) Umuonyeshe kama yeye ni ndugu ao dada katika kutaniko, kwa hiyo, ni wa maana sana na anahitajiwa. (1 Wakorintho 12:12-26) Umusomee andiko fulani lenye kutia moyo katika Biblia ili kumuonyesha kama Yehova anamuhangaikia kabisa. (Zaburi 34:18; Mathayo 10:29-31) Kutumia wakati wetu pamoja na mutu aliyevunjika moyo na kumuambia ‘neno nzuri’ kutamufanya ajisikie kuwa anapendwa na kuwa yeye ni mutu wa maana.​—Methali 12:25.

20, 21. Ni mambo gani yanayoweza kufanya shauri likubaliwe bila magumu?

20 Kutoa mashauri mazuri. Sisi ni watu wasio wakamilifu, kwa hiyo, kila wakati sisi wote tuna lazima ya mashauri. Biblia inatushauri hivi: ‘Sikiliza shauri na kukubali nizamu, ili upate kuwa na hekima katika wakati wako ujao.’ (Methali 19:20) Si wazee tu ndio walio na daraka la kutolea wengine mashauri. Wazazi wana daraka la kushauria watoto wao. (Waefeso 6:4) Dada wenye kukomaa wanaweza kuwashauria wanawake vijana. (Tito 2:3-5) Upendo wetu kwa wengine utatuchochea kuwatolea mashauri ambayo wanaweza kukubali bila kujisikia kuwa wanaumizwa. Ni nini inayoweza kutusaidia kutolea wengine mashauri mazuri? Tuchunguze mambo matatu yanayofanya mahauri yakubaliwe bila magumu yanapotolewa: hali nzuri na sababu inayomuchochea mushauri, mahali mashauri hayo yamechukuliwa, na namna yanatolewa.

21 Hali ya mushauri inaweza kufanya shauri likubaliwe ao lisikubaliwe. Kwa hiyo, ujiulize, ‘Mimi ningependa mutu anayenishauria awe katika hali gani ili nikubali shauri lake kwa urahisi?’ Ikiwa unajua kama mushauri wako ni mutu anayekuhangaikia, hazungumuze nawe kwa sababu ya hasira, na kama hana mawazo yoyote mabaya juu yako, itakuwa vyepesi kukubali shauri lake, sivyo? Kwa hiyo, unapowatolea wengine mashauri, unapaswa pia kuwa hivyo, sivyo? Shauri linalokubaliwa bila magumu ni lile linalochukuliwa katika Neno la Mungu. (2 Timotheo 3:16) Iwe tunasoma shauri moja kwa moja katika Biblia ao hapana, shauri lolote tunalotoa linapaswa kuwa na musingi katika Biblia. Ndio sababu wazee wanapaswa kuwa waangalifu ili wasiwalazimishe wengine kufuata mawazo yao; wala hawapaswe kupotosha Maandiko ili kufanya ionekane kama yanaunga mukono mawazo yao ya kipekee. Pia shauri litakubaliwa ikiwa linatolewa kwa namna nzuri. Shauri likitolewa kwa fazili ni rahisi kulikubali, na mutu anayeshauriwa hatajisikia kuwa anafezeheshwa.—Wakolosai 4:6.

22. Namna gani utatumia zawadi yako ya uwezo wa kusema?

22 Kwa kweli, uwezo wa kusema ni zawadi ya bei sana ambayo Mungu alitupatia. Kumupenda Yehova kunapaswa kutuchochea tuitumie zawadi hiyo vizuri. Na tusisahau kwamba maneno tunayotoa katika kinywa chetu yana nguvu ya kujenga ao kubomoa. Kwa hiyo, tujikaze kutumia zawadi hiyo ‘ili kujenga,’ kama Mupaji wa zawadi hiyo alivyokusudia. Tukifanya hivyo, maneno yetu yatawatia moyo na kuwatuliza wale walio karibu yetu na yatatusaidia ili tubaki katika upendo wa Mungu.

a Katika Kiebrania neno linalotafsiriwa “upotovu” kwenye Methali 15:4 linaweza pia kumaanisha “kuenda pembeni,-enye kuharibika.”

b Neno la Kigiriki linalotafsiriwa “ubatili” linatafsiriwa pia na neno “bure” na “isiyozaa.”—1 Wakorintho 15:17; 1 Petro 1:18.

c Katika Biblia, neno “uchafu” linatumiwa katika maana nyingi inayoonyesha zambi ya aina mbalimbali. Hata ikiwa halmashauri ya hukumu haiwezi kuundwa kwa sababu ya kila uchafu, ndugu ao dada anaweza kutengwa na kutaniko kwa sababu ya zoea la ukosefu mukubwa wa usafi na ikiwa hatubu—2 Wakorintho 12:21; Waefeso 4:19; soma “Maulizo ya Wasomaji Wetu” katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 15, Mwezi wa 7, 2006.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine