SURA YA 13
Sikukuu Zinazomuchukiza Mungu
“Endeleeni kuhakikisha lile linalokubalika kwa Bwana.”—WAEFESO 5:10.
1. Ni watu wa namna gani ambao Yehova anavuta kwake, na sababu gani wanapaswa kuendelea kuwa macho kiroho?
YESU alisema hivi: ‘Waabudu wa kweli watamuabudu Baba kwa roho na kweli, kwa maana, kwa kweli, Baba anawatafuta watu wa namna hiyo wamuabudu.’ (Yohana 4:23) Yehova anapopata watu kama hao, kama alivyokupata wewe, anawavuta kwake na kwa Mwana wake. (Yohana 6:44) Hilo ni pendeleo kubwa kabisa! Lakini, watu hao wanaopenda kweli ya Biblia, wanapaswa ‘kuendelea kuhakikisha lile linalokubalika kwa Bwana’ kwa sababu Shetani ni fundi sana wa kudanganya.—Waefeso 5:10; Ufunuo 12:9.
2. Namna gani Yehova anawaona wale wanaojaribu kuchanganya dini ya kweli na ile ya uongo? Fasiria.
2 Tufikirie jambo lililotokea karibu na Mulima Sinai, wakati Waisraeli walimuomba Haruni awafanyie mungu. Kwa sababu ya kukazwa, Haruni alikubali na akatengeneza kitoto cha ngombe cha zahabu, na akawaambia kama sanamu hiyo inamuwakilisha Yehova. Alisema hivi: “Kutakuwa na sherehe [sikukuu] kwa ajili ya Yehova kesho.” Je, Yehova alifurahia tendo hilo la kuchanganya ibada ya kweli na ile ya uongo? Hapana. Kwa sababu ya tendo hilo Yehova aliwaua waabudu-sanamu karibu 3000. (Kutoka 32:1-6, 10, 28) Hilo linatufundisha nini? Ikiwa tunataka kubaki katika upendo wa Mungu, hatupaswe ‘kugusa kitu chochote kisicho safi’ na tunapaswa kuichunga kweli kwa wivu ili isichafuliwe kwa njia yoyote.—Isaya 52:11; Ezekieli 44:23; Wagalatia 5:9.
3, 4. Sababu gani tunapaswa kufikiria kwa uzito kanuni za Biblia tunapochunguza desturi na sikukuu zinazopendwa na watu wengi?
3 Lakini, jambo la huzuni ni kwamba, mitume, wao waliokuwa wanazuia mafundisho ya uongo yasiingie katika kutaniko, walipokufa wote; Wakristo wa uongo ambao hawakupenda mafundisho ya kweli ya Biblia walianza kufuata desturi za kipagani, kufanya sikukuu za mataifa na za kidini na kuanza kuziita kuwa za Kikristo. (2 Wathesalonike 2:7, 10) Unapoangalia vizuri sikukuu hizo, utaona kama zingine zinaonyesha kabisa roho ya ulimwengu, wala si roho ya Mungu. Sikukuu hizo za ulimwengu zinapatana katika jambo hili: zinachochea tamaa ya mwili, zinaunga mukono mafundisho ya dini ya uongo na mambo ya kuzungumuza na pepo ao mashetani; mambo ambayo yanatambulisha ‘Babiloni Mukubwa.’a (Ufunuo 18:2-4, 23) Pia, tusisahau hili: Yehova alijionea yeye mwenyewe mazoea yenye kuchukiza ya dini za kipagani, na dini hizo ndio chanzo cha desturi nyingi zinazopendwa na watu wengi leo. Bila shaka, alichukizwa na sikukuu hizo, leo pia anachukizwa nazo. Hauone kama inafaa watu wafuate mawazo yake juu ya sikukuu hizo?—2 Yohana 6, 7.
4 Kwa sababu sisi ni Wakristo wa kweli, tunajua kama sikukuu fulani zinamuchukiza Yehova. Lakini, tunapaswa kuazimia kabisa katika moyo wetu kutoshiriki hata kidogo katika sikukuu hizo. Acha tuchunguze tena kwa nini Yehova anachukizwa na sikukuu hizo; hilo litatia nguvu azimio letu la kuepuka kila kitu kinachoweza kutuzuia tusibaki katika upendo wa Mungu.
NOELI NI IBADA YA JUA AMBAYO ILIPEWA JINA MUPYA
5. Sababu gani tunaamini kabisa kama Yesu hakuzaliwa tarehe 25, Mwezi wa 12?
5 Hakuna andiko katika Biblia linaloonyesha kama watu walifanya sikukuu ili kukumbuka siku ya kuzaliwa kwa Yesu. Hata tarehe ya kuzaliwa kwake haijulikane. Jambo tunalojua kabisa ni kwamba hakuzaliwa tarehe 25 Mwezi wa 12, kwa sababu wakati huo ni wakati wa baridi kali sana mahali alikozaliwa.b Kwa mufano, Luka aliandika kwamba wakati Yesu alizaliwa, ‘wachungaji walikuwa wakiishi inje,’ wakichunga makundi yao ya wanyama. (Luka 2:8-11) Ikiwa wachungaji walikuwa ‘wakiishi inje’ kila mwezi, hakungekuwa na lazima ya kutaja jambo hilo. Lakini, kwa kuwa Mwezi wa 12, ni wakati wa baridi sana Bethlehemu, ni kipindi cha mvua na teluji, wakati huo wanyama walikuwa wakifungiwa ndani, na wachungaji hawangeishi inje. Pia, Yosefu na Maria walienda Bethlehemu kwa sababu César Auguste alikuwa ameamuru watu wahesabiwe. (Luka 2:1-7) Ni vigumu kufikiri kwamba César angewaamuru watu ambao walikuwa wanachukia utawala wa Roma wafunge safari ili kuenda kujiandikisha katika majiji ya kwao wakati wa kipindi cha baridi kali sana hivyo.
6, 7. (a) Desturi nyingi za Noeli zilianzia wapi? (b) Kuna tofauti gani kati ya kutoleana zawadi wakati wa Noeli na kutoleana zawadi kwa Wakristo?
6 Noeli haikutokana na Biblia, lakini inatokana na sikukuu za zamani za kipagani, kama vile sikukuu ya Waroma inayoitwa Saturnalia, sikukuu iliyokuwa ikifanywa kwa ajili ya Saturne, mungu wa kilimo ao mashamba. Vilevile kitabu fulani kinasema kwamba waabudu wa mungu Mithra walifanya sikukuu ya “kuzaliwa kwa jua lisiloweza kushindwa” tarehe 25 Mwezi wa 12. “Noeli ilianza wakati ibada ya mungu-jua ilikuwa nguvu sana katika Roma,” miaka 300 hivi kisha kifo cha Kristo.—New Catholic Encyclopedia.
Upendo unachochea Wakristo wa kweli kutolea wengine
7 Wakati wapagani walikuwa wanafurahia sikukuu zao, walikuwa wanatoleana zawadi, walikuwa wanakula na kunywa; mambo ambayo watu wanazoea kufanya hata leo wakati wa Noeli. Lakini, kama ilivyo leo pia, mazoea ya kutoleana zawadi wakati huo hayakupatana kabisa na shauri la andiko la 2 Wakorintho 9:7, linalosema: ‘Kila mumoja na afanye kama alivyoazimia moyoni mwake, si kwa kutopenda wala kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu anamupenda mutoaji muchangamufu.’ Upendo ndio unawasukuma Wakristo wa kweli kuwatolea wengine zawadi; wala hawalazimishwe kungojea tarehe fulani ili kufanya hivyo; wanapomutolea mutu fulani zawadi hawatazamie mutu huyo awatolee pia zawadi. (Luka 14:12-14; Matendo 20:35) Pia, wao ni wenye furaha sana kwa sababu wao si watumwa tena wa mahangaiko na madeni makubwa ambayo watu wengi wanajiingiza ndani wakati huo wa Noeli.—Mathayo 11:28-30; Yohana 8:32.
8. Je, wale wanajimu walimutolea Yesu zawadi ili kufurahia kuzaliwa kwake? Fasiria.
8 Lakini, watu wengine wanaweza kujitetea hivi: Je, wale wanajimu hawakumutolea Yesu zawadi ili kufurahia siku ya kuzaliwa kwake? Hapana. Hapo zamani watu walikuwa na desturi ya kuwatolea watu wa maana zawadi ili kuwaonyesha heshima. (1 Wafalme 10:1, 2, 10, 13; Mathayo 2:2, 11) Jambo lingine ni kwamba, wanajimu hao hawakuja usiku ule ambao Yesu alizaliwa. Walipofika, Yesu hakuwa kitoto kichanga katika sanduku la kulishia wanyama; walimukuta katika nyumba; alikuwa na umri wa miezi mingi.
YALE BIBLIA INASEMA KUHUSU SIKUKUU ZA KUZALIWA
9. Ni mambo gani yaliyotendeka kwenye sikukuu za kuzaliwa ambazo Biblia inazungumuzia?
9 Hata ikiwa sikuzote kuzaliwa kwa mutoto ni jambo lenye kuleta furaha sana, hakuna andiko katika Biblia linaloonyesha kwamba watu walifanya sikukuu ya kuzaliwa kwa ajili ya mutumishi fulani wa Mungu. (Zaburi 127:3) Je, tunaweza kusema kwamba ni kusahau tu? Hapana, kwa sababu Biblia inazungumuzia sikukuu za kuzaliwa mbili: ile ya Farao na ile ya Herode Antipa. (Mwanzo 40:20-22; Marko 6:21-29) Hata hivyo, Biblia inaonyesha kwamba kwenye sikukuu hizo mbili mambo mabaya yalifanyika, hasa kwenye sikukuu ya kuzaliwa kwa Herode, kwa kuwa siku hiyo Yohana Mubatizaji alikatwa kichwa.
10, 11. Wakristo wa kwanza waliona namna gani kufanya sikukuu ya kukumbuka siku ya kuzaliwa kwa mutu, na sababu gani?
10 Kitabu fulani kinasema hivi: “Wakristo wa kwanza waliona sikukuu ya kukumbuka siku ya kuzaliwa kwa mutu, hata iwe nani, kuwa desturi ya kipagani.” (The World Book Encyclopedia) Kwa mufano, Wagiriki wa zamani waliamini kwamba kila mutu ana roho fulani inayomulinda, na kwamba roho hiyo ilikuwa hapo wakati wa kuzaliwa kwake na inaendelea kumulinda maisha yake yote. Kitabu kingine kinasema kwamba roho hiyo “ilikuwa na uhusiano wa kiajabu pamoja na mungu ambaye siku ya kuzaliwa kwake ililingana na siku ya kuzaliwa kwa mutu huyo.” (Les coutumes et usages des anniversaires (katika Kiingereza) Pia, tangu zamani, sikukuu za kukumbuka siku ya kuzaliwa kwa mutu zina uhusiano na mambo ya unajimu ao uaguzi kupitia nyota ao elimu ya kutabiri maisha ya watu kupitia nyota.
11 Watumishi wa Mungu waliepuka sikukuu hizo za kukumbuka siku ya kuzaliwa kwa mutu kwa sababu zilikuwa za kipagani ao zilihusiana na mambo ya kuzungumuza na pepo; waliziepuka pia kwa sababu hazikupatana na kanuni za Biblia. Kwa nini? Wanaume na wanawake hao walikuwa watu wanyenyekevu na wenye kiasi ambao hawakuona siku ya kuzaliwa kwao kuwa jambo la maana sana linalopaswa kufanyiwa sikukuu.c (Mika 6:8; Luka 9:48) Badala yake, walimutukuza Yehova na kumushukuru kwa sababu ya zawadi yenye bei ya uzima.d—Zaburi 8:3, 4; 36:9; Ufunuo 4:11.
12. Namna gani siku yetu ya kufa ni nzuri zaidi kuliko siku tuliyozaliwa?
12 Watu waaminifu wote wanapokufa, Mungu anawachunga vizuri katika akili yake, na kuna tumaini kwamba atawarudisha kwenye uzima. (Ayubu 14:14, 15) Andiko la Mhubiri 7:1, linasema hivi: ‘Jina ni bora kuliko mafuta mazuri, na siku ya kufa kuliko siku ya kuzaliwa kwa mutu.’ “Jina” letu ni sifa nzuri ambayo tumejifanyia mbele za Mungu kwa kumutumikia kwa uaminifu. Ni jambo la lazima kujua kwamba Wakristo wameamuriwa kukumbuka tu kifo cha Yesu, wala si kuzaliwa kwake; wokovu wetu unategemea “jina” lake nzuri.—Luka 22:17-20; Waebrania 1:3, 4.
PASAKA NI SIKUKUU INAYOFICHA IBADA YA UWEZO WA KUZAA
13, 14. Desturi zinazopendwa na watu wengi za sikukuu ya Pasaka zilitoka wapi?
13 Hata ikiwa watu wanafikiri kwamba Pasaka ni sikukuu ya kukumbuka ufufuo wa Kristo, ukweli ni kwamba inatokana na dini ya uongo. Jina Pasaka linaweza kumufanya mutu afikiri kwamba ni ile Pasaka ya Wayahudi, lakini ni tofauti. Sikukuu hiyo inaitwa Easter katika Kiingereza, nayo inatokana na jina Eostre, ao Ostara, jina la mungu wa mapambazuko na majira ya kuchipuka kwa majani aliyekuwa akiabudiwa na watu wa zamani wa Angleterre. Na namna gani sungura na mayai vimefikia kutumiwa wakati wa sikukuu hiyo ya Pasaka? Kitabu kimoja kinasema kwamba mayai kwa “muda murefu yamekuwa yakitumiwa kama alama ya uzima mupya na ufufuo,” nayo sungura kama alama ya uwezo wa kuzaa. (Encyclopædia Britannica) Kwa hiyo, sikukuu hiyo ya Pasaka, kwa kweli ni sikukuu inayoficha ibada ya uwezo wa kuzaa, ambayo wanasingizia kuwa ni sikukuu ya kufufuka kwa Kristo.e
14 Yehova anaweza kukubali watu wafurahie sikukuu ya ibada ya uwezo wa kuzaa, ibada yenye kuchukiza, ili kukumbuka ufufuo wa Mwana wake? Hilo haliwezekane! (2 Wakorintho 6:17, 18) Hakuna andiko katika Biblia linaloamuru ao kuruhusu kufanya ukumbusho wa kufufuka kwa Yesu. Kwa hiyo, kukumbuka ufufuo wa Yesu kwa kuuvalisha jina la Pasaka, sikukuu ya wapagani, ni kukosa uaminifu sana.
SIKUKUU YA WATAKATIFU WOTE SI YA KIKRISTO
15. Sikukuu ya Halloween ilitoka wapi, na tarehe waliochagua ili kufanya sikukuu hiyo inaonyesha nini?
15 Sikukuu ya Watakatifu Wote, inayoitwa Halloween inafanywa siku inayotangulia “Siku ya Watakatifu Wote.” Kwenye sikukuu hiyo watu wanavaa kama wachawi; wanavaa mavazi ya kutisha na vitu vingine vya kuchorwa vinavyoogopesha. Sikukuu hiyo ilianzishwa na Waselti wa zamani wa Angleterre na Irlande. Siku iliyokuwa na mwezi wenye kuonekana muzima karibu zaidi na tarehe 1 Mwezi wa 11, Waselti walikuwa wakikumbuka sikukuu ya Samain, maana yake, “mwisho wa kipindi cha jua kali.” Walikuwa wanaamini kwamba wakati wa Samain, pazia iliyokuwa inatenga wanadamu na ulimwengu wa roho iliondolewa na kwamba roho wema na waovu walikuwa wanazunguka-zunguka duniani. Ilizaniwa kuwa nafsi za watu waliokufa zilirudi katika familia zao; na familia zao zilikuwa zinaweka kwenye milango chakula na pombe ili kutuliza nafsi hizo. Kwa hiyo, leo wakati watoto wanavaa kama wachawi na kuenda nyumba kwa nyumba na kuwatisha watu kwamba watawalaani ikiwa hawawape zawadi, wanaendeleza bila kujua desturi hiyo ya Samain.
FANYA SIKU YA NDOA YAKO ISICHAFULIWE
16, 17. (a) Sababu gani Wakristo wanaojitayarisha kufunga ndoa wanapaswa kuchunguza ikiwa desturi za siku ya ndoa za mahali pao zinapatana na kanuni za Biblia? (b) Juu ya desturi kama vile kutupia watu muchele ao vitu vingine, ni nini Wakristo wanapaswa kujua?
16 Hivi karibuni, “hakuna sauti ya bwana-arusi na bibi-arusi itakayosikiwa tena kamwe ndani” ya Babiloni Mukubwa. (Ufunuo 18:23) Sababu gani? Sababu moja ni hii: mazoea ya Babiloni Mukubwa ya kupashana habari na pepo ao mashetani yanaweza kuchafua ndoa yenu tangu mwanzo wayo.—Marko 10:6-9.
17 Kila inchi ina desturi zake. Labda zingine zinaweza kuonekana kuwa si mbaya, lakini zilitokana na desturi za Kibabiloni; watu walikuwa wanafikiri zitawaletea bwana-arusi na bibi-arusi ao wageni wao “bahati njema.” (Isaya 65:11) Kama vile desturi ya kuwatupia muchele ao vitu vingine. Labda desturi hiyo ilitokana na wazo la kwamba chakula kinatuliza roho waovu na kuwazuia wasiwazuru bwana-arusi na bibi-arusi. Pia, tangu zamani, muchele umekuwa alama ya uwezo wa kuzaa, furaha, na maisha marefu. Kwa hiyo, ni wazi kwamba wale wanaopenda kubaki katika upendo wa Mungu watakataa desturi hizo chafu.—2 Wakorintho 6:14-18.
18. Wale wanaojitayarisha kufunga ndoa na wale wanaoalikwa wanapaswa kufuata kanuni gani za Biblia?
18 Tena, watumishi wa Yehova wanaepuka mazoea ya ulimwengu ambayo yanaweza kufanya ndoa na karamu ya ndoa isemwe vibaya ao kukwaza zamiri za wengine. Kwa mufano, wanaepuka kufanya hotuba zenye zihaka zinazoumiza ao maneno ya mizaha yanayohusiana na kitendo cha ndoa, ao yanayoweza kufezehesha wale wanaofunga ndoa ao wale wanaohuzuria. (Methali 26:18, 19; Luka 6:31; 10:27) Pia, wanaepuka kufanya karamu zenye mambo mengi, zisizo na kiasi, ambazo ni njia ya ‘mutu kujionyesha mali yake maishani.’ (1 Yohana 2:16) Ikiwa unajitayarisha kufunga ndoa, usisahau kwamba Yehova anataka siku hiyo yako ya pekee, unapoikumbuka katika maisha yako, usijute, lakini uwe mwenye furaha kabisa.f
KUINUA BILAURI NA KUVIGONGANISHA—NI VIBAYA?
19, 20. Kitabu kimoja kinasema nini juu ya chanzo cha desturi ya kuinua bilauri na kuvigonganisha, na sababu gani Wakristo wanapaswa kuepuka desturi hiyo?
19 Mara nyingi kwenye karamu ya ndoa ao karamu zingine, watu wanazoea kuinua bilauri na kuvigonganisha ili kuwatakia wengine heri. Kitabu Le Guide international des alcools et des cultures cha mwaka wa 1995, (katika Kiingereza) kinasema: “Kuinua bilauri na kuvigonganisha . . . labda zoea hilo linatokana na desturi ya zamani ya kufanya matambikio ili kuwatolea miungu kinywaji kitakatifu . . . ili sala ikubaliwe, sala fupi yenye maneno ‘maisha marefu’ ao ‘afya njema!’”
20 Ni kweli, labda watu wengi hawataona desturi hiyo kuwa ya kidini ao ya mambo ya uchawi. Hata hivyo, desturi ya kuinua bilauri vyenye kuwa na divai ao pombe na kuvigonganisha inaweza kuonekana kuwa alama ya kuomba baraka fulani “mbinguni,” ni kusema, kuomba nguvu fulani isiyo ya kawaida. Wengine wamekuwa na desturi ya kumwanga pombe kwenye udongo kuwa sadaka ya kinywaji ili wasipatwe na jambo mbaya ao kuwafurahisha mababu waliokufa. Desturi hizo hazipatane na Maandiko.—Yohana 14:6; 16:23.g
‘NINYI MUNAOMUPENDA YEHOVA, MUCHUKIE YALIYO MABAYA’
21. Ni sikukuu gani zinazopendwa na watu wengi ambazo hata ikiwa si za kidini, Wakristo wanapaswa kuziepuka, na kwa nini?
21 Leo, mwenendo wa watu wengi ni wenye kuharibika sana, kwa sababu Babiloni Mukubwa amechochea waziwazi mwenendo huo ao amefunga macho juu ya mwenendo huo. Kwa mufano, inchi fulani zina sikukuu fulani zinazofanywa kila mwaka, kama vile carnaval ao Mardi Gras; wakati huo watu wanacheza dansi chafu na kusifu wanaume wanaolala na wanaume na wanawake wanaolala na wanawake wenzao. Je, mutu ‘anayemupenda Yehova’ kabisa anaweza kweli kuenda kwenye maandamano (ao defile) hayo ao kutazama jambo hilo kwenye televizyo? Akifanya hivyo, je, ataonyesha kweli kwamba anachukia yaliyo mabaya? (Zaburi 1:1, 2; 97:10) Ni vizuri kabisa kumuiga mutunga-zaburi, aliyesali hivi: “Uyafanye macho yangu yapite ili yasione jambo lisilofaa!”—Zaburi 119:37.
22. Ni sikukuu gani ao desturi gani Mukristo anaweza kuamua kulingana na zamiri yake ikiwa atashiriki ao hapana?
22 Siku watu wa ulimwengu wanafurahia sikukuu zao, Mukristo anapaswa kuwa mwangalifu ili mwenendo wake usionyeshe kama yeye pia anajiunga nao. Mutume Paulo aliandika: ‘Kama munakula ao munakunywa ao munafanya jambo lingine lolote, mufanye mambo yote kwa utukufu wa Mungu.’ (1 Wakorintho 10:31; soma kisanduku “Namna ya Kufanya Maamuzi Mazuri.”) Lakini, ikiwa desturi ao sikukuu fulani haina ndani mambo ya kidini, ya politike, ya kutukuza taifa, ao haivunje kanuni yoyote ya Biblia, basi kila Mukristo anaweza kuamua mwenyewe ikiwa ataishiriki ao hapana. Hata hivyo, anapaswa pia kufikiria jinsi wengine wataona jambo hilo ili asiwakwaze.
TUMUTUKUZE MUNGU KWA MANENO NA MATENDO
23, 24. Namna gani tunaweza kutolea watu ushahidi muzuri kuhusu sheria za haki za Yehova?
23 Jambo la kwanza ambalo watu wengi wanafikiria juu ya sikukuu hizo ni kwamba zinawatolea nafasi ya kukutana na watu wa familia na marafiki. Kwa hiyo, ikiwa mutu fulani anatulaumu kwamba tunapitisha kiasi ao tunakosa upendo kwa sababu tunafuata yale Biblia inasema, tunaweza kumuelezea kwa upole kwamba Mashahidi wa Yehova wanapitisha pia wakati na watu wa familia na marafiki ili kufurahi pamoja. (Methali 11:25; Mhubiri 3:12, 13; 2 Wakorintho 9:7) Tunafanya hivyo siku ni siku katika mwaka. Hata hivyo, kwa sababu tunamupenda Mungu na sheria zake, hatungependa desturi zinazomuchukiza Mungu ziharibu wakati huo wenye furaha tunaopitisha pamoja.—Soma kisanduku “Ibada ya Kweli Inamuletea Mutu Furaha ya Kweli.”
24 Mashahidi wa Yehova fulani walipata nafasi ya kujibia watu waliotaka kujua kabisa hali yetu juu ya sikukuu mbalimbali, walitumia habari zinazopatikana kwenye sura ya 16 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini?h Hata hivyo, usisahau kwamba kusudi letu ni kuwasaidia watu wajue mafundisho ya kweli, wala si kushinda mabishano. Kwa hiyo, uwe mwenye heshima, onyesha upole, na ‘maneno yako yawe yenye neema sikuzote, yenye kukolezwa chumvi.’—Wakolosai 4:6.
25, 26. Namna gani wazazi wanaweza kuwasaidia watoto wao wakomae katika imani na wamupende Yehova zaidi?
25 Kwa kuwa sisi ni watumishi wa Yehova, tumefundishwa vizuri mambo mengi. Tunajua mambo tunayoamini na tunajua sababu gani hatufanye mambo fulani. (Waebrania 5:14) Kwa hiyo, wazazi muwafundishe watoto wenu wajue kutumia kanuni za Biblia. Munapofanya hivyo, imani yao inatiwa nguvu, munawasaidia kutumia Maandiko ili kuwajibu wale wanaowauliza juu ya mambo wanayoamini, na munawasaidia kuona kama Yehova anawapenda.—Isaya 48:17, 18; 1 Petro 3:15.
26 Wale wote wanaomuabudu Mungu “kwa roho na kweli” wanaepuka sikukuu zisizopatana na Biblia na zaidi ya hilo wanajikaza kujiendesha kwa uaminifu. (Yohana 4:23) Leo, watu wengi wanasema hakuna faida ya kujiendesha hivyo. Lakini katika sura inayofuata tutaona kwamba jambo Mungu anatuomba tufanye ndio njia inayoleta faida zaidi.
a Soma kisanduku “Je, Nijiunge na Wengine Katika Sikukuu Hii?””. Sikukuu fulani za mataifa na za kidini zinaonyeshwa katika Index des publications Watch Tower, iliyochapishwa na Mashahidi wa Yehova.
b Kwa kutegemea hesabu za Biblia na historia ya wanadamu, inaonekana Yesu alizaliwa mwaka wa 2 mbele ya wakati wetu, mwezi wa Ethanimu, ambao ni mwezi wa Kiyahudi unaopatikana katikati ya Mwezi wa 9 na wa 10, kulingana na kalendari yetu ya leo.—Soma kitabu Étude perspicace des Écritures, Buku la 2, ukurasa wa 21, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.
c Soma kisanduku Siku ““Takatifu” Katika Ibada ya Kishetani.”
d Agano la Sheria lilimuomba mwanamuke amutolee Mungu toleo la zambi kisha kuzaa. (Mambo ya Walawi 12:1-8) Sheria hiyo iliwakumbusha Waisraeli kwamba wanadamu wanapitisha zambi kwa watoto wao, na sheria hiyo iliwasaidia kuwa na maoni yanayofaa juu ya kuzaliwa kwa mutoto, na labda iliwasaidia wasifuate desturi za kipagani juu ya siku ya kuzaliwa.—Zaburi 51:5.
e Eostre alijulikana pia kuwa mungu-mwanamuke wa uwezo wa kuzaa. Kulingana na Dictionnaire de la Mythologie (katika Kiingereza), “Eostre alikuwa na sungura wake mwenye kupenda mayai sana aliyeonekana katika mwezi, pia sanamu yake [Eostre] inamuonyesha akiwa mwenye kichwa cha sungura.”
f Soma habari tatu zinazozungumuzia siku ya ndoa na karamu ya ndoa katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 10, 2006, ukurasa wa 18-31.
g Soma Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 2, 2007, ukurasa wa 30-31.
h Kimechapishwa na Mashahidi wa Yehova.