Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • hf sehemu 4 uku. 12-14
  • Namna ya Kutumia Feza Vizuri

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna ya Kutumia Feza Vizuri
  • Familia Yenu Inaweza Kuwa na Furaha
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • 1 MUPANGE MAMBO VIZURI
  • 2 UWE WAZI NA UONE MAMBO NAMNA YALIVYO
  • Namna ya Kuwa na Mawazo ya Muzuri Juu ya Feza
    Amuka!—2015
  • Feza
    Amuka!—2014
  • Makuta Njo Chanzo ya Mambo Yote ya Mubaya?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
Familia Yenu Inaweza Kuwa na Furaha
hf sehemu 4 uku. 12-14
Bibi na bwana wanazungumuzia kwa uangalifu namna ya kutumia feza zao

SOMO LA 4

Namna ya Kutumia Feza Vizuri

‘Kwa shauri mipango yenyewe inafanywa imara.’​—Methali 20:18

Sisi wote tunahitaji feza ili kutosheleza mahitaji ya familia yetu. (Methali 30:8) Kwa vyovyote, “feza ni ulinzi.” (Mhubiri 7:12) Inaweza kuwa vigumu kuzungumuzia feza kati yenu wawili, lakini musiache feza zitokeze matatizo katika ndoa yenu. (Waefeso 4:32) Ni lazima bibi na bwana watumainiane na kuungana mukono wakati wanaamua namna watatumia feza zao.

1 MUPANGE MAMBO VIZURI

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: ‘Ni nani kati yenu anayetaka kujenga munara ambaye haketi kwanza na kuhesabu garama, ili aone kama ana kiasi cha kutosha kuukamilisha?’ (Luka 14:28) Ni vizuri muamue pamoja namna mutatumia feza zenu. (Amosi 3:3) Muamue ni vitu gani munapaswa kuuza na kiasi cha feza ambacho munaweza kutumia. (Methali 31:16) Hamupaswe kuuza kitu fulani kwa sababu tu muna feza za kukiuza. Muepuke madeni. Mutumie tu feza mulizo nazo.​—Methali 21:5; 22:7.

MAMBO YA KUFANYA:

  • Ikiwa mwishoni mwa mwezi munaweka kiasi fulani cha feza, muamue pamoja namna mutazitumia

  • Ikiwa munapungukiwa feza, muamue kupunguza garama zenu. Kwa mufano, munaweza kujipikia chakula kuliko kuuza chakula kwenye mukahawa oa restora

Bibi na bwana wanafikiria vitu vya kununua

2 UWE WAZI NA UONE MAMBO NAMNA YALIVYO

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: ‘Fanya mupango wa unyoofu, si machoni pa Yehova tu, bali pia machoni pa wanadamu.’ (2 Wakorintho 8:21) Umuambie waziwazi bibi ao bwana yako feza unazopokea na zile unazotumia.

Usikose kumuelezea mwenzako wakati unataka kufanya maamuzi makubwa kuhusiana na feza. (Methali 13:10) Kuzungumuza pamoja kuhusu mambo ya feza kutawasaidia muendeleze umoja katika ndoa yenu. Usione feza unazopata kuwa zako, lakini uzione kuwa za familia.​—1 Timotheo 5:8.

Bibi na bwana wakiwa kwenye boutique wanatazama liste ya vitu vya kununua

MAMBO YA KUFANYA:

  • Mukubaliane kuhusu kiasi cha feza ambacho kila mumoja wenu anaweza kutumia bila kumuuliza mwengine

  • Musingoje mupaka matatizo yatokee ili muzungumuzie mambo ya feza

MAWAZO YENU JUU YA FEZA

Hata kama feza ni za lazima, musiache ziharibu ndoa yenu ao kuwaletea mahangaiko. (Matayo 6:25-34) Si lazima muwe na feza nyingi ili kufurahia maisha. Biblia inasema hivi: ‘Mujilinde na kila namna ya tamaa.’ (Luka 12:15) Hakuna kitu ambacho feza zinaweza kuuza ambacho ni cha maana zaidi kuliko ndoa yenu. Kwa hiyo, mutosheke na feza mulizo nazo, na musipuuze hata kidogo uhusiano wenu na Mungu. Mukifanya hivyo, familia yenu itakuwa yenye furaha, na mutakubaliwa na Yehova.​—Waebrania 13:5.

JIULIZE . . .

  • Tukiwa familia, tunaweza kufanya nini ili kuepuka madeni?

  • Ni siku gani mimi na bibi ao bwana yangu tulizungumuza kwa mara ya mwisho kuhusu namna tunaweza kutumia feza zetu?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine