SEHEMU YA 9
Dunia Itakuwa Paradiso Wakati Gani?
Mateso yenye kuwa mu dunia inaonyesha kama Ufalme wa Mungu uko karibu kutenda. Luka 21:10, 11; 2 Timoteo 3:1-5
Kuko mambo mingi sana yenye Biblia ilisema mbele ya wakati kama itatokea, na ile mambo iko inaonekana leo. Biblia ilisema kama watu watakuwa wenye kupenda feza, wenye hawatii ao kusikia wazazi wao, wakali, na wenye kupenda raha ao mambo ya kujifurahisha sana.
Tena, ilisema kama kutakuwa matetemeko makubwa ya inchi, vita, njaa, na magonjwa yenye kuenea sana. Ile mambo iko inaonekana leo.
Tena, Yesu alisema kama habari njema ya Ufalme itahubiriwa mu dunia yote.—Matayo 24:14.
Ufalme utamaliza mambo yote ya mubaya. 2 Petro 3:13
Hivi karibuni, Yehova ataua watu wabaya wote.
Shetani na pepo wake wachafu watapewa azabu ao malipizi.
Wale wenye wanamusikiliza Mungu wataokoka na kuingia mu dunia yenye haki, kwenye hakutakuwa tena woga, watu watapendana na kila mutu atatumainia mwenzake.