Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • jy sura 23 uku. 60-uku. 61 fu. 5
  • Yesu Anafanya Miujiza Katika Kapernaumu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yesu Anafanya Miujiza Katika Kapernaumu
  • Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Utumishi Wake Unapanuka Katika Galilaya
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Yesu Anaponyesha Kijana Mwanaume Mwenye Kuwa na Pepo Muchafu
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
jy sura 23 uku. 60-uku. 61 fu. 5
Wagonjwa wanajikusanya kwa Petro, na Yesu anawaponyesha

SURA YA 23

Yesu Anafanya Miujiza Katika Kapernaumu

MATAYO 8:14-17 MARKO 1:21-34 LUKA 4:31-41

  • YESU ANAFUKUZA PEPO MUCHAFU

  • MAMA-MUKWE WA PETRO ANAPONYESHWA

Yesu amealika wanafunzi ine, ni kusema, Petro, Andrea, Yakobo, na Yohana, ili wakuwe wavuvi wa watu. Sasa, kwenye siku ya Sabato, wote wanaenda kwenye sinagogi ya Kapernaumu. Yesu anafundisha katika sinagogi, na tena watu wanashangazwa na namna yake ya kufundisha. Hafundishe kama waandishi, lakini anafundisha kama mutu mwenye kuwa na mamlaka.

Siku hii ya Sabato, kuko mwanaume mumoja mwenye kuwa chini ya nguvu za pepo muchafu. Katika sinagogi, mwanaume huyo analalamika kwa sauti kubwa: “Tuko na shida gani na wewe, Yesu Munazareti? Je, umekuja kutuharibu? Ninajua kabisa wewe ni nani, Mutakatifu wa Mungu!” Yesu anakemea pepo muchafu mwenye kuwa ndani ya mwanaume huyo kwa kusema hivi: “Nyamaza, na umutoke!”—Marko 1:24, 25.

Kwa hiyo, roho huyo muovu anaangusha mwanaume huyo chini kwa kumutikisa-tikisa na kufanya makelele kwa sauti yake yote. Lakini ule pepo muchafu anamutoka mwanaume huyo “bila kumuumiza.” (Luka 4:35) Watu wenye kuwa katika sinagogi wanashangaa sana! Wanauliza, “Ni jambo gani hili? Ni fundisho mupya! Anaamuru kwa mamlaka hata roho wachafu, na wanamutii.” (Marko 1:27) Ni wazi kwamba tukio hili lenye kushangaza linajulikana katika Galilaya yote.

Wakati Yesu na wanafunzi wake wanatoka katika sinagogi, wanaenda kwa Simoni, ao Petro. Huko, mama-mukwe wa Petro ni mugonjwa sana; iko na homa kali. Wanamuomba Yesu amusaidie. Kwa hiyo, Yesu anamuendea, anamukamata kwenye mukono, na kumusimamisha. Palepale anapona na anaanza kutumikia Yesu na wanafunzi wenye walikuwa pamoja naye, pengine kwa kuwatayarishia chakula.

Wakati jua linashuka, watu wa maeneo mbalimbali wanakuja nyumbani kwa Petro na wagonjwa wao. Kisha muda kidogo inaonekana kuwa watu wa muji wote wamekutana kwenye mulango. Juu ya nini? Wanapenda wapone. Kwa kweli, ‘wote wenye walikuwa na watu wenye kuteswa na magonjwa mbalimbali wanawaleta kwake. Anawaponyesha kwa kuweka mikono yake juu ya kila mugonjwa.’ (Luka 4:40) Ndiyo, hata kama wako na magonjwa ya namna gani, Yesu anawasaidia, kama vile tu ilitabiriwa. (Isaya 53:4) Anafanya hata wale wenye kuwa chini ya nguvu za pepo wachafu wakuwe huru. Wakati roho waovu wanatoka, wanasema kwa sauti kubwa: “Wewe ndiye Mwana wa Mungu.” (Luka 4:41) Lakini Yesu anawakemea na hawaruhusu kusema tena. Wanajua kuwa Yesu ndiye Kristo, na kuwa hapendi waonyeshe kama vile wako wanamutumikia Mungu wa kweli.

KUINGIWA NA PEPO MUCHAFU

Wakati pepo wachafu walikuwa wanaingia mutu fulani, walikuwa wanatesa sana mutu huyo. (Matayo 17:14-18) Lakini kisha kuachiliwa huru na pepo hao wachafu, akili na hali ya kimwili ya mutu huyo vilirudia kama kawaida. Mara kwa mara, Yesu alionyesha uwezo wake wa kufukuza pepo wachafu kupitia roho takatifu ya Mungu.—Luka 8:39; 11:20.

  • Katika Kapernaumu, ni jambo gani linafanyika siku ya Sabato kwenye sinagogi?

  • Yesu anaenda wapi wakati anatoka kwenye sinagogi, na anafanya nini huko?

  • Watu wa muji wanatenda namna gani juu ya mambo yenye Yesu amefanya katika muji wao?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine