Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • fg somo 10 uli. 1-4
  • Namna Gani Unaweza Kujua Dini ya Kweli?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna Gani Unaweza Kujua Dini ya Kweli?
  • Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Unaweza Kuitambua Ibada ya Kweli Jinsi Gani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Dini Inayokubaliwa na Mungu
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Namna Gani Unaweza Kuipata Ile Dini ya Kweli?
    Mungu Anataka Nini Kwetu?
  • Njia ya Muzuri ya Kumuabudu Mungu
    Biblia Inatufundisha Nini?
Ona Habari Zaidi
Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
fg somo 10 uli. 1-4

SOMO LA 10

Namna Gani Unaweza Kujua Dini ya Kweli?

1. Kuko dini moja tu ya kweli?

Mafundisho ya Yesu

“Mufanye angalisho na manabii wa uongo.”​—MATAYO 7:15.

Yesu alifundisha wanafunzi wake dini moja tu, dini ya kweli. Alifananisha dini hiyo na barabara yenye kuongoza kwenye uzima wa milele. Yesu alisema kama ni ‘watu kidogo ndio wanapata’ barabara hiyo. (Matayo 7:14) Mungu anaitika tu dini yenye mafundisho yake inatoka mu Biblia. Waabudu wote wa kweli wako na imani moja.​—Soma Yohana 4:23, 24; 14:6; Waefeso 4:4, 5.

Angalia video Mungu Anakubali Dini Zote?

2. Yesu alisema nini juu ya Wakristo wa uongo?

Kiongozi mumoja wa dini akifundisha kanisani. Baadaye anabariki askari wanaoenda kwenye vita.

“Wanatangaza mbele ya watu wote kwamba wanamujua Mungu, lakini wanamukana kupitia matendo yao.”​—TITO 1:16.

Yesu alionya ao alitoa angalisho kama manabii wa uongo wangeharibisha Ukristo wa kweli. Kwa inje, manabii hao wa uongo wanaonekana kuwa waabudu wa kweli. Makanisa yao inajiita kuwa ya Kikristo. Lakini unaweza kujua kama hawako Wakristo wa kweli. Namna gani? Dini ya kweli tu njo inatokeza Wakristo wa kweli wenye kuwa na sifa na matendo ya muzuri yenye watu wanaweza kuona waziwazi.​—Soma Matayo 7:13-23.

3. Namna gani unaweza kujua Wakristo wa kweli?

Tuzungumuzie mambo tano yenye kufuata yenye inasaidia kujua Wakristo wa kweli:

  • Wakristo wa kweli wanaona Biblia kuwa Neno la Mungu na wanaiheshimia kabisa. Wanajikaza kutumia kanuni za Biblia mu maisha yao. Kwa hiyo, dini ya kweli haiko kama dini zenye zinafundisha mawazo ya wanadamu. (Matayo 15:7-9) Wakristo wa kweli wanatumia mu maisha yao mambo yenye wanafundisha wengine.​—Soma Yohana 17:17; 2 Timoteo 3:16, 17.

  • Mukristo anatoa hotuba. Baadaye anahubiria watu kuhusu Ufalme wa Mungu, anasaidia watu waliopigwa na musiba, anasaidia mutu mwenye kuzeeka.

    Wanafunzi wa kweli wa Yesu wanaheshimia jina la Mungu, Yehova. Yesu aliheshimia jina la Mungu kwa kujulisha watu jina hilo. Alisaidia watu wamujue Mungu na aliwafundisha wasali jina la Mungu litakaswe. (Matayo 6:9) Mahali kwenye unaishi, ni dini gani yenye inajulisha watu jina la Mungu?​—Soma Yohana 17:26; Waroma 10:13, 14.

  • Wakristo wa kweli wanahubiri juu ya Ufalme wa Mungu. Mungu alimutuma Yesu ili ahubiri habari njema ya Ufalme. Ufalme wa Mungu tu njo utamaliza magumu ya wanadamu. Yesu aliendelea kuzungumuza juu ya Ufalme huo mupaka siku alikufa. (Luka 4:43; 8:1; 23:42, 43) Alisema kama wanafunzi wake wangehubiri juu ya Ufalme huo. Kama mutu fulani anakuja kuzungumuza na wewe juu ya Ufalme wa Mungu, utawaza iko wa dini gani?​—Soma Matayo 24:14.

  • Wanafunzi wa Yesu hawako sehemu ya ulimwengu huu mubaya. Unaweza kuwajua kwa sababu hawajiingize mu mambo ya politike ao mambo kama vile maandamano, ao ugomvi kati ya watu. (Yohana 17:16; 18:36) Tena, hawaige ao kufuata matendo na mawazo ya mubaya ya watu wa ulimwengu huu.​—Soma Yakobo 4:4.

  • Wakristo wa kweli wanapendana kabisa. Neno la Mungu linawafundisha kuheshimia watu wa kila kabila. Hata kama mara mingi dini za uongo zimeunga kabisa mukono vita kati ya mataifa, Wakristo wa kweli wanakataa kufanya vile. (Mika 4:1-3) Lakini, Wakristo wa kweli wanafurahia kutumia wakati wao na mali yao ili kusaidia watu wengine na kuwatia moyo.​—Soma Yohana 13:34, 35; 1 Yohana 4:20.

4. Unaweza kujua dini ya kweli?

Ni dini gani yenye mafundisho yake yote inatoka mu Neno la Mungu? Ni dini gani yenye inaheshimiaka jina la Mungu? Na ni dini gani yenye inatangaziaka watu kama Ufalme wa Mungu tu njo utamaliza magumu ya wanadamu? Ni dini gani yenye waabudu wake wanapendanaka na wanakataa kujiingiza mu mambo ya vita? Unawaza nini?​—Soma 1 Yohana 3:10-12.

Ili kupata habari zaidi, ona sura ya 15 ya kitabu Biblia Inatufundisha Nini?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine