Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • jy sura 38 uku. 96-uku. 97 fu. 7
  • Yohana Anapenda Kupata Habari Juu ya Yesu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yohana Anapenda Kupata Habari Juu ya Yesu
  • Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Yesu Anaongezeka na Yohana Anapunguka
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Yohana Mubatizaji​—Mufano Wake Unaweza Kutusaidia Tuendelee Kuwa na Furaha
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • Yesu Kristo Ni Nani?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Yesu Kristo Ni Nani?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
Ona Habari Zaidi
Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
jy sura 38 uku. 96-uku. 97 fu. 7
Yohana Mubatizaji anakaa katika gereza peke yake

SURA YA 38

Yohana Anapenda Kupata Habari Juu Ya Yesu

MATAYO 11:2-15 LUKA 7:18-30

  • YOHANA MUBATIZAJI ANAULIZA JUU YA DARAKA LA YESU

  • YESU ANAMUSIFU YOHANA

Yohana Mubatizaji amekuwa katika gereza kumepita karibu mwaka moja. Lakini, iko anapata habari juu ya miujiza yenye Yesu iko anafanya. Waza namna Yohana anajisikia wakati wanafunzi wake wanamuambia kama Yesu amefufua mutoto wa mujane katika muji wa Naini. Hata hivyo, Yohana anapenda Yesu mwenyewe amuambie maana ya mambo yote hayo. Kwa hiyo, Yohana anatuma wawili kati ya wanafunzi wake. Ili wafanye nini? Wanapaswa kumuuliza Yesu hivi: “Wewe ndiye Ule Mwenye Anakuja, ao tungojee mwingine?”—Luka 7:19.

Je, hilo linaonekana kuwa ulizo lenye kushangaza? Yohana ni mwanaume mwaminifu mwenye, wakati alibatiza Yesu kumepita karibu miaka mbili, aliona roho ya Mungu inashuka juu ya Yesu na alisikia sauti ya Mungu yenye kutangaza kuwa amemukubali Yesu. Hatuna sababu za kufikiri kuwa imani ya Yohana imekuwa zaifu. Kama ilikuwa hivyo, Yesu hangemusifu Yohana, kama vile anamusifu wakati huu. Lakini ikiwa Yohana angali na imani, sababu gani anauliza ulizo hilo juu ya Yesu?

Pengine Yohana anapenda tu Yesu mwenyewe amuhakikishie kuwa yeye ndiye Masiya. Hilo lingemutia Yohana nguvu wakati anaendelea kuteseka katika gereza. Na ulizo la Yohana linaonekana kuwa na maana ingine. Anajua muzuri unabii mbalimbali wa Biblia wenye kuonyesha kuwa Mutiwa-Mafuta wa Mungu anapaswa kuwa mufalme na mukombozi. Lakini, Yohana iko katika gereza kumepita miezi mingi kisha yeye kumubatiza Yesu. Kwa hiyo, Yohana iko anauliza ikiwa kuko mwingine mwenye iko anakuja, mwenye atachukua nafasi ya Yesu na kutimiza mambo yote yenye yalitabiriwa kuwa Masiya atatimiza.

Mwanaume kilema na mwanamuke kipofu wanafurahi kisha Yesu kuwaponyesha

Kuliko tu kuambia wanafunzi wa Yohana kuwa, ‘Ndiyo kabisa, ni mimi ndiye Ule mwenye anapaswa kuja,’ Yesu anatoa ushuhuda kuwa anategemezwa na Mungu kwa kuponyesha watu wengi wenye kuwa na magonjwa na ulemavu mbalimbali. Kisha anaambia wanafunzi hivi: “Muende na mumuelezee Yohana mambo yenye munasikia na kuona: Sasa vipofu wanaona, vilema wanatembea, wenye ukoma wanafanywa kuwa safi, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanatangaziwa habari njema.”—Matayo 11:4, 5.

Wakati anauliza ulizo hilo, pengine Yohana anatazamia kuwa Yesu atafanya mambo mengi zaidi kupita yale yenye iko anafanya sasa na kuwa pengine atamukomboa kutoka katika gereza. Lakini, Yesu anapenda kusema kuwa Yohana asitazamie zaidi ya miujiza yenye iko anafanya.

Wakati wanafunzi wa Yohana wanatoka, Yesu anaambia watu kuwa Yohana ni mutu mwenye kupita nabii. Ni “mujumbe” wa Yehova mwenye alitabiriwa katika Malaki 3:1. Yeye pia ni nabii Eliya, mwenye alitabiriwa katika Malaki 4:5, 6. Yesu anaeleza hivi: “Kwa kweli ninawaambia ninyi, kati ya wale wenye walizaliwa na wanamuke, hakujatokea mutu yeyote mukubwa kuliko Yohana Mubatizaji, lakini mutu mwenye ni mudogo zaidi katika Ufalme wa mbinguni ni mukubwa kuliko yeye.”—Matayo 11:11.

Wakati Yesu anasema kama mutu mwenye kuwa mudogo zaidi katika Ufalme wa mbinguni ni mukubwa kuliko Yohana, Yesu iko anaonyesha kuwa Yohana hatakuwa katika Ufalme wa mbinguni. Yohana alitayarishia Yesu njia lakini alikufa mbele Kristo afungue njia ya kuenda mbinguni. (Waebrania 10:19, 20) Lakini Yohana, ni nabii muaminifu wa Mungu na ataishi katika dunia kama raia wa Ufalme wa Mungu.

  • Sababu gani Yohana anauliza ikiwa Yesu ndiye Ule Mwenye anapaswa kuja ao ikiwa inaomba kungojea mwingine?

  • Yesu anasema kuwa Yohana Mubatizaji anatimiza unabii gani mbalimbali?

  • Sababu gani Yohana hatakuwa na Yesu mbinguni?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine