Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • jy sura 7 uku. 22-uku. 23 fu. 6
  • Watu Wenye Elimu ya Nyota Wanaenda Kumuona Yesu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Watu Wenye Elimu ya Nyota Wanaenda Kumuona Yesu
  • Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ni Nani Aliyeituma ile “Nyota”?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Yehova Alimulinda Yesu
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Wanakimbia Mutawala Mukali
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
jy sura 7 uku. 22-uku. 23 fu. 6
Watu wenye elimu ya nyota wanafuata nyota yenye kuwaongoza mahali kwenye Yosefu, Maria, na Yesu wanaishi

SURA YA 7

Watu Wenye Elimu Ya Nyota Wanaenda Kumuona Yesu

MATAYO 2:1-12

  • WATU WENYE ELIMU YA NYOTA WANAFUATA “NYOTA” YENYE KUONGOZA YERUSALEMU NA KISHA KWENYE YESU IKO

Wanaume fulani wanakuja kutoka Mashariki. Ni wenye elimu ya nyota, ni kusema, wanaume wenye kujifunza mwendo wa nyota. Wanafanya hivyo kwa kuwaza kwamba, wataweza kufunua maana ya matukio katika maisha ya wanadamu. (Isaya 47:13) Wakati walikuwa nyumbani kwao huko Mashariki, waliona “nyota” na kuifuata kwenye mamia ya kilometre. Nyota hiyo haikuwaongoza Betlehemu, lakini Yerusalemu.

Wakati watu wenye elimu ya nyota wanafika Yerusalemu, wanauliza hivi: “Iko wapi ule mufalme wa Wayahudi mwenye alizaliwa? Kwa maana tuliona nyota yake wakati tulikuwa Mashariki, na tumekuja kuinama mbele yake.”—Matayo 2:1, 2.

Watu wenye elimu ya nyota wanainama mbele ya Mufalme Herode

Wakati Mufalme Herode wa Yerusalemu anasikia jambo hilo, anahangaika sana. Kwa hiyo, anawaita wakubwa wa makuhani na viongozi wengine wa dini ya Kiyahudi na kuwauliza mahali kwenye Kristo angepaswa kuzaliwa. Kwa kutumia Maandiko, wanamujibu hivi: “Katika Betlehemu.” (Matayo 2:5; Mika 5:2) Kisha kusikia hivyo, Herode anaita kwa siri watu hao wenye elimu ya nyota na kuwaambia hivi: “Muende na mutafute kwa uangalifu ule mutoto mudogo, na wakati mutamupata, muniletee habari ili mimi pia niende na kuinama mbele yake.” (Matayo 2:8) Kwa kweli, Herode anamutafuta mutoto huyo mudogo ili kumuua!

Kisha watu wenye elimu ya nyota kuondoka, jambo lenye kushangaza linatokea. “Nyota” yenye waliona wakati walikuwa Mashariki inaonekana mbele yao. Kwa kweli, nyota hiyo haiko ya kawaida, lakini imetayarishwa tu ili kuwaongoza. Wanaume hao wenye elimu ya nyota wanafuata nyota hiyo mupaka wakati inasimama juu ya nyumba kwenye Yosefu na Maria wako pamoja na mutoto wao mudogo.

Watu wenye elimu ya nyota ambao walifuata nyota mupaka Betlehemu wanapatia Maria na Yesu zawadi

Wakati wanaingia ndani ya nyumba, wanamuona Maria pamoja na mutoto mudogo, Yesu. Kwa hiyo, wanainama mbele ya Yesu. Na wanamupatia zawadi ya zahabu, ubani, na manemane. Kisha hapo, wakati wanakuwa karibu kurudia kwa Herode, Mungu anawaonya katika ndoto kama wasifanye hivyo. Kwa hiyo wanarudia katika inchi yao kupitia njia ingine.

Unawaza ni nani alitayarisha “nyota” hiyo yenye iliongoza watu wenye elimu ya nyota? Kumbuka kwamba nyota hiyo haikuwaongoza mara moja kwenye Yesu iko, ni kusema, Betlehemu. Lakini, iliwaongoza Yerusalemu, kwenye walikutana na Mufalme Herode mwenye alitaka kumuua Yesu. Na angefanya hivyo ikiwa Mungu hakutenda na kuonya wanaume hao wenye elimu ya nyota wasiambie Herode mahali kwenye Yesu alikuwa. Ni wazi kwamba, ni Shetani, adui wa Mungu, mwenye alipenda Yesu auawe, ndiye alitumia njia hiyo ili kujaribu kutimiza kusudi lake.

  • Ni nini inaonyesha kama “nyota” yenye wanaume wenye elimu ya nyota waliona haikuwa ya kawaida?

  • Mutoto mudogo Yesu iko wapi wakati watu wenye elimu ya nyota wanamupata?

  • Sababu gani tunaweza kusema kama ni Shetani ndiye aliongoza watu wenye elimu ya nyota?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine