Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • jy sura 47 uku. 118-uku. 119 fu. 6
  • Mutoto Mwanamuke Anaishi Tena!

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mutoto Mwanamuke Anaishi Tena!
  • Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Yesu Anafanya Miujiza Mingi
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Anaponyeshwa kwa Kugusa Nguo ya Yesu
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Anafanya Miujiza, Lakini Anakataliwa Hata Katika Nazareti
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Kifo Si Mwisho wa Mambo Yote!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
jy sura 47 uku. 118-uku. 119 fu. 6
Yesu anafufua binti ya Yairo

SURA YA 47

Mutoto Mwanamuke Anaishi Tena!

MATAYO 9:18, 23-26 MARKO 5:22-24, 35-43 LUKA 8:40-42, 49-56

  • YESU ANAFUFUA BINTI YA YAIRO

Yairo anaona kuwa Yesu ameponyesha mwanamuke mwenye alikuwa na ugonjwa wa kutokwa damu. Bila shaka, Yesu anaweza kusaidia mutoto wake pia, hata kama Yairo anafikiri kuwa ‘kufikia sasa mutoto wake mwanamuke atakuwa amekufa.’ (Matayo 9:18) Inawezekana kabisa Yesu asaidie mutoto huyo?

Wakati Yesu angali anazungumuza na mwanamuke mwenye ameponyesha, wanaume fulani wanakuja kutoka nyumbani kwa Yairo na kumuambia Yairo hivi: “Binti yako amekufa!” Wanaongeza hivi: “Sababu gani uendelee kumusumbua Mwalimu?”—Marko 5:35.

Hiyo ni habari yenye kuhuzunisha sana! Mwanaume huyo, mwenye watu wanaheshimia sana, anavunjika moyo sana. Binti yake mumoja tu amekufa. Lakini, Yesu anasikia habari hiyo, na anamuangalia Yairo na kumuambia kwa maneno yenye kutia moyo: “Usiogope, ukuwe tu na imani.”—Marko 5:36.

Watu wenye kulia wako pembeni ya kitanda kwenye kuko mutoto wa Yairo ambaye amekufa

Kisha Yesu anaenda na Yairo nyumbani kwake. Wakati wanafika, wanakuta muvurugo mwingi. Watu wenye kuwa nyumbani kwa Yairo wako wanalia, na kujipiga-piga kwa huzuni. Yesu anaingia ndani ya nyumba na kusema maneno haya yenye kushangaza: “Mutoto hakukufa lakini amelala usingizi.” (Marko 5:39) Wakati watu wanasikia hivyo, wanamucheka Yesu. Wanajua kama mutoto huyo tayari amekufa. Lakini, kwa kutumia mamlaka yenye Mungu amemupatia, Yesu ataonyesha kuwa inawezekana watu wafufuliwe kama vile tu wanaweza kuamushwa wakati wamelala usingizi muzito.

Sasa Yesu anatosha watu wote inje, lakini anaacha tu Petro, Yakobo, Yohana, na wazazi wa mutoto mwenye amekufa. Yesu anaenda na watu hao tano mahali kwenye mutoto huyo mwanamuke alikuwa amelala. Anamukamata kwenye mukono na kumuambia: “‘Talita kumi,’ maneno yenye wakati yanatafsiriwa yanamaanisha: ‘Mutoto mwanamuke, ninakuambia, “Simama!”’” (Marko 5:41) Mara moja, mutoto huyo anasimama na kuanza kutembea. Wazia namna Yairo na bibi yake wanafurahi wakati wanaona jambo hilo! Ili kuwahakikishia kuwa mutoto anaishi kabisa, Yesu anawaambia wamupatie kitu fulani cha kula.

Katika miujiza mingine yenye Yesu alifanya mbele ya hapo, aliambia watu wenye aliponyesha wasitangaze mambo yenye amefanya; anaambia wazazi hawa hivyohivyo. Hata hivyo, wazazi hao wenye furaha sana na watu wengine wanatangaza habari hiyo “katika eneo hilo lote.” (Matayo 9:26) Ni wazi kwamba, ikiwa unaona mutu mwenye unapenda anafufuliwa, utakuwa kabisa na furaha ya kuambia wengine juu ya jambo hilo, haiko vile? Huu ndio ufufuo wa pili wenye Yesu anafanya wenye umeandikwa katika vitabu vya Injili.

  • Yairo anapata habari gani, na namna gani Yesu anamutia moyo?

  • Hali iko namna gani wakati Yesu na Yairo wanafika nyumbani kwa Yairo?

  • Sababu gani Yesu anasema kuwa mutoto ni mwenye kulala tu usingizi?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine