Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • fg somo 1 uli. 1-3
  • Kuko Habari Gani Njema?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kuko Habari Gani Njema?
  • Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kwa Nini Ujifunze Kutoka kwa Mungu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Mungu Ana Kusudi Gani Kuelekea Dunia?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Mungu Anapenda Dunia Ikuwe Namna Gani?
    Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Ona Habari Zaidi
Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
fg somo 1 uli. 1-3

SOMO LA 1

Kuko Habari Gani Njema?

1. Ni habari gani yenye inatoka kwa Mungu?

Watu wako na maisha yenye furaha ku dunia

Mungu anapenda watu wakuwe na maisha yenye furaha ku dunia. Mungu aliumba dunia na kila kitu chenye kuwa ku dunia juu anapenda watu. Hivi karibuni, Mungu atafanya kila mutu akuwe na maisha ya muzuri ku dunia yote. Atatosha mambo yenye kuletea watu mateso.​—Soma Yeremia 29:11.

Hakuna serikali ao guvernema yenye imeweza kumaliza mambo ya kuumizana ao kuuana, magonjwa, ao kifo. Lakini kuko habari njema. Hivi karibuni, Mungu atatosha serikali zote za watu na kuweka serikali yake nafasi ya serikali hizo. Wale wenye ile serikali itatawala watakuwa na amani na afya ya muzuri.​—Soma Isaya 25:8; 33:24; Danieli 2:44.

2. Juu ya nini watu wako na lazima ya kusikia ile habari njema leo?

Mateso itaisha wakati tu Mungu atatosha watu wabaya ku dunia. (Sefania 2:3) Atafanya vile wakati gani? Tangu zamani, Neno la Mungu lilisema juu ya hali zenye zinatesa watu leo. Mambo ya mubaya yenye inatokea ku dunia leo inaonyesha kama wakati wenye Mungu atamaliza mateso uko karibu.​—Soma 2 Timoteo 3:1-5.

3. Tunapaswa kufanya nini?

Tunapaswa kujifunza juu ya Mungu kupitia Neno lake, Biblia. Biblia iko kama barua yenye baba mwenye upendo alituandikia. Inatuonyesha mambo yenye tunapaswa kufanya ili tukuwe na maisha ya muzuri leo, na ili tupate uzima wa milele ku dunia wakati wenye kuja. Kwa kweli, pengine watu fulani hawatafurahi wakati wanakuona uko unajifunza Biblia. Lakini, kwa sababu Mungu anatupatia ahadi (ao, malako) kama tunaweza kuwa na wakati muzuri wenye kuja, usiache wengine wakuzuie kujifunza Biblia.​—Soma Mezali 29:25; Ufunuo 14:6, 7.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine