SOMO LA 4
Namna ya Kutumia Feza Vizuri
‘Kwa shauri mipango yenyewe inafanywa imara.’—Methali 20:18
Sisi wote tunahitaji feza ili kutosheleza mahitaji ya familia yetu. (Methali 30:8) Kwa vyovyote, “feza ni ulinzi.” (Mhubiri 7:12) Inaweza kuwa vigumu kuzungumuzia feza kati yenu wawili, lakini musiache feza zitokeze matatizo katika ndoa yenu. (Waefeso 4:32) Ni lazima bibi na bwana watumainiane na kuungana mukono wakati wanaamua namna watatumia feza zao.
1 MUPANGE MAMBO VIZURI
MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: ‘Ni nani kati yenu anayetaka kujenga munara ambaye haketi kwanza na kuhesabu garama, ili aone kama ana kiasi cha kutosha kuukamilisha?’ (Luka 14:28) Ni vizuri muamue pamoja namna mutatumia feza zenu. (Amosi 3:3) Muamue ni vitu gani munapaswa kuuza na kiasi cha feza ambacho munaweza kutumia. (Methali 31:16) Hamupaswe kuuza kitu fulani kwa sababu tu muna feza za kukiuza. Muepuke madeni. Mutumie tu feza mulizo nazo.—Methali 21:5; 22:7.
MAMBO YA KUFANYA:
Ikiwa mwishoni mwa mwezi munaweka kiasi fulani cha feza, muamue pamoja namna mutazitumia
Ikiwa munapungukiwa feza, muamue kupunguza garama zenu. Kwa mufano, munaweza kujipikia chakula kuliko kuuza chakula kwenye mukahawa oa restora
2 UWE WAZI NA UONE MAMBO NAMNA YALIVYO
MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: ‘Fanya mupango wa unyoofu, si machoni pa Yehova tu, bali pia machoni pa wanadamu.’ (2 Wakorintho 8:21) Umuambie waziwazi bibi ao bwana yako feza unazopokea na zile unazotumia.
Usikose kumuelezea mwenzako wakati unataka kufanya maamuzi makubwa kuhusiana na feza. (Methali 13:10) Kuzungumuza pamoja kuhusu mambo ya feza kutawasaidia muendeleze umoja katika ndoa yenu. Usione feza unazopata kuwa zako, lakini uzione kuwa za familia.—1 Timotheo 5:8.
MAMBO YA KUFANYA:
Mukubaliane kuhusu kiasi cha feza ambacho kila mumoja wenu anaweza kutumia bila kumuuliza mwengine
Musingoje mupaka matatizo yatokee ili muzungumuzie mambo ya feza