Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • fg somo 8 uli. 1-5
  • Juu ya Nini Mungu Anaacha Mambo ya Mubaya na Mateso Iendelee?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Juu ya Nini Mungu Anaacha Mambo ya Mubaya na Mateso Iendelee?
  • Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kwa Nini Mungu Anaruhusu Uovu na Kuteseka?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Juu ya Nini Kuko Mateso Mingi Sana?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Juu ya Nini Kuko Mateso na Mambo Mingi ya Mubaya?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
Ona Habari Zaidi
Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
fg somo 8 uli. 1-5

SOMO LA 8

Juu ya Nini Mungu Anaacha Mambo ya Mubaya na Mateso Iendelee?

1. Mambo ya mubaya ilianza namna gani?

1. Adamu anatazama tunda lililokatazwa; 2. Watawala fulani; 3. Picha za vita

Mungu ameacha watu watawale kwa wakati murefu ili ionekane wazi kama hawawezi kumaliza magumu ya watu

Mambo ya mubaya ilianza ku dunia wakati Shetani alisema uongo wa kwanza. Ku mwanzo, Shetani alikuwa malaika mukamilifu, lakini “hakusimama imara katika kweli.” (Yohana 8:44) Alipenda kuabudiwa, lakini ni Mungu tu njo anapaswa kuabudiwa. Shetani alimudanganya Eva, mwanamuke wa kwanza, na akamuchochea amutii ao amusikie yeye kuliko kumutii Mungu. Adamu alimusikiliza bibi yake, Eva, naye pia akakosa kumutii Mungu. Uamuzi wa Adamu ulileta mateso na kifo.​—Soma Mwanzo 3:1-6, 19.

Wakati Shetani alimuchochea Eva asimutii Mungu, alianzisha upinzani juu ya haki ya Mungu ya kutawala. Watu wengi wamejiunga na Shetani katika upinzani wake, wanakataa Mungu asikuwe Mutawala wao. Kwa hiyo, Shetani amekuwa “mutawala wa ulimwengu.”​—Soma Yohana 14:30; 1 Yohana 5:19.

2. Ku mwanzo, kulikuwa kiumbe fulani chenye hakikukuwa kikamilifu?

Hapana, kazi zote za Mungu ni kamilifu. Malaika na watu wenye Mungu aliumba walikuwa na uwezo wa kumutii kwa ukamilifu. (Kumbukumbu la Torati 32:4, 5) Wakati Mungu alituumba, alitupatia uhuru wa kuchagua kufanya mambo ya muzuri ao mambo ya mubaya. Uhuru huo unatupatia nafasi ya kuonyesha kama tunamupenda Mungu.​—Soma Yakobo 1:13-15; 1 Yohana 5:3.

3. Juu ya nini Mungu ameacha mateso iendelee mupaka leo?

Kuanzia wakati upinzani ulitokea mu Edeni, Yehova ameacha haki yake ya kutawala ipingwe. Juu ya nini? Juu ya kuonyesha kama nguvu yenye watu wanafanya ili kujitawala wenyewe bila musaada wa Mungu, haiwezi kuleta matokeo ya muzuri. (Muhubiri 7:29; 8:9) Kisha miaka 6 000 yenye watu wamejitawala wenyewe, jambo hilo limeonekana wazi. Serikali ao guvernema za watu zimeshindwa kumaliza vita, matendo ya kuvunja sheria, ukosefu wa haki, ao magonjwa.​—Soma Yeremia 10:23; Waroma 9:17.

Tofauti na utatawala wa watu, utawala wa Mungu unaletea faida wale wenye kuukubali. (Isaya 48:17, 18) Hivi karibuni, Yehova ataharibu serikali zote za watu. Wale tu wenye wanaitika Mungu awatawale njo wenye wataishi ku dunia.​—Isaya 11:9. Soma Danieli 2:44.

Angalia video Sababu Gani Mungu Anaacha Mateso?

4. Uvumilivu wa Mungu unatupatia nafasi ya kufanya nini?

Shetani alisema kama watu wanamutumikia Yehova juu ya faida fulani. Je, unapenda kuonyesha kama Shetani ni musema-uongo? Unaweza kufanya vile! Uvumilivu wa Mungu unatupatia sisi wote nafasi ya kuonyesha ikiwa tunaunga mukono utawala wa Mungu ao utawala wa watu. Namna yetu ya kuishi njo yenye inaonyesha kama tunaunga mukono utawala wa Mungu ao hapana.​—Soma Yobu 1:8-12; Mezali 27:11.

5. Tunaweza kufanya nini ili kuonyesha kama tunamuchagua Mungu akuwe Mutawala wetu?

Watu wanaojifunza Biblia

Maamuzi yenye tunakamata inaonyesha ikiwa tunataka Mungu akuwe mutawala wetu ao hapana

Tunaweza kuonyesha kama tunamuchagua Mungu akuwe Mutawala wetu wakati tunatafuta dini ya kweli yenye mafundisho yake inatoka mu Biblia, Neno la Mungu, na kujiunga na dini hiyo. (Yohana 4:23) Tutaonyesha kama Shetani haiko mutawala wetu wakati tunakataa kujiingiza mu mambo ya politike na vita, kama vile Yesu alifanya.​—Soma Yohana 17:14.

Shetani anatumia nguvu yake ili kuchochea watu wafanye matendo machafu na yenye kuumiza wengine. Wakati tunaepuka ile matendo, marafiki wetu na watu wa jamaa yetu wanaweza kutuchekelea ao kutupinga. (1 Petro 4:3, 4) Kwa hiyo, tunapaswa kukamata uamuzi. Je, tutajiunga na watu wenye wanamupenda Mungu? Tutatii sheria zake zenye hekima na zenye upendo? Kama tunafanya vile, tutaonyesha kabisa kama Shetani alisema uongo wakati alisema kama hakuna mutu mwenye anaweza kubakia muaminifu kwa Mungu wakati ni nguvu kufanya vile.​—Soma 1 Wakorinto 6:9, 10; 15:33.

Juu Mungu anapenda watu, hilo linatufanya tuamini kabisa kama siku fulani mambo ya mubaya na mateso itaisha. Wale wenye wanaamini kama utawala wa Mungu njo utawala wenye unafaa na wanamuitika akuwe Mutawala wao wataishi ku dunia milele.​—Soma Yohana 3:16.

Ili kupata habari zaidi, ona sura ya 11 ya kitabu Biblia Inatufundisha Nini?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine