Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • jy sura 92 uku. 216-uku. 217 fu. 7
  • Watu Kumi Wenye Ukoma Wanaponyeshwa​—⁠Mumoja Anaonyesha Shukrani

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Watu Kumi Wenye Ukoma Wanaponyeshwa​—⁠Mumoja Anaonyesha Shukrani
  • Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Yesu Anafanya Miujiza Mingi
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • “Mjionyeshe Kuwa Wenye Shukrani”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Anaponyesha Mutu Mwenye Ukoma kwa Huruma
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Ulijua?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
jy sura 92 uku. 216-uku. 217 fu. 7
Mumoja kati ya wale watu kumi wenye Yesu anaponyesha ukoma anarudia kumushukuru

SURA YA 92

Watu Kumi Wenye Ukoma Wanaponyeshwa —Mumoja Anaonyesha Shukrani

LUKA 17:11-19

  • YESU ANAPONYESHA WATU KUMI WENYE UKOMA

Ili kuvuruga mipango ya Sanhedrini ya kutaka kumuua, Yesu anaenda katika muji wa Efraimu, wenye kuwa ngambo ya kaskazini mashariki mwa Yerusalemu. Anabakia kule na wanafunzi wake, mbali na maadui wake. (Yohana 11:54) Lakini Pasaka ya mwaka wa 33 wakati wetu ni yenye kukaribia, kwa hiyo Yesu anaanza tena safari. Anapita katika Samaria, ngambo ya kaskazini na anapanda mupaka Galilaya, hii ni mara yake ya mwisho kutembelea sehemu hii mbele ya kifo chake.

Wakati Yesu anaanza safari yake, kutoka muji mumoja mupaka muji mwengine, anakutana na wanaume kumi wenye ukoma. Namna fulani ya ukoma inaweza kufanya sehemu za mwili ziharibike pole pole, kama vile sehemu za vidole vya mikono na vya miguu, ao masikio. (Hesabu 12:10-12) Sheria ya Mungu inasema kuwa mutu mwenye ukoma anapaswa kusema kwa sauti kubwa, “Mimi siko safi, mimi siko safi!” na kuwa anapaswa kujitenga na watu wengine.—Mambo ya Walawi 13:45, 46.

Kwa hiyo, wale wenye ukoma wanasimama mbali na Yesu. Lakini wanasema hivi kwa sauti kubwa: “Yesu, Mwalimu, utusikilie huruma!” Wakati anaona watu hao wenye ukoma, Yesu anawatolea muongozo huu: “Muende mujionyeshe kwa makuhani.” (Luka 17:13, 14) Kwa kufanya hivyo anaonyesha kwamba anatii Sheria ya Mungu, yenye inaruhusu makuhani kutangaza kwamba watu wenye walikuwa na ukoma wamepona na wako sasa safi. Kwa hiyo, wanaweza kuishi tena pamoja na watu wenye kuwa na afya ya muzuri.—Mambo ya Walawi 13:9-17.

Yesu anakutana na wanaume kumi wenye ukoma

Watu hao kumi wenye ukoma wanatumainia uwezo wa Yesu wa kufanya miujiza. Wanaenda kuonana na makuhani, mbele hata waponyeshwe. Wakati wako katika njia, imani yao katika Yesu inabarikiwa. Wanaanza kuona na kujisikia kwamba wamepona!

Watu kenda kati ya wale kumi wenye wameponyeshwa ukoma wanaendelea na njia yao. Lakini mumoja haendelee. Huyu mwanaume, Musamaria, anarudia kumutafuta Yesu. Sababu gani? Anamushukuru sana Yesu kwa kuona mambo yenye yametokea. Mutu huyu mwenye alikuwa na ukoma ‘anamutukuza Mungu kwa sauti kubwa,’ kwa sababu anatambua kama ni Mungu ndiye alimuponyesha. (Luka 17:15) Wakati anamuona Yesu, anaanguka mbele yake, na kumushukuru.

Yesu anaambia hivi watu wenye kumuzunguka: “Wote kumi (10) walitakaswa, haiko vile? Basi, wale wengine kenda (9) wako wapi? Je, hakuna mwingine mwenye alirudia ili kutukuza Mungu isipokuwa mutu huyu wa taifa lingine?” Kisha Yesu anamuambia ule Musamaria: “Simama uende; imani yako imekuponyesha.”—Luka 17:17-19.

Kwa kuwaponyesha watu kumi wenye ukoma, Yesu anaonyesha kama Yehova anamuunga mukono. Sasa mumoja kati ya wale kumi haponyeshwe tu, lakini pengine iko kwenye njia ya uzima. Hatuishi wakati huo wenye Mungu anamutumia Yesu ili kufanya miujiza kama hiyo. Lakini kwa kumuamini Yesu, tunaweza kuwa kwenye njia ya uzima, ni kusema, uzima wa milele. Je, tunaonyesha kama sisi ni wenye shukrani, kama vile ule Musamaria alifanya?

  • Ili kuvuruga mipango ya kumuua, Yesu anafanya safari ya kuenda wapi?

  • Sababu gani watu kumi wenye ukoma walisimama mbali, na sababu gani Yesu anawaambia waende kuonana na makuhani?

  • Kupitia jambo lenye lilimupata Musamaria, tunapaswa kufikiria nini?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine