Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • bt sura 25 uku. 196-202
  • “Ninapeleka kesi yangu ya hukumu kwa Kaisari!”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Ninapeleka kesi yangu ya hukumu kwa Kaisari!”
  • “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Kusimama Mbele ya Kiti cha Hukumu’ (Mdo. 25:1-12)
  • “Mimi Sikukosa Kutii” (Mdo. 25:13–26:23)
  • “Ungenishawishi Nikuwe Mukristo” (Mdo. 26:24-32)
  • Ukuwe Hodari​—Yehova Ni Musaidizi Wako
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Paulo Anapelekwa Roma
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • “Neno la Yehova Likaendelea Kuongezeka”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
“Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
bt sura 25 uku. 196-202

SURA YA 25

“Ninapeleka Kesi Yangu ya Hukumu kwa Kaisari!”

Paulo anatuachia mufano wa kutetea habari njema

Inategemea Matendo 25:1–26:32

1, 2. (a) Paulo anajikuta mu hali gani? (b) Tunaweza kujiuliza ulizo gani?

MAASKARI wako wanamuchunga sana Paulo katika Kaisaria. Miaka mbili mbele ya pale wakati alirudia Yudea kwa siku mbili tu, Wayahudi walijaribu kumuua karibu mara tatu. (Mdo. 21:27-36; 23:10, 12-15, 27) Mupaka sasa, maadui wake hawajaweza kumuua, lakini hawachoke. Wakati Paulo anatambua kama inawezekana aangukie tena mu mikono ya maadui wake, anaambia hivi Festo, gavana Muroma: “Ninapeleka kesi yangu ya hukumu kwa Kaisari!”−Mdo. 25:11.

2 Yehova aliunga mukono uamuzi wa Paulo wa kupeleka kesi yake kwa mutawala wa Roma? Jibu ya ile ulizo ni ya maana kwetu, juu tuko tunatoa ushahidi kwa ukamili kuhusu Ufalme wa Mungu mu hizi siku za mwisho. Tuko na lazima ya kujua ikiwa Paulo alituachia mufano wa kufuata “katika kutetea habari njema na kuifanya ikubaliwe kisheria.”​—Flp. 1:7.

‘Kusimama Mbele ya Kiti cha Hukumu’ (Mdo. 25:1-12)

3, 4. (a) Juu ya nini Wayahudi waliomba Paulo apelekwe Yerusalemu, na namna gani Paulo aliponyoka kifo? (b) Namna gani Yehova anategemeza watumishi wake leo sawa vile alitegemeza Paulo?

3 Siku tatu kisha Festo kuwa gavana wa Yudea, alienda Yerusalemu.a Kule, alisikia makuhani na wanaume wenye vyeo kati ya Wayahudi wakimushitaki Paulo makosa mazito. Walijua kama Waroma walipenda ule gavana afanye amani pamoya nao na Wayahudi wote. Kwa hiyo, walimuomba awafanyie jambo fulani, walimuambia hivi: Umulete Paulo Yerusalemu, na umuhukumu huku. Lakini, walikuwa na mupango mubaya wakati waliomba vile. Walikuwa wanapanga kumuua Paulo mu njia ya kutoka Kaisaria kuenda Yerusalemu. Festo hakukubali ombi yao, aliwaambia hivi: “Basi wale wenye kuwa na mamlaka kati yenu washuke pamoja na mimi [katika Kaisaria] na wamushitaki, kama kwa kweli mwanaume huyu amefanya kosa fulani.” (Mdo. 25:5) Kwa hiyo, mara ingine Paulo aliponyoka kifo.

4 Mu magumu yote ya Paulo, Yehova alitumia Yesu Kristo ili kumutegemeza. Kumbuka kama, mu maono, Yesu aliambia hivi ule mutume wake: “Usiogope!” (Mdo. 23:11) Leo pia, watu wa Mungu wanapambana na magumu mingi na wanateswa. Yehova hawaepushe na magumu yote, lakini anawapatia hekima na nguvu ya kuivumilia. Tunaweza kuwa hakika kama Mungu wetu mwenye upendo ataendelea kutupatia “nguvu zenye kupita zile za kawaida.”​—2 Ko. 4:7.

5. Namna gani Festo alishugulikia kesi ya Paulo?

5 Kisha siku fulani, Festo ‘alikaa kwenye kiti cha hukumu’ katika Kaisaria.b Mbele yake kulikuwa Paulo na wenye walikuwa wanamushitaki. Juu walimushitaki mambo yenye hakufanya, Paulo alisema hivi: “Sikutenda zambi yoyote juu ya Sheria ya Wayahudi ao juu ya hekalu ao juu ya Kaisari.” Ule mutume hakukuwa na kosa na alistahili kuachiliwa. Festo angetenda namna gani? Juu alitafuta kukubaliwa na Wayahudi, alimuuliza hivi Paulo: “Je, ungependa kupanda kuenda Yerusalemu uhukumiwe kule mbele yangu juu ya mambo haya?” (Mdo. 25:6-9) Ile haikukuwa wazo ya muzuri kabisa! Kama Paulo angerudishwa Yerusalemu, watu wenye walimushitaki njo wangemuhukumu na bila shaka angeuawa. Mu hii hali, Festo alikuwa anahangaikia sana kufurahisha watu kuliko kutenda kwa haki. Pontio Pilato, mwenye alikuwaka pia gavana, alitendaka vilevile wakati alikuwa anashugulikia kesi ya mufungwa fulani wa maana sana. (Yoh. 19:12-16) Leo pia, waamuzi wanaweza kututendea bila haki juu tu ya kufurahisha watu. Kwa hiyo, hatupaswe kushangala wakati tribinali zinatuhukumu hata kama kuko ushuhuda wenye unaonyesha kama hatuna kosa.

6, 7. Juu ya nini Paulo aliomba kesi yake isikilizwe na Kaisari, na aliachia Wakristo wa kweli mufano gani?

6 Tamaa ya Festo ya kufurahisha Wayahudi ingefanya Paulo auawe. Kwa hiyo, Paulo alitumia haki yenye alikuwa nayo akiwa raia wa Roma. Aliambia hivi Festo: “Nimesimama mbele ya kiti cha hukumu cha Kaisari, kwenye ninapaswa kuhukumiwa. Sikutendea Wayahudi kosa, kama vile wewe pia unaelewa muzuri sasa. . . . Ninapeleka kesi yangu ya hukumu kwa Kaisari!” Kwa kawaida, wakati mutu alifanya ile ombi hangeweza kurudia nyuma. Festo alionyesha ile kwa kusema hivi: “Umeomba kesi yako ya hukumu isikilizwe na Kaisari; utaenda kwa Kaisari.” (Mdo. 25:10-12) Kwa kuomba kesi yake isikilizwe na mwenye kuwa na mamlaka zaidi, Paulo aliachia mufano Wakristo wa kweli leo. Wakati wapinzani wanajaribu kutuletea “matatizo kwa kutumia sheria,” Mashahidi wa Yehova wanatafuta musaada kwenye tribinali ili kutetea haki yetu ya kuhubiri habari njema.c​—Zb. 94:20.

7 Kwa hiyo, kisha kufungwa kwa miaka mbili juu ya makosa yenye hakufanya, Paulo alipewa nafasi ya kujitetea katika Roma. Lakini, mbele aende kule, mutu mwingine mwenye mamlaka alipenda kumuona.

Watu mu jumba ya tribinali kisha uamuzi kutolewa. Ndugu, mwanasheria, na Mashahidi wengine wote hawafurahi. Watu wenye hawako Mashahidi wanafurahi na wako napongeza kikundi ya wanasheria wenye walikuwa nasamba na Mashahidi.

Tunaomba kusikilizwa na tribinali kubwa zaidi wakati waamuzi wanatuhukumu

“Mimi Sikukosa Kutii” (Mdo. 25:13–26:23)

8, 9. Juu ya nini Mufalme Agripa alitembelea Kaisaria?

8 Siku fulani kisha Paulo kuomba kesi yake ipelekwe kwa Kaisari, Mufalme Agripa na dada yake Bernike ‘walimutembelea Festo [gavana wa mupya] ili kumusalimia’.d Zamani mu Utawala wa Roma, watu wenye mamlaka walikuwa na zoea ya kutembelea magavana wapya. Bila shaka, wakati Agripa alienda kumutembelea Festo ili kumupongeza kwa sababu aliwekwa kuwa gavana, alikuwa anatafuta kuanzisha naye urafiki wenye ungemuletea faida wakati wenye kuya.​—Mdo. 25:13.

KUENDA KWENYE TRIBINALI KWA AJILI YA IBADA YA KWELI LEO

Mara kwa mara, Mashahidi wa Yehova wameomba wasikilizwe na tribinali zenye kuwa kubwa zaidi ili kutetea haki yao ya kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu. Tuone mifano mbili.

Tarehe 28 Mwezi wa 3, 1938, Tribinali Kubwa Zaidi ya Amerika ilibadilisha maamuzi ya tribinali ya jimbo ya Georgia kwa kusema kama ilikuwa makosa kufunga kikundi ya Mashahidi wa Yehova kwa sababu tu walitolea watu vichapo vyenye kutegemea Biblia mu muji wa Griffin. Iliamua pia kama wale Mashahidi walipaswa kulipwa. Ile ilikuwa kesi ya kwanza kati ya kesi za mingi zenye Mashahidi wa Yehova walipeleka ku ile tribinali kubwa ili kutetea haki yao ya kuhubiri habari njema.g

Ingine kesi ilihusu Shahidi mwingine katika Ugiriki mwenye kuitwa Minos Kokkinakis. Kwa kipindi ya miaka 48, alifungwa zaidi ya mara 60. Alishitakiwa kama alikuwa “anafanya watu wabadilishe dini yao.” Mara 18 alipelekwa ku tribinali. Alifanya miaka mingi mu gereza na mu uhamisho katika visiwa vya mbali vya Bahari ya Aegea. Kisha kuhukumiwa kwa mara ya mwisho mu 1986, tribinali kubwa ya Ugiriki ilikatala kumusikiliza tena. Kwa hiyo, aliomba kusikilizwa na Tribinali Kubwa ya Haki za Kibinadamu ya Ulaya. Tarehe 25 Mwezi wa 5, 1993, ile tribinali iliamua kama Ugiriki ilivunja haki ya uhuru wa kuabudu wa ndugu Kokkinakis.

Mashahidi wa Yehova wameomba kusikilizwa na Tribinali Kubwa ya Haki za Kibinadamu ya Ulaya mara mingi na tumepata ushindi mu kesi za mingi. Hakuna tengenezo ingine, ikuwe tengenezo ya kidini ao tengenezo yenye haiko ya kidini, yenye imeweza kutetea haki za kawaida za kibinadamu mbele ya Tribinali Kubwa ya Haki za Kibinadamu ya Ulaya sawa vile tengenezo yetu.

Ushindi wa Mashahidi wa Yehova unaletea watu wengine faida? Mutu fulani mwenye elimu, mwenye kuitwa Charles C. Haynes, aliandika hivi: “Siye wote tuko na deni, tunapaswa kushukuru sana Mashahidi wa Yehova. Hata watukanwe, wafukuzwe mu muji ao wapigwe mara ngapi, wanaendelea kupigania haki yao, na kwa hiyo, haki yetu pia ya kuwa na uhuru wa kuabudu. Wakati wanapata ushindi, na siye wote tunapata ushindi.”

g Ona habari kuhusu uamuzi wa Tribinali Kubwa Zaidi ya Amerika kuhusu uhuru wa kusema yenye ilitolewa mu Amuka! ya tarehe 8 Mwezi wa 1, 2003, ukurasa wa 3-11.

9 Festo alimuambia Mufalme Agripa kuhusu Paulo. Ile ilifanya Agripa apende kuzungumuza na Paulo. Siku yenye ilifuata, wale wanaume wawili wenye mamlaka waliikala kwenye kiti ya hukumu. Lakini, mamlaka yao haikukuwa kitu ikilinganishwa na maneno yenye nguvu yenye Paulo alikuwa karibu kusema.​—Mdo. 25:22-27.

10, 11. Namna gani Paulo alimuonyesha Agripa heshima, na alimuambia nini kuhusu maisha yake ya zamani?

10 Kwa heshima, Paulo alimushukuru Mufalme Agripa kwa nafasi yenye alipewa ya kujitetea mbele yake, zaidi sana juu Mufalme Agripa alijua muzuri desturi za Wayahudi na mabishano yao. Kisha Paulo alianza kueleza maisha yake ya zamani: “Niliishi nikiwa Mufarisayo kulingana na musimamo mukali wa ibada katika zehebu letu.” (Mdo. 26:5) Wakati Paulo alikuwa Mufarisayo, alikuwa anangoya kuya kwa Masiya. Na sasa juu alikuwa Mukristo, alionyesha kwa uhodari kama Yesu Kristo njo ule Masiya mwenye walikuwa wanangoya kwa muda murefu. Kwa hiyo, Paulo alifasiria Agripa kama alikuwa anahukumiwa kwa sababu alikuwa anahubiri kama ahadi ya Mungu, yenye yeye na wapinzani wake waliamini, ilikuwa natimia. Ile ilifanya Agripa apende hata zaidi kumusikiliza Paulo.e

11 Kisha, Paulo alifasiria namna alikuwa anatesa sana Wakristo zamani. Alisema hivi: “Mimi kwa upande wangu, niliamini kwamba nilipaswa kufanya matendo mengi ili kupinga jina la Yesu Munazareti. . . . Kwa sababu nilikuwa nimewakasirikia sana [wafuasi wa Kristo], nilifikia kuwatesa hata katika miji ingine.” (Mdo. 26:9-11) Paulo hakukuwa anatia chumvi. Watu wengi walijua namna alitesa sana Wakristo. (Gal. 1:13, 23) Pengine Agripa alijiuliza: ‘Nini njo ilifanya huyu mwanaume abadilike?’

12, 13. (a) Paulo alisema nini ili kufasiria namna alifikia kuwa Mukristo? (b) Ni mu maana gani Paulo alikuwa ‘napiga-piga miguu yake kwenye michokoo’?

12 Maneno ya Paulo yenye ilifuata, ilijibia ile ulizo: “Wakati nilikuwa katika safari ya kuenda Damasko na nilikuwa na mamlaka na maagizo kutoka kwa wakubwa wa makuhani, katikati ya muchana niliona katika barabara, Ee Mufalme, mwangaza kutoka mbinguni wenye kupita mwangaza wa jua ukanizunguka mimi na wale wenye walikuwa wanasafiri pamoja na mimi. Na wakati tulikuwa tumeanguka chini, nikasikia sauti inaniambia katika luga ya Kiebrania: ‘Sauli, Sauli, sababu gani unanitesa? Kuendelea kupiga-piga miguu yako kwenye michokoo kutafanya uumie.’ Lakini nikasema: ‘Wewe ni nani Bwana?’ Na Bwana akasema: ‘Mimi ni Yesu, mwenye unatesa.’”f​—Mdo. 26:12-15.

13 Mbele Paulo apate ile maono, kwa njia ya mufano alikuwa ‘napiga-piga miguu yake kwenye michokoo [ao fimbo yenye chongo yenye inatumiwa ili kumuongoza munyama].’ Sawa vile tu munyama alikuwa anajiumiza mwenyewe kwa kupiga sehemu yenye kuchongoka ya fimbo yenye kumuongoza, Paulo alikuwa anajiumiza mwenyewe kiroho kwa kutenda kinyume na mapenzi ya Mungu. Wakati Yesu, mwenye alikuwa amefufuliwa, alimutokea Paulo mu barabara ya kuenda Damasko, alisaidia ule mwanaume mwenye alikuwa ameongozwa mubaya abadilishe mawazo yake.​—Yoh. 16:1, 2.

14, 15. Paulo alisema nini kuhusu mabadiliko yenye alifanya mu maisha yake?

14 Kwa kweli, Paulo alifanya mabadiliko makubwa mu maisha yake. Alimuambia hivi Agripa: “Mimi sikukosa kutii maono hayo kutoka mbinguni, lakini kwanza kwa wale wenye kuwa Damasko kisha kwa wale wenye kuwa Yerusalemu, na katika inchi yote ya Yudea, na pia kwa mataifa, nilipeleka ujumbe kwamba wanapaswa kutubu na kugeukia kwa Mungu kwa kufanya matendo yenye yanaonyesha kwamba wametubu.” (Mdo. 26:19, 20) Kwa miaka mingi, Paulo alikuwa anatimiza mugao wenye Yesu alimupatia mu ile maono yenye alimuonyeshaka katikati ya muchana. Matokeo ilikuwa nini? Wale wenye walikubali habari njema yenye Paulo aliwahubiria, walitubu na kuacha tabia zao za mubaya na wakaanza kufanya mapenzi ya Mungu. Wale watu wakakuwa raia wazuri, wakaanza kutii sheria na kuendeleza amani kila fasi kwenye waliishi.

15 Lakini, Wayahudi wenye walikuwa wanamupinga Paulo, hawakuona faida yenye habari njema ilikuwa inaletea watu. Paulo alisema hivi: “Ndiyo sababu Wayahudi walinikamata katika hekalu na wakataka kuniua. Lakini, kwa sababu nimepata musaada kutoka kwa Mungu, ninaendelea mupaka leo kutoa ushahidi kwa wadogo na kwa wakubwa pia.”​—Mdo. 26:21, 22.

16. Namna gani tunaweza kumuiga Paulo wakati tunazungumuza na waamuzi na watawala kuhusu mambo yenye tunaamini?

16 Juu tuko Wakristo wa kweli, tunapaswa ‘sikuzote kuwa tayari kutetea’ imani yetu. (1 Pe. 3:15) Wakati tunazungumuza na waamuzi na watawala kuhusu mambo yenye tunaamini, inaweza kuwa muzuri tuige njia yenye Paulo alitumia wakati alizungumuza na Agripa na Festo. Kwa heshima, tuwaambie namna kweli za Biblia zinabadilisha maisha ya watu, inaweza kuwa maisha yetu ao maisha ya wale wenye walikubali ujumbe wetu. Kwa kufanya vile, tunaweza kugusa mioyo ya watu wenye mamlaka.

“Ungenishawishi Nikuwe Mukristo” (Mdo. 26:24-32)

17. Festo alitenda namna gani kisha kusikia maneno ya Paulo, na namna gani watu wengi leo wanatenda vile?

17 Wakati walikuwa wanasikiliza ushuhuda wenye kusadikisha wa Paulo, wale wanaume wawili wenye mamlaka walishindwa kubakia kimya. Biblia inasema hivi juu ya mambo yenye ilitokea: “Sasa wakati Paulo alikuwa anajitetea kwa kusema mambo hayo, Festo akasema kwa sauti kubwa: ‘Unapoteza akili, Paulo! Kusoma sana kunakufanya upoteze akili!’” (Mdo. 26:24) Namna Festo alitenda, njo vile watu wengi wanatendaka leo. Wanaonaka kama wale wenye wanafundisha mambo yenye Biblia inasema kabisa, wamepoteza akili. Watu wenye walisoma sana mu hii dunia, wanaona kama ni nguvu kukubali mambo yenye Biblia inasema kuhusu ufufuo wa wafu.

18. Paulo alimujibia namna gani Festo, na ile ilifanya Agripa aseme nini?

18 Paulo hakunyamaza, alimujibia hivi ule gavana: “Mimi sipoteze akili, Ee Mutukufu Festo, lakini ninasema maneno ya kweli na ya akili ya muzuri. Kwa maana, kwa kweli, mufalme mwenye ninazungumuza naye kwa uhuru anajua muzuri mambo haya . . . Mufalme Agripa, je, unaamini Manabii? Ninajua unawaamini.” Agripa alimujibia hivi: “Kwa wakati kidogo ungenishawishi nikuwe Mukristo.” (Mdo. 26:25-28) Ikuwe ile maneno ilitoka ku moyo ao hapana, inaonyesha kama ushuhuda wa Paulo uligusa sana ule mufalme.

19. Festo na Agripa walikamata uamuzi gani kuhusu Paulo?

19 Kisha Agripa na Festo wakasimama. Ile ilionyesha kama ilikuwa mwisho wa kumusikiliza Paulo. “Wakati walikuwa wanaondoka, wakaanza kuambiana: ‘Mutu huyu hafanye jambo lolote lenye linastahili kifo ao vifungo vya gereza.’ Kisha Agripa akamuambia Festo: ‘Mutu huyu angeachwa huru kama hangekuwa ameomba kesi yake ya hukumu isikilizwe na Kaisari.’” (Mdo. 26:31, 32) Walijua kama Paulo hakukuwa na kosa. Pengine ile ingefanya waanze kutendea muzuri zaidi Wakristo.

20. Ushahidi wa Paulo mbele ya wale watu wawili wenye mamlaka ulikuwa na matokeo gani?

20 Inaonekana kuwa, wale watu wawili wenye mamlaka hawakukubali habari njema ya Ufalme wa Mungu. Ni kusema Paulo alichokea bure wakati alitetea habari njema mbele yao? Jibu ni hapana. Paulo alipata nafasi ya kuhubiria “wafalme na magavana” katika Yudea, wenye pengine ingekuwa nguvu wahubiriwe mu njia ingine yoyote. (Lu. 21:12, 13) Pia, uaminifu wake na namna alivumilia magumu ilitia moyo ndugu na dada zake.​—Flp. 1:12-14.

21. Wakati tunaendelea kuhubiri tunapata matokeo gani ya muzuri?

21 Leo pia mambo iko vile. Wakati tunaendelea kuhubiri hata kama tunapata magumu na wengine wanatupinga, tunapata matokeo ya muzuri. Tunaweza kutolea ushahidi watu wenye mamlaka, wenye pengine ingekuwa nguvu kupata. Uaminifu wetu na uvumilivu wetu unaweza kutia Wakristo wenzetu moyo, na kuwachochea wao pia wakuwe hodari zaidi mu kazi ya kutoa ushahidi kwa ukamili kuhusu Ufalme wa Mungu.

GAVANA MUROMA PORKIO FESTO

Habari zenye tunajua kabisa kuhusu Porkio Festo, ni zenye zinazungumuziwa mu kitabu ya Matendo ya Mitume na mu maandishi ya Flavius Josèph. Mu mwaka wa 58 hivi K.K.Y. Festo aliwekwa kuwa gavana wa Yudea pa nafasi ya Feliksi. Na inaonekana kama alikufa kisha kutawala kwa miaka mbili ao tatu hivi.

Porkio Festo.

Inaonekana kuwa Festo alikuwa gavana muzuri kuliko Feliksi, mwenye alitawala mbele yake na kuliko Albino, mwenye alitawala kisha yeye. Ku mwanzo wa utawala wa Festo, mu Yudea mulikuwa wanyanganyi wengi. Kulingana na Flavius Josèph, “Festo . . . alijiwekea muradi wa kupatia malipizi wale wenye walikuwa wanavuruga amani mu inchi. Kwa hiyo, alikamata wanyanganyi wengi, na aliua wengi kati yao.” Wakati alikuwa natawala, Wayahudi walijenga ukuta ili kuzuia Mufalme Agripa asikuwe anaona mambo yenye ilikuwa inafanyika ku hekalu. Ku mwanzo, Festo aliwaambia wabomoe ule ukuta. Lakini, wakati Wayahudi walimuomba ikiwa wanaweza kupeleka ile tatizo mbele ya Nero, mutawala wa Roma, aliwaruhusu wapeleke tatizo yao.

Inaonekana Festo alifanya yake yote ili kumaliza watu wenye kuvunja sheria na waasi. Lakini, juu alipenda kuendelea kuwa na uhusiano muzuri na Wayahudi, alikuwa tayari kutenda bila haki. Kwa mufano, ni vile alitendea Paulo.

MUFALME HERODE AGRIPA WA PILI

Agripa mwenye kuzungumuziwa mu Matendo sura ya 25 alikuwa Mufalme Herode Agripa wa Pili, na alikuwa mujukuu wa mutoto wa Herode Mukubwa na mwana wa Herode mwenye alishambulia kutaniko la Yerusalemu miaka 14 yenye ilikuwa imepita. (Mdo. 12:1) Agripa njo alikuwa mutawala wa mwisho wa mu familia ya Herode.

Mufalme Herode Agrippa ya Pili.

Wakati baba yake alikufa mu mwaka wa 44 K.K.Y., Agripa alikuwa na miaka 17 na alikuwa Roma. Kule alikuwa napewa elimu ku makao ya kifalme ya Klaudio, mutawala wa Roma. Washauri wa Mutawala Klaudio waliona kama Agripa hakupaswa kuriti ufalme wa baba yake juu alikuwa angali kijana sana. Kwa hiyo gavana Muroma aliwekwa pa nafasi yake. Hata vile kulingana na Flavius Josèph, wakati Agripa alikuwa angali Roma alizungumuza kwa ajili ya Wayahudi na alitetea haki zao.

Mu mwaka wa 50 hivi K.K.Y., Klaudio alimufanya Agripa kuwa mufalme wa Chalcis na mu mwaka wa 53 K.K.Y., alimuongezea Iturea, Trakoniti, na Abilene. Agripa alipewa mamlaka ya kusimamia hekalu ya Yerusalemu na ya kuweka kuhani mukubwa. Nero mwenye alikamata nafasi ya Mutawala Klaudio aliongezea Agripa maeneo ya Galilaya na Perea. Wakati Agripa alikutana na Paulo alikuwa Kaisaria pamoya na dada yake Bernike, mwenye alikuwa ameachana na bwana yake mufalme wa Kilikia.​—Mdo. 25:13.

Mu mwaka wa 66 K.K.Y., Agripa alijaribu kuzuia Wayahudi wasiasi Utawala wa Roma lakini Wayahudi walikatala kumusikiliza. Kwa hiyo, Agripa alijiunga na Waroma. Kisha Waroma kumaliza ule uasi, mutawala mupya Vaspasiani aliongezea Agripa maeneo ingine ili kumushukuru.

a Ona kisanduku “Gavana Muroma Porkio Festo.”

b “Kiti cha hukumu” ilikuwa nini? Ilikuwa fasi yenye kuinuka, kwenye kulikuwa kiti ya muamuzi. Ile ilifanya watu waone kama, maamuzi yake ya mwisho ilikuwa mazito na haingeweza kubadilika. Pilato aliikala ku kiti ya hukumu wakati alikuwa anachunguza mashitaka yenye watu walimushitaki Yesu.

c Ona kisanduku “Kuenda Kwenye Tribinali kwa Ajili ya Ibada ya Kweli Leo.”

d Ona kisanduku, “Mufalme Herode Agripa wa Pili.”

e Juu Paulo alikuwa Mukristo, alikubali kama Yesu njo Masiya. Wayahudi wenye walimukatala Yesu, walimuona Paulo kuwa muasi-imani.​—Mdo. 21:21, 27, 28.

f Mutu fulani mwenye elimu ya Biblia alisema hivi kuhusu maneno ya Paulo kwamba alikuwa anasafiri “katikati ya muchana:” “Kwa kawaida, watu wenye kusafiri walikuwa wanapumuzika katikati ya muchana kwa sababu ya joto yenye ilikuwa ile saa. Hawakupumuzika ikiwa tu walikuwa na jambo ya haraka sana ya kufanya. Ile inatusaidia kuelewa namna Paulo alikuwa ameazimia kabisa kutesa Wakristo.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine