SURA YA 7
Watu Wenye Elimu Ya Nyota Wanaenda Kumuona Yesu
WATU WENYE ELIMU YA NYOTA WANAFUATA “NYOTA” YENYE KUONGOZA YERUSALEMU NA KISHA KWENYE YESU IKO
Wanaume fulani wanakuja kutoka Mashariki. Ni wenye elimu ya nyota, ni kusema, wanaume wenye kujifunza mwendo wa nyota. Wanafanya hivyo kwa kuwaza kwamba, wataweza kufunua maana ya matukio katika maisha ya wanadamu. (Isaya 47:13) Wakati walikuwa nyumbani kwao huko Mashariki, waliona “nyota” na kuifuata kwenye mamia ya kilometre. Nyota hiyo haikuwaongoza Betlehemu, lakini Yerusalemu.
Wakati watu wenye elimu ya nyota wanafika Yerusalemu, wanauliza hivi: “Iko wapi ule mufalme wa Wayahudi mwenye alizaliwa? Kwa maana tuliona nyota yake wakati tulikuwa Mashariki, na tumekuja kuinama mbele yake.”—Matayo 2:1, 2.
Wakati Mufalme Herode wa Yerusalemu anasikia jambo hilo, anahangaika sana. Kwa hiyo, anawaita wakubwa wa makuhani na viongozi wengine wa dini ya Kiyahudi na kuwauliza mahali kwenye Kristo angepaswa kuzaliwa. Kwa kutumia Maandiko, wanamujibu hivi: “Katika Betlehemu.” (Matayo 2:5; Mika 5:2) Kisha kusikia hivyo, Herode anaita kwa siri watu hao wenye elimu ya nyota na kuwaambia hivi: “Muende na mutafute kwa uangalifu ule mutoto mudogo, na wakati mutamupata, muniletee habari ili mimi pia niende na kuinama mbele yake.” (Matayo 2:8) Kwa kweli, Herode anamutafuta mutoto huyo mudogo ili kumuua!
Kisha watu wenye elimu ya nyota kuondoka, jambo lenye kushangaza linatokea. “Nyota” yenye waliona wakati walikuwa Mashariki inaonekana mbele yao. Kwa kweli, nyota hiyo haiko ya kawaida, lakini imetayarishwa tu ili kuwaongoza. Wanaume hao wenye elimu ya nyota wanafuata nyota hiyo mupaka wakati inasimama juu ya nyumba kwenye Yosefu na Maria wako pamoja na mutoto wao mudogo.
Wakati wanaingia ndani ya nyumba, wanamuona Maria pamoja na mutoto mudogo, Yesu. Kwa hiyo, wanainama mbele ya Yesu. Na wanamupatia zawadi ya zahabu, ubani, na manemane. Kisha hapo, wakati wanakuwa karibu kurudia kwa Herode, Mungu anawaonya katika ndoto kama wasifanye hivyo. Kwa hiyo wanarudia katika inchi yao kupitia njia ingine.
Unawaza ni nani alitayarisha “nyota” hiyo yenye iliongoza watu wenye elimu ya nyota? Kumbuka kwamba nyota hiyo haikuwaongoza mara moja kwenye Yesu iko, ni kusema, Betlehemu. Lakini, iliwaongoza Yerusalemu, kwenye walikutana na Mufalme Herode mwenye alitaka kumuua Yesu. Na angefanya hivyo ikiwa Mungu hakutenda na kuonya wanaume hao wenye elimu ya nyota wasiambie Herode mahali kwenye Yesu alikuwa. Ni wazi kwamba, ni Shetani, adui wa Mungu, mwenye alipenda Yesu auawe, ndiye alitumia njia hiyo ili kujaribu kutimiza kusudi lake.