Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • yc somo 3 uku. 8-9
  • Rahabu Alimuamini Yehova

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Rahabu Alimuamini Yehova
  • Uwafundishe Watoto Wako
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Rahabu Alificha Wapelelezi
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • ‘Alitangazwa Kuwa Muadilifu kwa Matendo’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Uwafundishe Watoto Wako
yc somo 3 uku. 8-9
Rahabu anafika ku sehemu ya juu ya nyumba kwenye wapelelezi wanajificha

SOMO LA 3

Rahabu Alimuamini Yehova

Wazia tunaishi katika muji wa Yeriko. Muji huo unapatikana mu inchi ya Kanaani. Watu wa muji huo hawamuamini Yehova. Lakini katika muji huo kuko mwanamuke anayeitwa Rahabu.

Wakati Rahabu alikuwa angali mutoto mudogo alisikia hadisi juu ya Musa. Alisikia vile Musa aligawanya Bahari Nyekundu. Alisikia pia vile Musa aliwaondoa Waisraeli katika inchi ya Misri. Tena, Rahabu alisikia vile Yehova aliwasaidia Waisraeli kushinda maadui zao katika vita mbalimbali. Sasa, Rahabu anasikia kama Waisraeli wako karibu na Yeriko!

Rahabu anawaficha wapelelezi juu alimuamini Yehova

Siku moja mangaribi, Waisraeli wawili walikuja mu muji wa Yeriko ili kupeleleza muji huo. Nao wakafika kwa Rahabu. Naye Rahabu akawakaribisha mu nyumba yake. Wakati wa usiku, watu wanamuambia mufalme wa Yeriko kama wapelelezi wamekwisha kuingia mu muji, na wako kwa Rahabu. Kwa hiyo, mufalme anatuma wanaume ili kuwakamata wapelelezi hao. Rahabu anawaficha wapelelezi katika sehemu ya juu ya nyumba yake. Kisha Rahabu anawaambia hivi wanaume wenye mufalme alituma: ‘Ni kweli wapelelezi walikuwa hapa, lakini wamekwisha kuondoka katika muji. Mukiwafuata sasa, munaweza kuwakamata!’ Unajua ni juu ya nini Rahabu anawaficha wapelelezi hao?— Ni juu Rahabu anamuamini Yehova na anajua kama Yehova atawapatia Waisraeli inchi ya Kanaani.

Wapelelezi hao wanataka kuenda. Lakini mbele ya kuenda wanamuambia Rahabu hivi: ‘Weye na wazazi wako na ndugu zako mutaokoka wakati Yeriko itaharibiwa.’ Unajua mambo yenye wapelelezi wanamuomba Rahabu afanye?— Wanamuambia hivi: ‘Kamata kamba hii ya rangi nyekundu na uifunge ku dirisha ya nyumba yako. Ukifanya hivyo, kila mutu mwenye iko mu nyumba yako hatakufa.’ Rahabu alifanya kabisakabisa kama vile wapelelezi walimuambia. Unajua ni nini ilitokea kisha wapelelezi kuenda?—

Kamba ya rangi nyekundu iko ku dirisha ya nyumba ya Rahabu ku ukuta wa Yeriko

Yehova aliokoa Rahabu na wazazi wake na ndugu zake

Kisha siku kidogo, Waisraeli wanafika Yeriko. Wanatembea kwa kuzunguka muji huo bila kufanya fujo. Wanazunguka muji mara moja kila siku kwa siku sita. Lakini siku ya saba wanazunguka muji mara saba. Kisha wote wanapiga kelele kwa sauti kubwa. Yehova akafanya ukuta wenye kuzunguka muji wa Yeriko ubomoke na kuanguka chini. Lakini nyumba yenye ilikuwa na kamba ya rangi nyekundu ku dirisha haikubomoka hata kidogo! Unaona nyumba hiyo ku hii picha?— Rahabu na wazazi wake na ndugu zake wanaokoka!

Mufano wa Rahabu unakufundisha nini?— Rahabu alimuamini Yehova juu alisikia mambo ya ajabu yenye Yehova alifanya. Weye pia unajifunza mambo mingi ya ajabu yenye Yehova alifanya. Unamuamini Yehova kama vile Rahabu?— Tunajua kama unafanya vile!

SOMA KATIKA BIBLIA YAKO

  • Yoshua 2:1-24; 6:1-5, 14, 15, 20-25

  • Waebrania 11:31

MAULIZO:

  • Ni hadisi gani Rahabu alisikia wakati alikuwa angali mutoto mudogo?

  • Rahabu alifanya nini ili kuwasaidia wapelelezi? Ni juu ya nini aliwasaidia?

  • Wapelelezi hao walimuambia Rahabu nini?

  • Mufano wa Rahabu unakufundisha nini?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine