Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • yc somo 9 uku. 20-21
  • Yeremia Hakuacha Kuwatangazia Watu Habari ya Yehova

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yeremia Hakuacha Kuwatangazia Watu Habari ya Yehova
  • Uwafundishe Watoto Wako
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Yehova Anatuma Yeremia Aende Kuhubiri
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Kaa Macho, Kama Yeremia Alivyofanya
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Ukuwe na Ujasiri Kama Yeremia
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2017
Uwafundishe Watoto Wako
yc somo 9 uku. 20-21

SOMO LA 9

Yeremia Hakuacha Kuwatangazia Watu Habari ya Yehova

Yeremia anazungukwa na watu wengi wenye kukasirika

Watu hawa wanamusirikia Yeremia juu ya nini?

Yeremia iko anatoshwa mu shimo ndefu lenye kuwa na matope mingi

Yehova alimuokoa Yeremia

Wakati tunawatangazia watu habari ya Yehova, kuko wakati wanatuchekelea ao kutusirikia. Ile inaweza kutufanya tuache kuwatangazia watu habari ya Mungu. Kuko wakati weye pia umejisikia vile?— Katika Biblia muko hadisi ya kijana mumoja mwenye alimupenda Yehova. Kijana ule anaitwa Yeremia. Wakati fulani Yeremia alitaka kuacha kuwatangazia watu habari ya Yehova. Ni vizuri tuzungumuze sasa juu ya kijana Yeremia.

Wakati Yeremia alikuwa angali kijana tu, Yehova alimuambia kama anapashwa kuwaelezea watu waache kufanya matendo mabaya. Yeremia alijisikia kama hataweza kufanya ile kazi. Kwa hiyo, aliogopa kabisa. Yeremia alimuambia Yehova hivi: ‘Sijue kabisa kusema. Miye ningali mutoto tu.’ Lakini Yehova akamuambia hivi: ‘Usiogope Yeremia. Miye nitakusaidia.’

Wakati Yeremia alisikia vile, akaanza kuwatangazia watu habari ya Yehova. Aliwaambia watu hivi: ‘Kama hamubadilishe matendo yenu, Yehova atawaazibu.’ Unawaza watu walibadilisha matendo yao kama vile Yeremia aliwaambia?— Kuliko kubadilisha matendo yao, watu walimuchekelea Yeremia na kumusirikia sana. Wengine hata walitaka kumuua! Kwa hiyo, unawaza Yeremia alijisikia namna gani?— Yeremia aliogopa, na alianza kusema: ‘Sitawatangazia watu tena habari ya Yehova.’ Lakini, unawaza aliacha kabisa kuwatangazia watu habari ya Yehova?— Hakuacha. Yeremia alimupenda sana Yehova, kwa hiyo, haingewezekana aache kuwatangazia watu habari ya Yehova. Na Yehova aliendelea kumulinda Yeremia, juu Yeremia hakuacha kuwatangazia watu habari ya Yehova.

Kwa mufano, siku moja, wanaume fulani wabaya walimutupa Yeremia mu shimo yenye kuwa na matope mingi. Katika ile shimo, Yeremia hakuwa na chakula ao maji. Wale wanaume walimuacha Yeremia katika ile shimo ili akufie mule. Lakini, Yehova alimusaidia, na Yeremia hakukufa!

Mufano wa Yeremia unakufundisha nini?— Hata kama wakati fulani Yeremia aliogopa, hakuacha kuwatangazia watu habari ya Yehova. Weye pia watu wanaweza kukuchekelea ao kukusirikia wakati unawaambia habari ya Yehova. Unaweza kusikia haya na unaweza hata kuogopa. Lakini usiache hata kidogo kuwaambia watu habari ya Yehova. Kila siku, Yehova atakusaidia kama vile alimusaidia Yeremia.

SOMA KATIKA BIBLIA YAKO

  • Yeremia 1:4-8; 20:7-9; 26:8-19, 24; 38:6-13

MAULIZO:

  • Yehova alimuambia Yeremia afanye nini?

  • Yeremia alitaka kuacha kuwatangazia watu habari ya Yehova juu ya nini?

  • Namna gani Yehova alimusaidia Yeremia?

  • Mufano wa Yeremia unakufundisha nini?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine