Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • jy sura 129 uku. 294-uku. 295 fu. 2
  • Pilato Anasema: “Muangalie! Mwanaume!”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Pilato Anasema: “Muangalie! Mwanaume!”
  • Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Pilato na Herode Wanaona Kuwa Yesu Hana Kosa
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Yesu Anatolewa na Anapelekwa ili Auawe
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Yesu Anakufa Kule Golgota
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Sanhedrini Inamusambisha, Kisha Anapelekwa kwa Pilato
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
jy sura 129 uku. 294-uku. 295 fu. 2
Yesu anavaa, taji la miiba na nguo ya zambarau, Pilato anamuleta inje

SURA YA 129

Pilato Anasema: “Muangalie! Mwanaume!”

MATAYO 27:15-17, 20-30 MARKO 15:6-19 LUKA 23:18-25 YOHANA 18:39–19:5

  • PILATO ANAJARIBU KUMUACHILIA YESU

  • WAYAHUDI WANAOMBA BARABA AACHILIWE

  • YESU ANACHEKELEWA NA KUTENDEWA MUBAYA

Pilato anaambia hivi kikundi cha watu wenye wanapenda kumuua Yesu: “Sikupata jambo lolote lenye kuhakikisha mashitaka yenye munaleta juu yake. Kwa kweli, hata Herode hakupata jambo lolote.” (Luka 23:14, 15) Sasa, ili kujaribu kumulinda Yesu, Pilato anatumia njia ingine kwa kuambia watu hivi: “Muko na desturi kwamba niwafungulie mutu mumoja siku ya Pasaka. Basi, munataka niwafungulie Mufalme wa Wayahudi?”—Yohana 18:39.

Pilato anajua kama kuko mufungwa mumoja mwenye anaitwa Baraba, mwenye anajulikana kuwa mwizi, mwenye kuleta muvurugo, na muuaji. Kwa hiyo, Pilato anawaambia hivi: “Munataka niwafungulie nani, Baraba ao Yesu mwenye kuitwa Kristo?” Kwa sababu wanachochewa na wakubwa wa makuhani, watu wanaomba Baraba afunguliwe, hapana Yesu. Pilato anawauliza tena hivi: “Munataka niwafungulie nani kati ya hawa wawili?” Watu hao wanalalamika hivi: “Baraba”!—Matayo 27:17, 21.

Pilato anahuzunika, na anawauliza hivi: “Basi, nifanye nini na Yesu mwenye kuitwa Kristo?” Watu wanalalamika hivi: “Auawe kwenye muti!” (Matayo 27:22) Bila haya, wanaomba mutu mwenye hana kosa auawe. Pilato anawauliza hivi: “Sababu gani? Mutu huyu amefanya jambo gani la mubaya? Mimi sikuona ndani yake jambo lolote lenye linafanya astahili kifo; kwa hiyo nitamupatia azabu kisha nitamufungua.”—Luka 23:22.

Hata kama Pilato anajikaza sana, watu hao wenye hasira wanalalamika hivi kwa sauti moja: “Auawe kwenye muti!” (Matayo 27:23) Viongozi wa dini wamechochea kikundi hicho kikuwe na hasira kali mupaka kinapenda kumwanga damu ya mutu! Na haiko damu ya mutu mwenye alifanya makosa makubwa, ao ya muuaji fulani. Ni damu ya mutu mwenye hana kosa mwenye walikaribisha katika Yerusalemu kama Mufalme siku tano zenye zilikuwa zimepita. Ikiwa wanafunzi wa Yesu wako pale, wanabakia kimya na bila kujionyesha.

Pilato anaona kuwa watu hawakubali maombi yake. Muvurugo unaanza, kwa hiyo, anakamata maji na ananawa mikono yake mbele ya macho ya watu hao. Anawaambia hivi: “Damu ya mutu huyu haiko juu ya kichwa changu. Ile ni mambo yenu wenyewe.” Hata hivyo, hilo halibadilishe mawazo yao. Lakini wanasema hivi: “Damu yake ikuwe juu yetu na juu ya watoto wetu.”—Matayo 27:24, 25.

Gavana anapenda kuwafurahisha watu hao kuliko kufanya jambo lenye anajua kuwa ni sawa. Pilato anakubali ombi la watu, na anamuachilia Baraba. Anaamuru Yesu atoshwe manguo na kupigwa.

Kisha kumupiga mubaya sana, maaskari wanamupeleka Yesu katika nyumba ya gavana. Kikundi cha maaskari kinakusanyika na kumupiga tena kwa mijeledi. Wanatengeneza taji la miiba na kumuvalisha taji hilo kwenye kichwa. Pia maaskari wanatia katika mukono wa kuume wa Yesu utete na kumuvalisha nguo ya murefu ya rangi nyekundu, kama ile yenye wafalme wanavaa. Wanamuambia hivi kwa zarau: “Jambo, wewe Mufalme wa Wayahudi!” (Matayo 27:28, 29) Zaidi ya hilo, wanamutemea Yesu mate na kuendelea kumupiga makofi katika sura. Kisha wanakamata utete wenye uko katika mikono yake, wanautumia ili kumupiga kwenye kichwa, na kufanya “taji” la miiba la kumupatisha haya liingie zaidi katika kichwa chake.

Yesu anajiendesha kwa heshima na anabakia imara wakati wanamufanyia mambo hayo yote, hilo linamushangaza Pilato mupaka anajaribu tena kujionyesha kuwa hana kosa, anasema hivi: “Muone! Ninamuleta inje kwenu ili mujue kwamba sione kosa lolote ndani yake.” Je, Pilato anawaza kuwa kumuleta Yesu sasa akiwa mwenye kuumia na kutokwa damu kunaweza kufanya watu hao wabadilishe mawazo yao? Wakati Yesu anasimama mbele ya watu hao wenye hawana huruma, Pilato anasema hivi: “Muangalie! Mwanaume!”—Yohana 19:4, 5.

Hata kama Yesu ni mwenye kuumia anajiendesha kwa heshima na kwa utulivu mupaka hata Pilato anatambua jambo hilo, kwa sababu maneno yake yanaonekana kuwa yenye heshima na huruma.

KUPIGWA MIJELEDI

Fimbo ya mijeledi

Katika gazeti lake, doktere William Edwards anaeleza zoea la Waroma la kupiga watu mijeledi:

“Kwa kawaida kifaa chenye walizoea kutumia ni kiboko kifupi (flagramu ao flagelamu) chenye kamba nyingi za ngozi, mojamoja ao zenye kusukwa zenye kuwa na urefu mbalimbali, zenye zilifungwa ndani kwenye sehemu ya mwisho-mwisho vipande vidogo-vidogo vya chuma ao vya mifupa yenye kuchongoka ya kondoo. . . . Wakati maaskari Waroma walimupiga tena na tena mufungwa kwenye mugongo kwa nguvu sana, vile vipande vya chuma vingechubua sana, na zile kamba za ngozi na mifupa ya kondoo vingekata ngozi na sehemu zenye kuwa chini ya ngozi. Kisha, wakati waliendelea kumupiga mijeledi, vidonda vilipasuka mupaka kufikia kwenye misuli na kutokeza nyuzinyuzi zenye kuninginia za minofu yenye kutoka damu.” (The Journal of the American Medical Association)

  • Namna gani Pilato anajaribu kumuachilia Yesu, na kwa hiyo kujionyesha kuwa hana kosa?

  • Kupigwa mijeledi kulitia ndani nini?

  • Kisha Yesu kupigwa mijeledi, namna gani anatendewa tena mubaya?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine