Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • jy sura 29 uku. 72-uku. 73 fu. 8
  • Mutu Anaweza Kufanya Matendo ya Muzuri Siku ya Sabato?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mutu Anaweza Kufanya Matendo ya Muzuri Siku ya Sabato?
  • Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Aliwapenda Watu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
jy sura 29 uku. 72-uku. 73 fu. 8
Yesu anazungumuza na mwanaume mugonjwa pembeni ya kiziwa cha maji cha Betzata

SURA YA 29

Mutu Anaweza Kufanya Matendo Ya Muzuri Siku Ya Sabato?

YOHANA 5:1-16

  • YESU ANAHUBIRI KATIKA YUDEA

  • ANAPONYESHA MWANUME MWENYE KUGONJWA KWENYE KIZIWA CHA MAJI

Yesu amefanya mambo mengi wakati wa utumishi wake katika Galilaya. Lakini, wakati anasema, “Ni lazima pia nitangaze habari njema ya Ufalme wa Mungu katika miji mingine,” Yesu anafikiria maeneo mengine zaidi ya Galilaya. Kwa hiyo, anaenda “kuhubiri katika masinagogi ya Yudea.” (Luka 4:43, 44) Hilo linafaa kwa sababu sasa ni kipindi cha kuchipuka kwa majani na siku ya sherehe katika Yerusalemu inakaribia.

Wakati tunalinganisha mambo yenye tulisoma juu ya utumishi wa Yesu katika Galilaya na yale anafanya katika Yudea, tunaona kuwa Injili zinatoa habari kidogo juu ya kazi ya Yesu katika Yudea. Hata kama watu wengi katika Yuda hawapendezwe, hilo halimuzuie Yesu kuhubiri kwa bidii na kufanya matendo ya muzuri kila mahali kwenye anapatikana.

Sasa Yesu anaenda katika Yerusalemu, muji mukubwa wa Yudea, kwa ajili ya Pasaka ya mwaka wa 31 wakati wetu. Katika nafasi kwenye watu wengi wanapatikana karibu na Mulango wa Kondoo, kuko kiziwa kikubwa cha maji chenye kuzungukwa na nguzo chenye kuitwa Betzata. Wagonjwa wengi, vipofu, na vilema wanakuja kwenye kiziwa hicho. Sababu gani? Kwa sababu watu wanazoea kuamini kuwa mutu anaweza kuponyeshwa ikiwa anaingia katika kiziwa wakati maji yanavurugwa.

Sasa ni siku ya Sabato, na Yesu anaona mwanaume fulani kwenye kiziwa hicho mwenye amekuwa mugonjwa kwa miaka 38. Yesu anamuuliza hivi: “Je, unataka kupona?” Mwanaume huyo anajibu hivi: “Bwana, sina mutu wa kuniweka ndani ya kiziwa cha maji wakati maji yanavurugwa, lakini wakati ninakuja, mutu mwingine anaingia mbele yangu.”—Yohana 5:6, 7.

Yesu anasema jambo fulani lenye linapaswa kushangaza mwanaume huyo na mutu yeyote mwenye angelisikia: “Simama! Kamata kitanda chako na utembee.” (Yohana 5:8) Na mwanaume huyo anafanya kabisa hivyo. Kisha tu kuponyeshwa, mwanaume huyo anakamata kitanda chake na anaanza kutembea!

Wayahudi wanazungumuza na mwanaume mwenye Yesu aliponyesha

Kuliko kufurahi juu ya jambo la muzuri sana lenye limefanyika, Wayahudi wanaona mwanaume huyo na kumuhukumu kwa kusema: “Ni Sabato, na hauruhusiwe kubeba kitanda.” Mwanaume huyo anawajibu hivi: “Ule mwenye aliniponyesha aliniambia, ‘Kamata kitanda chako na utembee.’” (Yohana 5:10, 11) Wayahudi hao wanaona kuwa haifae kuponyesha watu siku ya Sabato.

Wanapenda kujua; kwa hiyo wanamuuliza hivi: “Ni nani ule mwenye alikuambia, ‘Ukikamate na utembee’?” Sababu gani wanauliza mwanaume huyo ulizo hilo? Kwa sababu Yesu “alikuwa amepotea katikati ya watu wengi,” na mwanaume mwenye ameponyeshwa hajue jina la Yesu. (Yohana 5:12, 13) Lakini mwanaume huyo atakutana tena na Yesu. Kisha, katika hekalu, mwanaume huyo anakutana na Yesu na anapata nafasi ya kujua mutu mwenye alimuponyesha kwenye kiziwa cha maji.

Mwanaume mwenye aliponyeshwa anakutana na Wayahudi wenye walimuuliza ni nani mwenye alimuponyesha. Anawaambia kama ni Yesu. Wakati wanajua jambo hilo, Wayahudi wanaenda kumuona Yesu. Je, wanaenda ili kujua ni kupitia njia gani Yesu iko na uwezo wa kufanya mambo hayo ya ajabu? Hapana. Lakini, wanaenda ili kumuonyesha Yesu kama amefanya kosa kwa kufanya mambo ya muzuri siku ya Sabato. Na wanaanza hata kumutesa!

  • Sababu gani Yesu anaenda katika Yudea, na ni mambo gani anaendelea kufanya?

  • Sababu gani watu wengi wanaenda kwenye kiziwa cha maji chenye kuitwa Betzata?

  • Yesu anafanya muujiza gani kwenye kiziwa cha maji, na Wayahudi fulani wanatenda namna gani?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine