Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • hf sehemu 7 uku. 22-25
  • Namna ya Kumufundisha Mutoto Wako

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna ya Kumufundisha Mutoto Wako
  • Familia Yenu Inaweza Kuwa na Furaha
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • 1 FANYA WATOTO WAKO WASIOGOPE KUZUNGUMUZA NA WEWE
  • 2 TAFUTA KUELEWA WANATAKA KUSEMA NINI
  • 3 MUWE NA UMOJA
  • 4 PANGA MAMBO
  • Uzoeze Mutoto Wako Amutumikie Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Unaweza Kufanya Nini Juu Familia Yako Ikuwe na Furaha?​—Sehemu ya 2
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Wazazi, Musaidie Watoto Wenu Wamupende Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
Familia Yenu Inaweza Kuwa na Furaha
hf sehemu 7 uku. 22-25
Baba na mutoto wanatengeneza kinga pamoja

SOMO LA 7

Namna ya Kumufundisha Mutoto Wako

“Maneno haya ninayokuamuru leo lazima yawe moyoni mwako; nawe uyakazie kwa mwana wako.”​—Kumbukumbu la Torati 6:6, 7

Wakati Yehova alianzisha familia, aliwapatia wazazi daraka la kuongoza watoto wao. (Wakolosai 3:20) Wewe muzazi una daraka la kumufundisha mutoto wako kumupenda Yehova na kumusaidia akomae na kuchukua mambo kwa uzito. (2 Timotheo 1:5; 3:15) Unapaswa pia kutafuta kujua mambo yaliyo katika moyo wa kijana ao binti yako. Bila shaka, mufano wako ni wa maana sana. Utamufundisha vizuri mutoto wako Neno la Yehova ikiwa wewe kwanza unaliweka katika moyo wako.​—Zaburi 40:8.

1 FANYA WATOTO WAKO WASIOGOPE KUZUNGUMUZA NA WEWE

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: ‘Uwe mwepesi kuhusu kusikia, si mwepesi wa kusema.’ (Yakobo 1:19) Unapenda watoto wako wajisikie huru kuzungumuza na wewe. Watoto wako wanapaswa kujua kwamba uko tayari kuwasikiliza wakati wanataka kuzungumuza na wewe. Fanya nyumba yako iwe mahali penye amani, hilo litawafanya wasiogope kujieleza. (Yakobo 3:18) Ikiwa wanaona kwamba utakuwa mukali ao mwenye kuwalaumu-laumu, wanaweza kuogopa kujieleza. Uwe muvumilivu, na kila mara uwaonyeshe kwamba unawapenda.​—Mathayo 3:17; 1 Wakorintho 8:1.

MAMBO YA KUFANYA:

  • Uwe tayari kusikiliza wakati watoto wako wanataka kuzungumuza na wewe

  • Zungumuza na watoto wako kwa ukawaida, usizungumuze nao tu wakati kuna matatizo

2 TAFUTA KUELEWA WANATAKA KUSEMA NINI

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: “Anayetumia ufahamu katika jambo atapata mema.” (Methali 16:20) Wakati fulani, utahitaji kutafuta kujua ikiwa watoto wanataka kusema nini ao mawazo yao ni nini kabisa. Vijana wanazoea kutilia mambo chumvi ao kusema mambo yasiyokuwa kabisa katika moyo wao. “Yeyote anapojibu jambo kabla ya kulisikia, huo ni upumbavu na aibu kwake.” (Methali 18:13) Usiwe mutu wa kukasirika haraka-haraka.​—Methali 19:11.

Mama anakaripia mutoto yake mwanamuke

MAMBO YA KUFANYA:

  • Hata watoto waseme nini, epuka kuwakatiza ao kukasirika haraka-haraka

  • Jaribu kukumbuka namna ulikuwa unafikiri wakati ulikuwa na miaka yao na mambo ambayo ulikuwa unaona kuwa ya maana

3 MUWE NA UMOJA

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: ‘Mwana wangu, sikiliza nizamu ya baba yako, wala usiiache sheria ya mama yako.’ (Methali 1:8) Yehova amepatia baba na mama mamlaka juu ya watoto. Munapaswa kufundisha watoto wenu kuwaheshimu na kuwatii. (Waefeso 6:1-3) Watoto wanaweza kujua ikiwa wazazi wao ‘wameunganishwa vema katika akili ileile.’ (1 Wakorintho 1:10) Ikiwa haukubaliane na mwenzako, usifanye hivyo mbele ya watoto wako kwa sababu hilo linaweza kupunguza heshima yao kwenu.

Baba anamukaripia mutoto wake wakati mama anakaa na mutoto wao mwengine katika jumba lingine

MAMBO YA KUFANYA:

  • Zungumuza na ukubaliane na bibi ao bwana yako juu ya namna ya kuadibisha watoto

  • Ikiwa muna maoni tofauti juu ya kuwafundisha watoto wenu, kila mumoja ajaribu kufikiria maoni ya mwenzake

4 PANGA MAMBO

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: ‘Mulee muvulana [kijana] kulingana na njia inayomufaa.’ (Methali 22:6) Watoto wako watazoezwa vizuri ikiwa tu unafanya jambo fulani. Unapaswa kupanga namna utawazoeza watoto, na mazoezi hayo yanatia ndani nizamu. (Zaburi 127:4; Methali 29:17) Nizamu haimaanishe tu malipizi, lakini inamaanisha pia kuwasaidia watoto wako waelewe sababu gani sheria fulani zimewekwa. (Methali 28:7) Tena, uwafundishe kupenda Neno la Yehova na kufikiri juu ya kanuni zake. (Zaburi 1:2) Hilo litawasaidia kuwa na zamiri nzuri.​—Waebrania 5:14.

MAMBO YA KUFANYA:

  • Wasaidie watoto wako wamuone Mungu kuwa mutu halisi ambaye wanaweza kutumainia

  • Waonyeshe namna ya kutambua na kuepuka mambo yanayoweza kuhatarisha hali yao ya kiroho, kwa mufano kwenye Internete na adresi za Internete za kupashana habari. Wafundishe namna ya kuepuka watu wanaoweza kuwatendea vibaya kingono

Mutoto anazoezwa na baba yake namna ya kumutumikia Yehova kuanzia utoto mupaka ubatizo

‘Mulee muvulana [kijana] kulingana na njia inayomufaa’

YEHOVA ATABARIKI JITIHADA ZAKO

Ukiwa muzazi, una mugawo wa pekee wa kufundisha mutoto wako mawazo ya Yehova. (Waefeso 6:4) Yehova anajua kama hilo ni daraka nzito, lakini uwe hakika kama ikiwa unapata matokeo mazuri, hilo litamutukuza Mungu na utapata furaha kubwa.​—Methali 23:24.

JIULIZE . . .

  • Ninaweza kufanya nini ili mutoto wangu ajisikie huru kuzungumuza na mimi kuhusu jambo lolote?

  • Ninaweza kujifunza nini kutokana na namna wazazi wengine wanalea watoto wao?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine