Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • yc somo 11 uku. 24-25
  • Wanaume Wenye Waliandika Juu ya Maisha ya Yesu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Wanaume Wenye Waliandika Juu ya Maisha ya Yesu
  • Uwafundishe Watoto Wako
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Bwana Wake Alimufundisha Kusamehe
    Tuige Imani Yao
  • “Watu Wenye Hawana Elimu na Watu wa Kawaida”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • Alibaki Mushikamanifu Ijapokuwa Majaribu
    Tuige Imani Yao
  • Yesu Kristo Ni Nani?
    Biblia Inatufundisha Nini?
Ona Habari Zaidi
Uwafundishe Watoto Wako
yc somo 11 uku. 24-25
Wanaume wenye waliandika juu ya maisha ya Yesu—Matayo, Marko, Luka, Yohana, Petro, Yakobo, Yuda, na Paulo

SOMO LA 11

Wanaume Wenye Waliandika Juu ya Maisha ya Yesu

Unawajua wanaume wenye kuwa ku picha hii?— Ni Matayo, Marko, Luka, Yohana, Petro, Yakobo, Yuda na Paulo. Waliishi wakati moja na Yesu, na waliandika juu ya maisha ya Yesu. Ni vizuri tuzungumuze sasa juu ya wanaume hao.

Wanaume hawa walifanya nini?

Kati ya wanaume hao, watatu walikuwa mitume wenye walikuwa wanahubiri pamoja na Yesu. Unawajua wale mitume watatu?— Ni Matayo, Yohana na Petro. Mutume Matayo na mutume Yohana walimujua Yesu vizuri sana. Na kila mumoja wao aliandika kitabu chenye kuzungumuza juu ya maisha ya Yesu. Mutume Yohana pia aliandika kitabu chenye kuitwa Ufunuo na aliandika pia barua tatu zenye kuitwa Yohana wa Kwanza, Yohana wa Pili na Yohana wa Tatu. Mutume Petro, yeye aliandika barua mbili zenye kuitwa Petro wa Kwanza na Petro wa Pili. Katika barua yake ya pili, Petro aliandika kama wakati fulani Yehova alisema maneno fulani juu ya Yesu. Kutokea mbinguni, Yehova alisema hivi: ‘Huyu ni mutoto wangu. Ninamupenda, na ninajivunia yeye.’

Wanaume wengine wenye kuonekana ku picha hii, nao pia waliandika vitabu vyenye kutufundisha juu ya Yesu. Tukamate mufano wa Marko. Inaonekana kama wakati Yesu alikamatwa, Marko alikuwa pale na aliona mambo yote yenye ilitendeka. Mwengine ni Luka. Yeye alikuwa muganga na inaonekana alikuwa Mukristo kisha Yesu kukufa.

Wanaume wengine wawili wenye unaona walikuwa ndugu za Yesu, ni kusema, wadogo yake. Wao pia waliandika vitabu fulani vya Biblia. Unajua majina yao?— Wanaitwa Yakobo na Yuda. Wakati Yesu alikuwa duniani hawakumuamini. Waliwaza kama Yesu ni mwendawazimu ao ni mwenye kupoteza akili. Lakini kisha walimuamini Yesu na wakakuwa Wakristo.

Huyu mwengine unaona ni Paulo. Yeye pia aliandika vitabu fulani vya Biblia. Mbele ya Paulo kuwa Mukristo, aliitwa Saulo. Aliwachukia Wakristo na aliwatesa sana. Unajua ni nini ilimufanya Paulo abadilike na kuwa Mukristo?— Mambo yalikuwa hivi: Siku moja, Paulo alifanya safari. Wakati alikuwa katika safari hiyo, mara moja alisikia mutu fulani anasema naye. Sauti ile ilitoka mbinguni. Na ile sauti ilikuwa sauti ya Yesu! Yesu alimuuliza Paulo: ‘Juu ya nini unawatesa sana wale wenye kuniamini?’ Kisha, Paulo alibadilika na akakuwa Mukristo. Katika Biblia muko vitabu 14 vyenye Paulo aliandika. Vile vitabu vinaanza na kitabu cha Waroma mupaka kitabu cha Waebrania.

Kila siku tunasoma Biblia, si vile?— Kwa kusoma Biblia, tunajifunza mambo mengi juu ya Yesu. Utapenda kabisa kujifunza mambo mengi juu ya Yesu?—

SOMA KATIKA BIBLIA YAKO

  • 2 Petro 1:16-18

  • Marko 3:21; 14:51

  • Yuda 1

  • Matendo 9:1-18

MAULIZO:

  • Taja majina ya mitume wa Yesu wenye waliandika juu ya maisha yake.

  • Taja majina ya ndugu wawili wa Yesu wenye waliandika vitabu fulani vya Biblia.

  • Ni nini ilimufanya Paulo abadilike na kuwa Mukristo?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine