Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • fg somo 15 uli. 1-4
  • Juu ya Nini Unapaswa Kuendelea Kujifunza Biblia?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Juu ya Nini Unapaswa Kuendelea Kujifunza Biblia?
  • Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Unaweza Kumkaribia Mungu Jinsi Gani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Kuwa Rafiki ya Mungu Ndiyo Njia ya Muzuri Zaidi ya Maisha
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Unaweza Kufanya Nini ili Umukaribie Mungu?
    Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
  • “Kumukaribia Mungu Ni Jambo la Muzuri” Kwetu!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
Ona Habari Zaidi
Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
fg somo 15 uli. 1-4

SOMO LA 15

Juu ya Nini Unapaswa Kuendelea Kujifunza Biblia?

1. Utapata faida gani kama unaendelea kujifunza Biblia?

Wanawake wawili wanaojifunza Biblia wakati wa mapumuziko mahali pa kazi

Kwa kweli, mafundisho ya musingi ya Biblia yenye umejifunza mu broshua hii, imekufanya umupende Yehova zaidi. Ni lazima uendelee kujifunza ili upendo wako kwa Yehova uendelee kuwa wenye nguvu. (1 Petro 2:2) Ili upate uzima wa milele, ni lazima uendelee kumukaribia Mungu kwa kujifunza Neno lake.​—Soma Yohana 17:3; Yuda 21.

Kama unaendelea kujifunza mambo mingi juu ya Mungu, imani yako itakuwa yenye nguvu zaidi. Imani hiyo itakusaidia ufanye mambo yenye kumufurahisha Mungu. (Waebrania 11:1, 6) Itakuchochea utubu na ufanye mabadiliko ya muzuri mu maisha yako.​—Soma Matendo 3:19.

2. Utafanya nini ili kusaidia wengine wapate faida kupitia mambo yenye umejifunza juu ya Mungu?

Mwanamuke anasali kwa Mungu

Unaweza kuwa na urafiki muzuri pamoja na Yehova

Kwa kawaida, kama mutu anapata habari njema anaambiaka wengine ile habari. Kwa hiyo, wewe pia hautakosa kuambia wengine mambo yenye umejifunza. Wakati unaendelea kujifunza Biblia, utajua namna ya kuitumia ili kuelezea wengine mambo yenye unaamini juu ya Yehova na kuwaambia juu ya habari njema.​—Soma Waroma 10:13-15.

Watu wengi wanaanza kwanza kuzungumuza na marafiki wao ao watu wa jamaa yao juu ya habari njema. Ufanye vile kwa heshima. Kuliko kuwaambia kama dini yao ni ya uongo, uwaambie juu ya ahadi (ao malako) za Mungu. Tena, ukumbuke kama mara mingi tabia yako ya muzuri njo yenye inapendeza watu kuliko mambo yenye unasema.​—Soma 2 Timoteo 2:24, 25.

3. Unaweza kuwa na urafiki gani pamoja na Mungu?

Kujifunza Neno la Mungu kutakusaidia ufanye maendeleo. Kisha, unaweza kuwa na urafiki muzuri sana pamoja na Yehova. Kwa kweli, Mungu anaweza kuitika uingie mu familia yake.​—Soma 2 Wakorinto 6:18.

4. Unaweza kufanya nini ili uendelee kufanya maendeleo?

Unaweza kufanya maendeleo kama unaendelea kujifunza Neno la Mungu. (Waebrania 5:13, 14) Omba Shahidi wa Yehova akufundishe Biblia kwa kutumia kitabu Biblia Inatufundisha Nini? Kama unaendelea kujifunza Neno la Mungu, utakuwa na furaha zaidi mu maisha yako.​—Soma Zaburi 1:1-3; 73:27, 28.

Mashahidi wa Yehova wanaomba bibi na bwana wajifunze Biblia

Habari njema inatoka kwa Yehova, Mungu mwenye furaha. Unaweza kumukaribia zaidi kwa kujiunga na watu wake. (Waebrania 10:24, 25) Kama unaendelea kujikaza ili kumufurahisha Yehova, utafikia kupata uzima wa kwelikweli, ni kusema, uzima wa milele. Kwa kweli, kumukaribia Yehova njo jambo la muzuri zaidi lenye unaweza kufanya mu maisha yako.​—Soma 1 Timoteo 1:11; 6:19.

Ili kupata habari zaidi, ona sura ya 18 ya kitabu Biblia Inatufundisha Nini?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine